Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Absolutely umegonga kwenye kichwa. Unafahamu kukitokea ajali Insurnce companies wanalipa fedha nyingi sana, ndio maana kama hujamaliza kulipa Fees kwenye kusoma wanakuandikia barua ili wawe updated.

Vile vile madai ya uongo kukitokea ajali.
 
Mtalii/Chinga.
Thanks. You have kept me in good company. I like Mwanasiasa and I like Mbowe.
 
Mwanasiasa.
Chinga aliweka namba za chuo na tulipiga na kuambiwa hayupo na hakuna aliyekuja na jibu. leo chuo kimefungwa unadai alikuwepo chuoni.


Hivi ni university gani hiyo utakayopiga simu tu na kumuulizia mwanafunzi wakujibu kama yupo school au hayupo....???? Hiyo information ya kama mwanafunzi yupo darasani au hayupo ni confidential labda wewe uwe polisi au afisa uhamiaji tena ujitambulishe vizuri ikiwezekana kimaandishi ndio utapewa hayo majibu. Pia, kuna uwezekano mkubwa hawatakupa specific lectures alizokosa kuhudhuria na alizohudhuria sana sana watakuambia amehudhuria labda 70% ya vipindi/lectures XX anazotakiwa kuhudhuria kwa semester au mwaka.

Uwezekano wa yeye kuondoka Hull Univ bila kuaga kwa wiki 2 au hata zaidi upo; tena ni mkubwa sana, wanafunzi maelfu wanafanya hivyo kwa sababu zao binafsi ikiwa ni pamoja na kuingia mitaani kufanya kazi.

Kuna hoja nyingi za msingi ambazo Chadema wanaweza kutujibu mfano hili suala la ukabila na family business, tusubiri JJ atakuja hapa kujibu kama ambavyo amejibu suala la chopa.

Ni kwa faida yetu wote kuwa vyama vya upinzani kama Chadema vinaeleweka vyema kwa wananchi kama mimi na wengine. Hii nafasi hapa ni sawa na 1 to 1 ambayo si CCM wala CUF wala yeyote yule kutoka chama chochote aliyepata kuja hapa kutuelezea kwa undani wasiwasi wetu kwa vyama vyao kama wanavyofanya Chadema.

Kama hatuna hoja ni vizuri kukaa kimya na kusoma tu hoja za wengine. Si vema kuendekeza ubishi wa kitoto.

Nawaombeni turudi kwenye hoja.
 
Mtalii aka chinga: mimi sina jazba, na wala sio sehemu ya personality yangu hiyo. Samahani kama jibu langu limeonekana la kijazba. Sioni umuhimu wa kukutafutia wanaforum wote waliojibu issue ya Mbowe kuwepo Hull maana sioni added value yake. Facts speak for themselves.

Halafu hii kwamba nimehama vyama kadhaa vya upinzani ni malicious and stupid propaganda. Nimewahi kuwa CCM na sasa CHADEMA. Sasa kama wewe unanijua kuliko ninavyojijua mwenyewe hongera sana na ubarikiwe kwa hiyo karama!
 
Mwanasiasa.

Mimi ukinifananisha na Chinga inakuwa mikoba zaidi. lakini kunifananisha na Mtoro wa shule hapo pagumu sikubali.

kingine kwenye kamati kuu ya Chadema itakayokaa kuja kujibu hoja humu naomba mniweke sawa. Chairman anasoma masomo gani kule Hull? kwani nimefuatilia na kuona Hull ni Mabingwa wa masomo ya Library,French na Kijerumani au atakuwa anawasiliana na Zitto KIJERUMANI?

kuna kazi Chadema zaidi Cuf!.
 

Mbowe aenda Mwanza kutoa shukrani


Na Mwandishi Wetu, Mwanza

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Freeman Mbowe, leo anaanza ziara ya siku moja mkoani hapa, kwa ajili ya kutoa shukrani kwa wananchi waliokipigia kura chama cheke katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na mratibu wa ziara hiyo, Lucy Owenya, ambaye pia ni mbunge wa viti maalum wa chama hicho, katika ziara hiyo Mbowe atatumia helikopta ambapo atahutubia mikutano ya hadhara katika wilaya nne kwa siku moja.

Lucy alisema wilaya ambazo zimepangwa kutembelewa na Mbowe ni Ukerewe, Misungwi, Sengerema, Nyamagana na
Ilemela.

“Katika ziara yake, licha ya kupita kuwashukuru wananchi kwa kukipa chama kura katika uchaguzi, pia atakuwa na ujumbe wa kuwaelezea wananchi ujulikanao
kama ‘Chadema Tumaini Jipya la Watanzania’ utakaotoa jibu la hatma ya nchi na matatizo ya sasa,” alisema
Owenya.

Akifafanua zaidi kuhusiana na tumaini jipya, alisema chama chake kinakuja na mpango mpya kwa Watanzania ambao utatoa ufumbuzi wa masuala ya kiuchumi, elimu, afya na huduma nyinginezo wenye lengo mahususi kwa nchi.

Katika uchaguzi mkuu uliopita mwaka jana, Mwenyekiti huyo aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama chake, alipata kura 668,736 sawa na asilimia 5.89 na kupata
wabunge watano wa majimbo na wengine sita wa viti maalum na kuwa washindi wa tatu baada ya Chama cha Wananchi (CUF) kilichokuwa cha pili kitaifa baada ya CCM.

Mara baada ya kumaliza ziara yake mkoani Mwanza, Mbowe anatarajiwa kuanza ziara kama hiyo kesho kutwa katika Mkoa wa Kagera na baadaye katika mikoa mingine kulingana na ratiba ya chama.
 
Dr Who,

Kolo ana husiana vipi na topic hii??

FD



Unajua huyo Chinga namfananisha na KOLO TOURE

ANAJUHUDI SANA HUMU NDANI

lakini zaidi ni kuwa jana ARSENAL ILISHINDA gemu yetu na WATFORD

ukienda katika forum ya MICHEZO humu ndani ya Jambo forum utaona


samahani kwa kukuhudhi mzeee
kwani wewe TOTENHAM?
 
Mbowe si msomaji wanafunzi wote wanajiandaa na mitihani ya kumaliza term january. yeye anapuyunga mitaani.
 
M wanasiasa.
Naomba nami nimbatize bwana Mbowe jina langu. Mbowe aka Mtalii.
anatalii kunishinda hata Mwenye jina?
na msemaji ni mtoto wa mzee Ndesamburo wenye NGO?
Mngetumia pesa zenu kumsomesha Mnyika.
 
DrWho,

Mimi ni MAN kwahiyo nipo Man Utd.

Mwanasiasa, Mwenyekiti wenu inaonekana ni kipanga sana, kama exams zinaanza Jan na yeye yupo mtaani kweli shule yake ni kali sana!!

FD
 
....

Mwanasiasa, Mwenyekiti wenu inaonekana ni kipanga sana, kama exams zinaanza Jan na yeye yupo mtaani kweli shule yake ni kali sana!!

FD

Hata mimi natatizika hapo, hasa ikizingatiwa kuwa anasoma undergrad na MBA at the same time.

Sie wanafunzi wengine tunakesha na makalkulesheni, kuchapa programmming codes, kutengeneza electronic prototypes na kumalizia term papers ... mwanafunzi mwenzetu wa digrii mbili yuko hewani na helikopta Mwanzaaa!!

Aisee, yaani tunaanza kumkumbuka Chinga.
 
Hongera na kila la heri Ndugu Mnyika!!

Another feather in your cap!

Mnyika Mwenyekiti IYDU

na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika, amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Vyama vya Kidemokrasia Duniani (IYDU).

Taarifa hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Erasto Tumbo, kwenye tovuti ya chama hicho jana.

Tumbo amesema Mnyika amechaguliwa katika nafasi hiyo kwenye uchaguzi uliofanyika wakati wa mkutano wa baraza la umoja huo nchini Uingereza mwanzoni mwa mwezi Desemba, mwaka huu.

Alisema katika uchaguzi huo, Mnyika alikuwa mgombea pekee kutoka Afrika, hivyo kuwa pia mwakilishi pekee wa Afrika katika Kamati Kuu ya IYDU.

Alisema kwenye taarifa hiyo kuwa mgombea wa nafasi hiyo anapendekezwa na chama chake na kuungwa mkono na nchi nyingine zaidi ya mbili.

“Uteuzi wa jina la Mnyika kugombea nafasi hiyo uliungwa mkono na vyama vya kidemokasia Afrika pamoja na nchi kadhaa za Ulaya hususan Norway na Finland,” alisema Tumbo.

Katika uchaguzi huo, Mbunge wa Bunge la Norway anayetoka Chama cha Hoyre, Peter Gitmark, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa IYDU.

Akizungumza baada ya kurejea nchini, akitoka kwenye uchaguzi huo, Mnyika alisema uchaguzi huo ulikuwa na ushindani mkubwa.

Alisema vigezo vilivyomfanya achaguliwe ni baada ya kuzunguzia suala la ongezeko la joto, UKIMWI na kukua kwa demokrasia ya vyama vingi.

Mkutano huo wa baraza la IYDU ulianza Novemba 29 na kumalizika Desemba 2006, na ulihudhuriwa na wajumbe 250, wengi wakiwa ni viongozi wa vijana na wabunge vijana kutoka nchi mbalimbali.

CHADEMA inaendelea kupata nafasi za juu kwenye umoja huo baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe, alipochaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia Afrika (DUA).

Mbunge wa chama hicho, Zitto Kabwe wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, katikati ya mwaka huu, aliteuliwa na Rais wa Ujerumani Horst Kohler kuwa miongoni mwa timu ya vijana wanaomshauri rais huyo kuhusu masuala ya siasa, uchumi na ushirikiano wa kimataifa.

SOURCE: Tanzania Daima 28 Desemba 2006
 
Hongera sana JJ, ni matumaini yangu kuwa utajifunza mengi kutoka IYDU.

Natumai hii itakupa nafasi ya kumalizia malengo yako binafsi hasa katika nyanja ya elimu.

Kila la KHERI and WEll DONE.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom