Mtalii,
Sasa naanza kushawishika na waliosema wewe ndiye Chinga. Kama hivyo ndivyo karibu sana ndugu yangu. Naona hujatia neno katika hoja nilizitoa kuhusu chopper. Nadhani sasa naweza kuendelea na hoja zingine.
Ila umeendelea kusisitiza uwongo(huwa sipendi kutumia neno hili) kwamba Mbowe alikuwepo Moshi kutoa misaada. Nimekwambia Mbowe hakuwepo Moshi wakati ule, misaada ilitolewa kwa niaba ya Grace Kiwelu(MB), gazeti liliripoti vibaya. Sasa kukanusha au kutokanusha hilo ni suala lingine na hasa ukizingatia habari imepita muda kidogo. Unaweza kuwasiliana na muandishi wa habari hiyo Ali Sonda 0784 329429 kwa ufafunuzi au wasiliana na gazeti husika.
Mbowe amerudi Tanzania hivi karibuni kwa ajili ya ziara zinazoanza kesho. Raha ya mijadala ni watu kukubali ukweli sio kuendelea kung'ang'ania uwongo la sivyo maana ya majadiliano inapotea!
Mkandara na DrWHO
Maswali yaliyoulizwa si magumu ila ni mengi yanayohitaji muda kuyajadili. Sasa kuna mambo mawili yamenishika mkono: Mosi, tuko kwenye hekaheka za maandalizi ya ziara mikoani. Infact viongozi wengi sasa wako field. Kwa hiyo kuna mambo mengi yapo mikononi mwangu kwa sasa. Pili, hii ni Xmas, nawakatikia heri mjazwa upendo, jitihada, mafanikio na furaha. Mara baada ya mapumziko nitaendelea na mjadala. Lakini kwa sasa kwa kuwa hoja zilikuwa nyingi na naona wapo wanaotaka nianze na family bussiness wengine uhusioano wa CHADEMA na conservative(na chagizo za DrWHO kuhusu realism!). Ipi nianze nayo?
Lakini fahamuni kuwa mpaka sasa hakuna hoja ambayo CHADEMA kama CHADEMA tumeifanyia kikao cha kuijadili kati ya hoja zilizosemwa humu. Bado hoja za humu ni maoni yangu binafsi. Ikitokea siku tukaamua kutoa tamko rasmi kabisa kujibu hoja nitawajulisha.
But nakubaliana na wewe Mkandara-walatini wanasema Scriptura maneti(kama bado nakumbuka spellings) kwamba 'maandishi hubaki'. Hivyo lazima niwe makini kiasi katika kuchangia hoja.
Na hii ni tofauti yangu kati Mtalii, DrWho na wengine. Mnaouwezo wa kuandika chochote,vyovyote,popote wakati wowote.
Mimi Mwenyekiti wangu yuko hapa(in a light touch) na wapinzani wangu wamejaa tele....Teh teh teh teh...
Once again, Happy holidays!
JJ