Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Ninachokiona mimi si tatizo kwa Mbowe wala Chifupa. Tatizo liko kwenye mifumo ya vyama vyote viwili vilivyowapa nafasi zisizowafaa. CHADEMA na CCM. vyama vyote ni Bomu na havijali maslahi ya watanzania zaidi ya masifa yasiyo na mpango na kughalimu gharama kubwa katika kuzitafuta sifa na kijilimbikizia ujinga.

Mbowe amefanya uzembe wa hali ya juu kuingia gharama kubwa bila kuwa na mikakati ya kweli ya kumkomboa mtanzania kwa kuwasaidia wagombea wake wa ubunge katika kushinda katika majimbo, kabla ya yeye kupenda kupepea na helikopta ili kujipatia umaarufu akijua wazi kwamba hawezi kufika Ikulu kwa njia hiyo.

Chifupa, bado anahitaji kujipanga upya katika mambo yake na siyo kutumia pesa za watu wanaomtumia ili kujipatia umaarufu wa kutoa misaada kwa watoto yatima, nk wakati tunajua wazi kwamba misaada hiyo haiendi katika midomo ya yatima hao.

Pia kununua card za bahati nasibu ya Mwalimu Nyerere kwa ajili ya vijana wote wa UVT-CCM, kwani angekuwa na nia ya kweli ya kuwaendeleza vijana hao angewaanzishia mbinu mbadala za kujikwamua kiuchumi na kuacha kucheza gwaride la ushabiki wakisubiri posho za mikutano ya CCM na rushwa za ndani ya chama chao.
 
J J Mnyika,
Kwanza yabidi nikupe hongera Chadema kwa kuweza kutupa maelezo ya ndani. hasa sisi tulioko nje ya uanachama sii rahisi kupewa Uwazi wa namna hiyo.

Mimi kidogo hesabu zimenipiga chenga hapa. Umesema Helikopta hukodishwa kwa masaa inayokuwa hewani na madai yako ni kuwa Helikopta ile iletumia masaa 2 kwa siku... hapa kidogo nashindwa kuelewa uwezo wa kufanya mikutano 8 na flying time ni masaa 2 tu. Hii inanipa picha kama kila Helikopta ikiruka hutumia dakika 20...na sidhani kama Freeman na wajumbe walilala huko vijijini kwa hiyo kuna safari ya kurudi mjini.

Nikijumlisha hapa napata masaa zaidi ya hayo. Kisha kila safari inavyozidi kuzama Uswekeni ina maana Dar au Arusha kunakuwa mbali zaidi...Hapa baada ya mikutano ya Mkoa nadhani mlikuwa mkirudi mahala kujifunga upya ama kuchukua pumzi mpya.
Well, itabidi nikuamini kwani nyie ndio mko ndani mmepiga mahesabu na kuona unafuu wakutumia hiyo chopa..lakini!

Mafanikio:-
Kidogo ndugu yangu mimi bado nasimama kweli reality!..sidhani kama Chopa ilikuwa na mafanikio ktk KURA. Hii ndio dhumuni la hiyo Chopa haswaaa!

Achana na CCM - hao CUF hawakutumia nguvu yeyote na wameweza kushika nafasi ya PILI. huoni kama Watanzania swala la Chopa sii muhimu kwao?.. Ila wabunge wagombea.. kama ulivyosema Wadanganyika sii wote washamba wapo wanaojua kupeta kuondoa hilo vumbi la Chopa. helikopta kwa wengi ni sawa na mwanamke anayejipodoa na hizo make-up, hapa tunaweza kukesha ktk kusifia uzuri wa mwanamke huyu. It all depends!

Je, ni kitu gani kimeweza kuwasimamisha CUF vizuri zaidi yenu hali Chadema was the name kabla ya Chopa... baada ya Chopa tu watu wengi walishukwa na imani kuwa Freeman ni mwenzao - Mlalahoi mwenye fedha za usalama wa maisha.
 
JJ,
kazi nzuri sana, umejibu hoja kwa ufasaha kabisa.

Mkandara,
Inawezekana kabisa walikuwa wanatumia masaa mawili mpaka matatu kwa siku hewani. Tena kwa mikoa kama Dar-Es-Salaam, ni swala la kuruka na kutua. Nakumbuka, Wakati mmoja tulikuwa viwanja vya urafiki Manzese tukisubiri Mkutano wa Freeman na jj, ambao walikuwa mbagala, Mtemelwa alikuwa akiwasiliana na watu wa huko, tulipotaarifiwa kwamba wamenyanyuka mbagala iliwagharimu pungufu ya dakika tano tu kuonekana kwenye anga za Manzese!

Naamini Helkopta, Hotuba murua za Freeman na hoja nzito wakati wa kampeni ziliikijenga sana CHADEMA. CHADEMA ndio chama kilichokuwa zaidi ya CUF kwenye uchaguzi mkuu. Mathalani CUF ilipoteza majimbo yote bara,CHADEMA ilipoteza mawili(Hai na Kigoma Mjini) na kuongeza matatu(Kighoma kaskazini,Mpanda Kati na Tarime). Walikuwa wakipata ruzku ya milioni tano kwa mwezi kwa sasa wanapkaribia milioni sitini. Kwa ujumla chama kina wabunge 11katika bunge la sasa tuki linganisha na wabunge watano wa kipindi kilichopita.

CHADEMA imekuwa, na sasa inatawala kwenye mijadala ya kisiasa.

Mvuto na umaarufu wa CHADEMA umeongezeka sana.Na isitoshe matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2005 ni ya kupikwa!!
 
Mkandara usisahau kuwa ni kura za Pemba zilizoifanya CUF iwe ya pili. Kusema kweli sisi CHADEMA hatuwezi kufua dafu kwa CUF huko Pemba na Unguja! Ila kwa bara, uuh, hao wenzetu hata kiti kimoja hawakupata!
 
Eric, Mwanasiasa,

Shukran kwa maelezo yenu. Sasa picha ipo wazi. Hao wabunge 11 wote ni wa kuchaguliwa na wananchi ama mnajumlisha na wale walioteuliwa!.

Je, kati ya hao wabunge ni wanagapi Freeman alitembelea majimbo yao na hiyo Chopa.

Samahani najaribu bado kuangalia uhalali wenu wa hii Chopa kuwa ilikkuwa muhimu.
 
Wapendwa,

Naona bado mjadala wa chopper unaendelea, mpaka tuamua kuuweka pembeni mjadala huu kwa muda ndio nitaingia mjadala wa family business na mingine.


DrWHO,

Nimeshindwa kukuelewa. Soma post yangu vizuri. Hakuna sehemu yoyote niliyosema mimi nafanya consultancy CHADEMA na kulipwa dola mia kwa siku. Consultancy ni kazi zangu za binafsi, si za CHADEMA wala si kwa CHADEMA. Soma vizuri tafadhali

Mvuvi,

Nashukuru kwa mchango wako, but I am afraid if a respond to every issues you have raised we will derail the trend of the current discussion. Ila suala moja. Si kweli kwamba Mbowe aliingia gharama kubwa kuwa na mikakati ya wazi ya kuwakomboa watanzania!. Kwanza tuondoe dhana ya Mbowe kwa kuwa unakuwa huvitendei haki vikao vya chama. Uamuzi wa kutumia helikopta ulifanywa na vikao vya chama kuanzia sekretariati, kamati kuu, baraza kuu na mkutano mkuu ambao naamini wengi wenu mliona kupitia kipindi maalum tulichokirusha kwenye TV.

Kwa hiyo CHADEMA iliamua kutumia milioni 200 kwenye helikopta, ambayo haikuwa inatumiwa na mgombea urais peke yake. Mathalani, Badala ya kupewa laki 4 za kunisadia kwenye kampeni kitendo cha kuelekeza pesa hizo kwenye chopper kilisaidia kuvuta kundi kubwa la watu Mbowe alipokuja Ubungo lakini pia image ya chama kwa ujumla ilikua. Lakini kwa upande mwingine Chadema iliamua milioni 500 zitumike katika mikakati mingine wakati wa kampeni ambayo kwa kiasi kikubwa ilielekezwa wa wabunge.

Ukweli ni kuwa chama kilifanya realistic evaluation kabla na wakati wa kampeni na kugundua majimbo ambayo tulikuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda, haya tuliyaita red na yalipewa raslimali zaidi ikiwemo mabango kwa wagombea na hata sehemu kiasi ya pesa. Na targeting yetu ililipa kwa kuwa haya ni majimbo yanayochangia zaidi hata katika ruzuku ya chama kwa sasa.

Mkandara.

Umerudia tena swali lako la siku zote| Kwa nini CHADEMA haikuchukua dola pamoja na heka heka zote hizo?Kwanini CHADEMA ilishika nafasi ya pili nyuma ya CUF? Hili ni swali pana, unaniruhusu nitulie nikufanyie uchambuzi kabla kujibu suala la family business?

Lakini nikueleze kwa ufupi tu]

Mosi, nakubaliana na Ongara kwamba matokeo ya 2005 hayakuwasilisha hali halisi ya ridhaa ya watanzania. Na mimi ni mhanga wa hili katika jimbo la Ubungo. Soma tamko la CHADEMA kuhusu uchaguzi(www.chadema.net) litakupa picha ya nini kilitokea. Ukitaka kujua kama hawa jamaa hawakushinda kwa kishindo kama ilivyosemwa angalia mshangao wa kikwete kuhusu matokeo lakini angalia pia jitihada wanazofanya kuua upinzani. Hiki kama wangekuwa ni chaguo la wananchi kwa asilimia zaidi ya 80 wangehangaika kiasi hiki kuvunja upinzani badala ya kutimiza ahadi zao kwa wananchi?

Pili, CHADEMA ilipata mafanikio katika kura. Na si kwa sababu ya chopper tu, ni chopper na mikakati mbalimbal. Na mafanikio hayo yamekuwa kwenye kura, ruzuku etc kama ifuatavyo..

CHADEMA imezidi kupanda Kisiasa: CHADEMA kiliendesha kampeni zenye ufanisi zaidi ukilinganisha na miaka mingine. Ongezeko la wagombea wazuri, ubunifu wa kutumia helikopta katika kampeni na utamaduni wa kuendesha siasa safi zinajozikita katika ajenda/hoja vilipandisha chama kisiasa. CHADEMA ilijitofautisha kwa kiasi kikubwa na vyama vingine kisera kwa kutilia mkazo sera ya mabadiliko ya mfumo wa utawala ikiwemo uundaji wa serikali ya majimbo. Chama kimepata mtaji mzuri wa kisiasa kutokana na uchaguzi mkuu 2005 mathalani kufahamika kote nchini, wapenzi na wanachama wapya, wagombea nk.

Pamoja na kushindwa sanjari na kupata matokeo ambayo hayakulingana na jitihada na kukubalika kwa chama, CHADEMA imekua zaidi kisiasa katika uchaguzi mkuu 2005. Chama kimeongeza idadi ya wabunge wa kuchaguliwa kutoka 4 mpaka 5 na kuongeza idadi ya kura za ujumla za ubunge kutoka asilimia 4.23 mpaka 8.2. Hili ni ngezeko la takribani asilimia 100.

Hii imepelekea chama kuwa na wabunge wa viti maalum 6 kutoka 1 na kufanya jumla ya wabunge wa chama kuwa 11 kutoka 5 ambalo ni sawa na ongezeko la asilimia 110. Ruzuku ya chama imeongezeka kutoka milioni 5.6 kwa mwezi mpaka milioni 35.5 na hivyo kutoa nguvu nyingine ya chama kuweza kujijenga kisiasa. CHADEMA ilisimamisha mgombea Urais kwa mara ya kwanza na kushika nafasi ya tatu. Jumla ya madiwani imeongezeka kutoka 64 mwaka 2000 mpaka 99 katika uchaguzi 2005.

Kwa upande wa Zanzibar chama kimeweza kusimamisha wagombea wengi zaidi kuliko chaguzi zingine na kushika nafasi ya tatu katika kura za ubunge katika majimbo mengi na kujitambulisha kama nguvu ya tatu katika siasa za visiwani. Matokeo haya mazuri yamepatikana kwa raslimali kidogo ambazo chama na wagombea wake walikuwa nazo katika uchaguzi. Kwa ujumla kampeni za CHADEMA zilitumia shilingi 753,786,505. Katika fedha hizi shilingi 223, 030,726 zilikuwa gharama za helikopta.

Hii ni ukiondoa gharama ambazo zilitumiwa na wagombea binafsi pamoja na wapenzi wa chama moja kwa moja katika maeneo yao

Tatu, umesema kwamba CUF hawakutumia nguvu yoyote lakini wameshika nafasi ya pili. Mimi si msemaji wa CUF, naomba vijana wa CUF waibuke hapa na kutoa takwimu ni pesa ngapi chama chao kilitumia. Nijuavyo mimi CHADEMA kilikuwa chama cha tatu kwa matumizi ya pesa, CCM kwanza, CUF pili. CUF ilitumia pesa nyingi zaidi sana ya CHADEMA. Ndio maana nasisitiza, CHADEMA imesema imetumia pesa ngapi, na vyama vingine viweke wazi basi matumizi yao. Nisingependa ninukuu kutoka habari za ndani kwako. Nataka itoke midomoni mwao.

Nne, umesema kitu gani kimeishusha CHADEMA wakati it was a name kabla ya chopper. Hii nayo sikubaliani nawe,hata ripoti za waangalizi wa uchaguzi zinataja chopper kama baadhi ya mambo makuu yaliyompandisha chati kiasi kikubwa Mbowe na CHADEMA.

Tano, linapokuja suala la kuzidiwa idadi wa wabunge katika bunge la muungano hapa kichofanya CHADEMA izidiwe ni Pemba factor. Otherwise CHADEMA ndio ingekuwa official opposition!

Sita, your basic question remains, if all that kwa nini CHADEMA imeshika nafasi ya tatu? Soma tamko la CHADEMA utapata baadhi ya majibu http://www.chadema.net/uchaguzi/ripoti1.php Tatizo ni kuwa watanzania walioipenda CHADEMA waliipenda weeee mpaka wakawa na matarajio yaliyozidi mipaka.

Mimi nikupe mtazamo wangu

1. Historia, tazama 1995, 2000 vyama vipi vilikuwa vya kwanza,pili, tatu na nne? Ukweli ni kwamba kabla ya 2005 CHADEMA haikuwa na nguvu ilizokuwa nazo 2005. Hii inamaanisha ni nini, CUF ilisha invest kwenye uchaguzi wa 2005 kabla ya mwaka huo hususani mara baada ya uchaguzi 2000. Hii iliwafanya wawe na mtandao maeneo mengi na kuokoteza kura country wide,hivyo pamoja na kukosa mbunge hata mmoja kwa nadharia ya haba na haba ni wazi kwamba wangeweza kuizidi kura CHADEMA ambayo haikuwa na wagombea kila mahali katika nchi hii. Na ushahidi mwingine, wa mtaji huo ni matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2004. Infact investment na mtadao wa CUF haulingani kabisa na matokeo waliyoyapata. Hivyo historia hii imeshaanza kubadilika watch 2009 na 2010.

2. hii inazaa sababu ya pili, mapungufu ya CHADEMA katika baadhi ya maeneo. Ukweli ni kuwa the new CHADEMA ni product ya kazi iliyaonzwa kufanywa na ziara za wabunge 2003 na kuzaa mabadiliko ya uongozi yaliyowaingiza wakina Freeman kwenye uongozi mwaka 2004 tu. Wengine tumeingia CHADEMA mwaka 2005. Kwa hiyo tulikuwa na less than a year ya kujiandaa. Kwa kipindi hicho kufupi tu cha maandalizi tumefanikiwa kupanda mpaka nafasi ya tatu na kufanikiwa kiasi ambacho nimedokeza hapo juu. Sasa tunamiaka mitano ya kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi ujao tukiwa na raslimali nyingi zaidi unategemea matokeo yatakuwaje? Unategemea CHADEMA itashika tena namba tatu?

3. Ukweli unabaki pale kuwa CHADEMA ndio chama pekee kikubwa cha upinzani kilichokuwa. Kwa hiyo ni chama kinachokuwa wakati upinzani kwa ujumla wake unashuka. Changamoto ni kuziba hii vacuum na kubaki kuwa na strong opposition kwa maslahi ya taifa na hatimaye kuweka madarakani alternative government.

4. Ni chama kipi cha upinzani kinachoonyesha matumaini ya kuwa alternative party Tanzania? Mashambulizi ya dola sasa yanaelekezwa wapi kwa upande wa bara?

Hii ni changamoto kwako na kwangu..

JJ

Ps. Mnaniruhusu sasa niingie kwenye hoja ya family business?stay tuned!
 
Mwanasiasa.

Chadema mwenzako anasema matokeo ni ya kupikwa 2005 jee tumuamini nani?

kama Cuf hawana kiti bara haina maana kuwa hawakubaliki.
kwa mantiki yako ya ki chadema unataka kutuambiwa kuwa TLP ni bora zaidi ya Cuf kisa wana Mbunge na Cuf hawana? Nani asiyejua kuwa kuna njama za kuiua cuf? sikiliza hata mahojiano ya mrema na redio butiama anashangaa kuona yeye anapata mbunge. na cuf kukosa.

Mwanasiasa na wana chadema msijidanganye kuwa chadema kinakubalika kuliko cuf, cuf ni chama cha wanyonge kinakubalika kila kona, na vijana wapo tayari kuandamana, kupingwa virungu, kujitolea kukodisha malori na kwenda mikutanoni. Chadema hakuna vijana wa kujitolea kwa hali, kama kuna watu wanajua kuna kitu kidogo. Cuf ni natural chama tena cha wananchi wote, nenda Mwanza kaone shughuli ya cuf, nenda Dodoma, Kondoa,lindi , mtwara hadi Bukoba.ni wafuasi wa cuf waliomzomea kikwete kwenye kampeni zake.

lakini chadema ni Hai. MACHAME, KARATU,MARANGU, MOSHI MJINI.
Mwanasiasa ukiambiwa uandamane kudai haki yako unaogopa FFU.tizama vijana wa cuf Temeke. mtoni, mbagara.
Mwanasiasa acha bwana hiyo ni family business tu.
 
Mkandara..

Soma tena majibu niliyoyatoa. Focus ya chopper na mikakati mingine ya chama ilikuwa majimbo ambayo tulikuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda ingawa chama kilipeleka pia majimbo mengine. Kwa hiyo hao wabunge wote walioshinda walisadiwa na chama ikiwemo ziara za chopa. Hiyo ndio maana ya targeting, tungesambaza nguvu tulizonazo ingekuwa hadithi ya mtaka yote kwa pupa. Hebu itathmini CHADEMA ilivyokuwa 200 mpaka 2004 kabla ya kuchangia kwa kina. Ila hii sasa ni historia, itazame CHADEMA inaelekea wapi? Ikoje, ina mikakati gani? je katika mwaka mmoja imeitekeleza kwa kiasi gani unaweza ku predict itakuwa wapi 2009, 2010 na hatimaye 2015.

Mswahili,

U r not fair ndugu. tembelea www.chadema.net uangalie ni majimbo yapi CHADEMA imefanya vizuri(kwa maneno mengine ni wapi kulikuwa hekaheka za uchaguzi( utagundua kuwa yamesambaa sehemu kubwa ya nchi si kilimanjaro pekee. Infact kilimanjaro tumepoteza some of our traditional strong holds!. Hili nitalichambua kwa kina wakati najadili je CHADEMA ni chama cha kichaga na kikristu?

inaelekea unapenda sana siasa za fujo na vurugu. Huo kwa kweli si utamaduni wa CHADEMA. Binafsi siamini katika Machavellianism!. Lakini ironically, katika uchaguzi uliopita ni katika eneo la CHADEMA Tarime ndipo damu ilimwagika katika uchaguz(Mungu awalaze mahali pema vijana wa CHADEMA waliokuwa wakitetea mabadiliko(. Sijui kama unajua yaliyokuwa yakitokea Karatu, Songea mjini na kwingineko. Stand for the truth ndugu yangu. Pamoja na utamaduni huu wa CHADEMA haiondoi ukweli kwamba kuna wakati inabidi kuichukua haki badala ya kuiomba.

Nakubaliana na wewe suala moja wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa 2004 maeneo mengi waliona CUF ndio ambayo ingeweza kuitetemesha CCM bara. By then CUf ndio ilikuwa ikionekana yenye nguvu zaidi bara. Hali ni tofauti kwa sasa.

But i do not underestimate nguvu na network ya CUF. infact niliwahi kusema hapa mapema mwaka huu CHADEMA na CUF kila chama kiendelee kujijenga na ikifika mapema 2008 vyama hivi vianze kuunda strategic alliance. (kama vyote vitakuwa vimejijenga ipasavyo mwaka 2007(. Kama kati ya vyama hivi kuna chochote bado kitakuwa kina election lag ya 2005 na kinaendelea kulala basi kimoja kiende mbele peke yake. Na hicho ndicho kitakachoungwa mkono na wapenda mageuzi wote bila kujali dini wala itikadi!

Nisingependa kujadili masuala ya ndani ya CUF, naamini wananchama wa cUF watakuja hapa na kuyajadili wa maslahi ya taifa.

Jamani eeeeh, niruhusuni nihamie kwenye hoja ya family bussiness.

JJ
 
Mnyika.

Usinitajie Karatu Huko Si Kaskazini?
Uchaguzi Wa Songea Niliufuatilia Sana Cuf Walikuwa Na Chiumbo Na Nyinyi Mlikuwa Na Mbogoro.

Sijasema Siasa Za Vurugu Nilichosema Chadema Ni Chama Cha Biashara Tu. Hakuna Mtu Anaweza Kutoa Chake Isipokuwa Akina Ndesamburo, Mtei Kwa Masharti Ya Watoto Wao Kupewa Vyeo.

Kwanini Mnyika Ulimkimbia Chinga?
 
mswahili: polepole usipayuke sana, CHADEMA inafanya biashara gani? Hebu nipe shule kidogo hapa tafadhali!
 
Mswahili

1. Kwa hiyo jimbo la karatu kwa kuwa liko kaskazini hata likifiwa na vitendo ambavyo vimetokea kwenye stronghold za cuf halina haki ya kutajwa kama mfano?

2. Over 80 percent ya maeneo uliyotaja ni Kilimanjaro. Tena mahali pengine umeparudia mara mbili mfano hai na machame ni sehemu moja. So between lines u wanted to send a message kuwa CHADEMA kilikuwa chama chenye nguvu Kilimanjaro pekee. Nimekwambia hii si kweli. Rejea matokeo ya uchaguzi na uangalie chama kimefanya vizuri wapi na wapi.

3. Soma vizuri post yako mwenyewe, you tended to suggest kwamba kipimo cha mafanikio ya chama cha siasa na uwezo wa kufanya vurugu na maandamano. It tell you, haya ni muhimu kwa chama cha siasa lakini yapo ya muhumu zaidi ya hayo. This is the culture we want to build in CHADEMA.

4. Sasa huyo Chiumbo unaweza kufananisha na heka heka za Mbogoro.

5. Umesema CHADEMA ni chama cha biashara, hakuna anayeweza kutoa chake isipokuwa ndesamburo na mtei etc. Nashukuru kwa kuongeza malicious allegation. Ni ruhusuni basi niache hii hoja ya chopper niingie suala la family business nikujibu haya yote basiiiiiiiiiiii!

6. Kwa nini nilimkimbia Chinga. Nioneshe kwenye post zangu wapi nilisema namkimbia chinga. Mimi naamini Chinga anasoma majibu yangu. Kama ningeteleza japo kwa sekunde angerudi hata kama ni kwa jina lingine. Chinga amesema ameondoka, lakini maswali yake yapo hapa bado. Na naamini chinga hakuandika kwa ajili yake binafsi, angefanya hivyo angeniandikia barua binafsi. Ameandika ulingo wa wazi ili umma usome. Nami nitamjibu mstari kwa mstari umma usome. Halafu umma utaamua kati ya uwongo na ukweli.

Niliwahi kumuonya Chinga mapema sana alipoanza kwamba aandike ukweli kwa kuwa kwa utamaduni wa forum hii watu wanaoandika porojo huwa huishia kudharaulika pale ukweli unapotamalaki.

Ndugu yangu Chinga, kama umesafiri. Ikirejea naomba uje na jina lako halisi ujibu hoja zangu nilizozielekeza kwako. Umelinuliza maswali, nakujibu sasa!
 
ufafanuzi,

Ninaposema jina lako halisi namaanisha urudi na jina la CHINGA na si vinginevyo.

JJ
 
JJ,
Ebu nimegee kidogo, endapo ndoto ya CHADEMA miaka ijayo inapata ridhaa ya wananchi kuingia Ikulu, CHADEMA ITAUNDA SERIKALI YA NAMNA GANI, YA MSETO AU?
 
JJ,
Hongera kijana. Baada ya majibu yako nadhani wanaondeleza masuala ya chopa basi ni shauri ya ubishi au basi ni kwa kuwa wakubwa huwa hawakubali kuwa wamekosea. Umewashushua kwelikweli na limewashuka shuuu!

Nilishangaa sana kuona eti chopa imekuwa suala bila hata ya kufanya tathimini. Mtu unaweza kuamua kusafiri kwenda mwanza kwa kutumia treni ukifikiria unapanda usafiri wa nauli nafuu lakini ukajikuta umetumia kiasi kilekile au zaidi ya aliyetumia basi. Kwa wenzetu hawa suala eti ni kwa nini utumie basi badala ya treni!!!!!

Hilo la CUF kushika namba mbili bila shaka Mwanasiasa na Eric wamejibu vema ni kura za Pemba na Temeke. Pia tusisahau Mbowe alivyo mzalendo alikuwa akiwapigia debe wagombea wa CUF pale walipokuwa wanakubalika mfano kule Geita kwa Peter Masabo. Sasa wewe Mswahili ebu tuambie ni wapi CUF ilisema CHADEMA inakubalika basi tuwaunge mkono?

Kwako JJ na wana CHADEMA tunajua nyie siyo malaika, na naamini mkiingia madarakani mkakosa upinzani kama walivyo CCM mtafanya kama wao tu.

Watu kama akina Kaburu lazima watakuwemo chamani iwe kwa kudandia mafanikio au kwa kuyatafuta. Msife moyo tunahitaji mpate wabunge wa kutosha tuanzie hapo; mosi, kutunga katiba mpya, pili kutumia bunge letu kuwajibisha serikali na tatu kuleta demokrasia ya kweli na utawala wa sheria.
 
JJ

can u clarify about CHADEMA's alliance with Consevatives in the UK?


also can you please also clarify that your Chairman Mr Freeman is a Realist

BTW

Weka space baada kuandika paragraph
 
JJ Mnyika,
Shukran za dhati kwa ufafanuzi wako wa hilo swala la Chopa!...nadhani inaridhisha vya kutosha kuona kwamba mahesabu yalitumika... a worth investment.

sasa nadhani tuingie ktk swala la family business... hapa nakuomba uwe makini na mtazamo wa watu tulioko nje!
Nikisema hivi nina maana kuwa kila unachokiona wewe ndani sii lazima kituvutie sisi na hata wewe nikikuweka nje utaweza kuyaona mapungufu.
Mathaln, CUF inadaiwa kuwa wadini - na wao wamesema mengi kukana jambo hilo badala ya kulifanyia kazi kabla ya uchaguzi. Matokeo yake?...

2005 walikosa kura bara na leo hii bado hawaamini kuwa udini ilikuwa ni sababu kubwa isipokuwa CCM.
Je, wewe kama Chadema na mtu aliyeko nje huoni kama CUF wana mapungufu hayo?.... huna haja ya kunijibu kwani naelewa jibu. 7 out of 10 people wanaamini kuna udini ndani ya CUF. You can't beat that bob!
Pili, Hii habari ya kujikita kaskazini - Kilimanjaro as a strong hold!..

Hii nadhani ni picha moja mbaya sana kwa sababu zilezile za CUF kujikita Pemba na Zanzibar zaidi...
Yes, hizi ni strong holds zenu lakini kumbukeni siasa za nchi za magharibi kujikita ktk hizi strong holds huko kwao hakuna Ukabila wala Udini ila PURE POLITICS - Afrika ni mazingira tofauti kabisa. Mbinu kati yetu na Ulaya lazima ziwe tofauti na sio kuchukua ya Ulaya kuyaleta Afrika kwa tafsiri ile ile inayotumika Ulaya. Maoni yangu mnapanda maple tree jangwani Dodoma bob!

Je, kuna kati yetu anaye afiki CUF kutumia pemba na Zanzibar kama strong hold zake bila kuzingatia kuwa Pemba na Zanzibar kuna waislaam 99%?...Is it a Perception over Reality or Reality over Perception!... kazi kwenu.
 
JJ ,

I am still waiting on my above questions.I a sure they re not that difficult
 
Mnyika.

vipi kuhusu biashara za diamond wanazofanya Chadema na mabwanyenye ya conservatives?
na utuambie sera za kibaguzi alizotoa Chinga amedai Cameron hana mpango na human rights vipi awe mshirika wenu?
 
Mswahili.

hao Chadema hawawezi kujibu hadi kamati kuu ikae, na wanachagua sehemu za kujibu
.
Mnyika alidanganya kuwa mwanadishi ALI Sonda alikosea kusema Mbowe yuko Moshi tulitegemea gazeti liandike habari ya kusahihisha story ile, hadi leo hakuna kitu, kusoma mchezo? mbowe kashindwa kusoma utotoni atasoma leo?

Mwanasiasa nae alileta uongo kuwa chuo chake (mbowe) kina utaratibu tofauti wa kufunga. akaja DR.Who na kutuwekea ratiba kuonesha kuwa Mbowe katoroka shule hilo halijatolewa tamko hadi leo.
naridhika na maneno ya Chinga kuwa chadema ni NGO tu hakuna kitu kingine.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom