Back to chopper!. Asichojua Chinga na wengine ni kuwa helikopta, tofauti na vyombo vingi vya usafiri gharama zake za kukodi zinahesabiwa kwa muda ambao helikopta inakuwa hewani. Helikopta ikiwa chini hailipiwi gharama za kukodi. Wanachofanya tu ni kukupa minimum flying time per day(which in most cases is 1hr) na minimum days you can hirre(which is most firms is one week). CHADEMA katika uchaguzi uliopita ilikuwa inatumia between 1 to 2 hours a day!. Si zaidi ya hapo.
Sasa tuchukue kadirio la juu- 2 hours a day, hii inafanya gharama kuwa dola 2,400 kwa siku. Mafuta ya ndege ni kati ya tsh 900 na 1200 kwa lita. Ila by experience mafuta ya masaa mawili ni takribani asilimia 10 ya gharama za kukodi kwa hiyo ni dola 240. Jumla kwa siku ni around dola 2640, tufanya 2700. Tukigeuza kwenda fedha za kibongo hii ni sawa na takribani 2,800,000 kwa kiwango changu cha kubadili fedha.
Kwa hiyo helikopta kwa siku ni shillingi hata tukimbandisha kupindukia milioni 3.
Ukifanya mikutano 8 kwa siku hii ni sawa na wastani wa kadirio la juu wa shilingi laki nne kwa mkutano mmoja. Laki nne kwa mkutano mmoja wa mgombea urais. Hii ni peanut jamani.
Mkutano uliofura watu(tazama picha kwenye
www.chadema.net) ambao wamekuja wenyewe bila kubebwa na FUSO wala mabasi wala kuletwa kulipwa posho wala kuja kwa kupewa fulana na kofia. Wanakuja kwa ridhaa yao. Hii ni kuwa very cost effective!
Naambiwa mkutano mmoja wa kikwete wa Jangwani uligharimu tsh milioni 20. Hii ni sawa na mikutano mingapi ya helikopta?
Gharama za kukodi ‘shangingi' moja kwa siku ni dola 200. Hii ni sawa na 1/6 ya kukodi helikopta!. Kikwete alikuwa na msafara wa mashangingi mangapi? (Mtaniambia aliyanunua- sawa sasa tuyahesabu katika rate ya kukodishwa!). No wonder katika maeneo walikuwa wakitumia mashangingi ya serikali. Msafara wa magari mengi unahitaji man power kiasi gani? Kama kila mmoja akilipwa posho ya kati ya 20 na 30 jumla ya gharama kwa siku ni kiasi gani?
Watafiti, tupeni majibu. Chinga,toa uchambuzi wa kifedha wa suala hili pia!
Kikwete na Shein walikuwa wavuki kwa magari pekee mkoa hadi mkoa. Walikuwa wakitumia ndege ya serikali. Eti walikuwa wanaikodi. Ndege ya serikali kukodi ni bei gani kwa safari? Inatofauti gani na helikopta? Lakini je, ndege inaweza kutua kijijini na kufanya mikutano kama nilivyosema? Nataka majibu ya kweli!
(iii) Helikopta inabeba zaidi ya kiongozi mmoja na viongozi wengine wananjia ya kuwepo
Si kweli kwamba helikopta ilimbeba Mbowe pekee. Helikopta inategemea ukubwa. Ile tuliyokodi katika uchaguzi 2005 ilikuwa na capacity ya kubeba abiria 3 na rubani. Kwa hiyo kupanga ni kuchagua, unaamua tu kuchagua ni viongozi wangapi wapande. Kwa hiyo alikuwa akipanda Mbowe, mratibu wa ziara ya helikopta ambaye humsaidia pia pilot kutambua maeneo na nafasi ya kiongozi mmoja. Hapa ilitegemea mahali. Yapo maeneo ambayo alipanda mgombea mwenza, yapo maeneo ambayo mgombea wa eneo husika wa ubunge alipanda na yapo maeneo ambayo kiongozi wa chama wa eneo husika alipanda. Kwa hiyo ilifanyika kutokana na situation. Binafsi nilipanda helikopta ilipokuja Ubungo- tulitua Kimara, Mbezi, Mabibo, Urafiki etc. Nilipanda kama mgombea ubunge. Kwa hiyo wagombea wanaosema helikopta ni ya Mbowe pekee ni wazushi. Tatizo ni kuwa ilikuwa ukitaka kupanda helikopta lazima uache jimbo lako uende kuipandia katika jimbo ambalo mkutano wa mwisho unafanyika kabla ya kufika kwako. Kwa hiyo wapo waliamua kubaki jimboni kwao waisubiri ije wampokee mgombea urais. It was a matter of choice. But what on hell is kupanda helikopta mpaka watu wagombanie? Kiongozi wa chama wa eneo husika anapaswa kuwa uwanjani akimsubiri mgombea wake wa urais afike ampokee, hizo ndizo itifaki. Zilitekelezwa katika maeneo yaliyofikika. So inawezekana viongozi kuwako katika maeneo mengi, it's a matter of choice hususani katika maeneo ambayo magari yanafika!.
(iv) Pesa zinaelekezwa pia katika matumizi mengine, kupanga ni kuchagua
Pesa zilingepelekwa katika maeneo mengine. I tell you today. Hizo milioni 200 zilizopelekwa katika helikopta zisingeleta impact kama ambayo imeletwa na helikopta. Kupanga ni kuchagua. Besides, kama ni kupelekwa maeneo mengine tsh 500 zilipelekwa katika maeneo mengine mabango, vipeperushi, vyombo vya habari, kusaidia wagombea katika red seats the list is long!. Nieleze ni mambo gani hayo mengine ambayo hayakupewa enough attention ambayo yangezidi hizo faida nilizofafanua hapo juu za helikopta?
(v) Helikopta ni suluba, helikopta ni kazi
Kwa yoyote aliyewahi kupanda helikopta ya polisi ambayo inashabihiana na ile iliyotumiwa na CHADEMA anajua kuwa kupanda helikopta ni kuweka roho rehani kama sio hewani. Helikopta inaleta suluba ya kuongeza idadi ya mikutano, binafsi nampa pole Freeman kwa kuhutubia mikutano mingi namna hiyo kwa siku. Huyu jamaa angekuwa kimeo angeanguka siku nyingi sana! Lakini the guy ame-survive all over. Sijasikia ameanguka jukwaani. Helikopta ni chombo cha kazi. Helikopta tunayotumia haina AC kama mashangingi, haina viti vinavyofanana na masofa kama mashangingi. Haina raha kama ndege ya serikali wala haina anasa kama ndege ya rais. Hakuna hostosess na juices mule. Kuna harufu ya moshi na vumbi la upepo mkali unaposhuka. Ni symbol ya mapambano na harakati!. Ni symbol ya vita dhidi ya mfumo mbovu wa utawala unaopenda anasa!
(vi) Tanzania imefikia ngazi ya kutumia helikopta
Wait a minute! Huku ni kujidharau. Wakenya jirani zetu hapo wanatumia helikopta mpaka kukagua mashamba. Ile helikopta tuliyokodi pamoja na kurudi kufanyiwa mapendekezo ilitumiwa pia na watu wa mashindano ya magari. Ni helikopta ilitumika kuhamasisha wananchi kwenye vuguvugu la chungwa(ODM) kuhusu katiba Kenya. Lazima tuwe na viongozi wenye kuona mbali na kujua nini tunastahili kwa raslimali tulizonazo!. Hatuwezi kuwa na chama kinachoona jembe la mkono ndio halali yetu tukipanda kidogo eti tutumie plau na mikokoteni ya kukokotwa na ng'ombe. Napenda utamaduni wetu...