Mbowe: Polisi tukutane Mahakamani ila siwapi Ushahidi

Mbowe: Polisi tukutane Mahakamani ila siwapi Ushahidi

CDM mtapata taabu sana! Ni kipi hao Polisi wamefanya kinachoweza kutufanya tuamini kwenye deadlines wanazotoa!? Kuna uharaka gani wa kupata huo ushahidi kutoka kwa Mbowe? Kama kuna uharaka huo basi wamwombe JK aharakishe kuundwa kwa tume huru, au aamrishe CDM watoe huo ushahidi!


Lakini kwa nini wasiende Mahakamani tu ili Mahakama itoe amri ya kutolewa kielelezo hicho. Maana hata Polisi wakikipata hawana kazi nacho- watadai wanaenda kuchunguza- hakuna haja, acha mahakama ikione ikikubali na kama watakuwa na mashaka watawapa Polisi wakachunguze! Kiherehere cha nini?

CDM mna plan B? Maana mkulu akichelewa mno, hizi propaganda zitazidi na mwisho watawapakazia eti mmechakachua. Ipo haja ya kwenda mahakama ya watu- Peoples Power!
 
Safi kamanda, wao kama wana tuhuma na Mh. Mbowe waende mahakamani kumshtaki. keep it up CDM.
 
Logic ya polisi siielewi kabisa. CDM imewatuhumu ninyi, na ushahidi unawahusu ninyi, then mnalazimisha mpewe ushahidi. Mbowe akitoa ushahidi kwa polisi yatakuwa maajabu ya karne.

Nawashauri polisi wapeleke kesi mahakamani.


Kweli kabisa,hakika umeongea kweli...
 
Nilifaulu vizuri sana, nikakatwa jina langu nafasi yangu akapewa Mkatoliki wakati wa Nyerere. Nikapelekwa shule za "private" nje ya Tanzania, sijawahi kufeli hata mara moja maishani mwangu.

Wewe ni muongo sema ulifeli tu usidanganye watu eti ulikatwa jina baada ya kufaulu! Huna tofauti na Mwanaasha Jakaya Kikwete aliyepata div. 0 pamoja na fursa zote alizonazo! Kwa jinsi ulivyo na mawazo yaliyo pinda hapa ni dhahiri kuwa ulifeli tu!
 
Kikwete amemtaka rais Bashir kuwasaka na kuwakamata watu waliowaua askari wa JWTZ lakini mwenyewe ameshindwa kuwasaka waliorusha mabomu na kuuawa raia wasio na hatia mchana kweupe!

.
Siku serikali ya Jk itakapo wakamata waliorusha bomu katika mikutano ya kanisani na ule wa Chadema ndipo atakapokuwa na haki ya kumtaka rais wa sudan akamate waliowaua makamanda wetu. Halafu toka ccm na serikali yake washitukiwa kujihusisha na mabomu ya Arusha waislamu wa Tanzania wamepumua na kustarehe kwa sasa maana mchawi wao aliyekuwa anafanya matukio ili kuwasingizia kwa kukuza mtafaruku kati ya waisilamu na wakristo kwa maslahi ya kisiasa amekamatwa kwa kufumaniwa. Kweli Mungu mkubwa hawezi kukuacha kudanganya watu waote na kwa wakati wote.
Nashindwa kuelewa kigugumizi cha rais kuunda tume huru ya kimahakama ni nini? Sipati picha kwa kweli na sijui dhamira ya rais wetu imeuawa na nini/nani.
.
 
Kwani safari hii kaandaa shilingi ngapi ya kuwahonga majaji make ya lwakatare aliandaa kiasi kikubwa.
Join Date : 15th June 2013
Posts : 1,544
Rep Power : 614
Likes Received147
Likes Given10



Angalieni huyu mtu join date ni juzi tu lakini hadi sasa amepost 1544 hawa ndio wale BUKU SABA United aka NCHEMBA United waliosajiliwa juzijuzi tu na wazee wa lumumba,hawa ndio wale waliotumwa na bwana wao Nchemba waje kwa fujo humu JF kuleta propaganda za kipuuzi.Haya wahi buku saba zako Lumumba mapema kesho siku imeisha hiyooo.
 
Wewe ni muongo sema ulifeli tu usidanganye watu eti ulikatwa jina baada ya kufaulu! Huna tofauti na Mwanaasha Jakaya Kikwete aliyepata div. 0 pamoja na fursa zote alizonazo! Kwa jinsi ulivyo na mawazo yaliyo pinda hapa ni dhahiri kuwa ulifeli tu!

Ahsante, wewe uliyefaulu tupo hapa pamoja na nnakuwacha mbali sana, au sio?
 
Wanaogopa nn kuteua hiyo tume?au serikali na polisi ndiyo wahusika?siku zote matukio makubwa km hayo yakitokea huwa kunauundwaji wa tume,ss hili vipi?
 
Yaani mtuhumiwa anaandika barua apelekewe ushahidi ofisi kwake sio mahakamani? kweli kabla ya ukombozi tutaone mengi, hajarukwa na akili au hajui kazi ya hakimu, sharia msumeno lazima na wao wafike mahakamani kujitetea, sijui tumuombe nao awachukue maelezo??? CDF?
 
Kwa maana hiyo kama Mbowe asingekuwa na ushahidi, ndo basi tena, uchunguzi wa tukio la Soweto ungebaki kuwa historia bila kukamatwa mtu yeyote? Wale mapolisi waliokuwepo uwanjani wakati tukio likitokea hawakuona lolote? Mwigulu na Lukuvi si pia wanao ushahidi kuwa ni CDM imejilipua, mbona hawabughudhiwi na Polisi ili nao watoe ushahidi wao?
Mkuu mambo yanayofanywa na serikali yetu yetu yanatia aibu sana
 
CDM mtapata taabu sana! Ni kipi hao Polisi wamefanya kinachoweza kutufanya tuamini kwenye deadlines wanazotoa!? Kuna uharaka gani wa kupata huo ushahidi kutoka kwa Mbowe? Kama kuna uharaka huo basi wamwombe JK aharakishe kuundwa kwa tume huru, au aamrishe CDM watoe huo ushahidi!


Lakini kwa nini wasiende Mahakamani tu ili Mahakama itoe amri ya kutolewa kielelezo hicho. Maana hata Polisi wakikipata hawana kazi nacho- watadai wanaenda kuchunguza- hakuna haja, acha mahakama ikione ikikubali na kama watakuwa na mashaka watawapa Polisi wakachunguze! Kiherehere cha nini?

CDM mna plan B? Maana mkulu akichelewa mno, hizi propaganda zitazidi na mwisho watawapakazia eti mmechakachua. Ipo haja ya kwenda mahakama ya watu- Peoples Power!
Mkuu naomba kusaidiwa,Hivi pale uwanja wa Soweto hapakuwa na askali polisi-Je kazi yao ilikuwa ni nini? Baada ya amani kutoweka na watu kupoteza maisha polisi waliokuwepo wametoa ushahidi gani wa kile kilichotokea as nafikiri wana ushahidi wa awali wa kile kilichotokea-Vinginevyo kila tuhesabu hatuna polisi
 
Hapo kwenye bold? Umelewa futari weweeeeeeeeeeeeee??????????

Dah, labda ungesema swaum, maana hapa nilipo ndio kwanza inakaribia saa saba mchana na futari mpaka kwenye kukaribia saa nne ya usiku, upo hapo ulipo?
 
Kauri hii siyo bure polisi wawe makini anaweza kufa mtu hawa watu kuuwa kwaokama kawa tu,polisi jiandaeni mwenzenu hamaanishi mahakama kweli ni lugha ya picha tu.


Umekwama wewe,huna lolote.
 
Mbowe heshimu mamlaka,Mbowe heshimu roho za watu wa Arusha waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu ili waliyofanya wahukumiwe hapa duniani na akhera.Msuguano na polisi hautokupa umaarufu zaidi ya kuonekana mpuuzi mbele ya wenye kujitambua.

Mbowe atakuwa pinda akitoa ushaidi polisi,ambao ndio watuhumiwa no1.iundwe tume kama ile ya wafanyabiashara wa madini wa ulanga waliouwawa na polisi mwabwepande.
 
Unaposema fanyeni kama mlivyofanya kwa Mwangosi una maana gani, baada ya mkanda kuonyeshwa unajua kilichoendelea, Chadema huwa hawakosei mara mbili, kama unaona Mbowe kuukalia mkanda ni kinyume cha sheria kawaambia mpelekeni mahakamani mengine ni blahblah tu endelea kufurahisha jamvi.

Video ya Mauaji ya Mwangosii ipo jamvini na unafiki wa serikali tunauona.. na hata ndugu wa marehemu wanajua nani aliyemuua ndugu yao.. hii ni haki ya kupata habari.. kuuendelea kuushikilia huu mkanda ni kuwanyima makusudi wafiwa na waadhirika nafasi ya kuupata ukweli ambalo ni kosaa si la kisheria peke yake kibinaadamu pia unawakosea hata ndugu na waadhirika woteee ambao hawapo katika huo ubishanio wa chadema na polisi.. Lengo la CDM siku zote lazima liwe kujiepusha na misuguano inayoongeza chuki na maumivu kwa raia na wanachama wake.. basi kama mnaona hii video ni nzuri sanaa mkae muanganie nyie na familia zenu. Hii sio video ya send offf wala harusii!!!??? Acha siasa jombaa hiiyo sio video ya kukaa nayo hata dakika chache na sikutegemea mbowe aeendelee kuikumbatia, hii serikali sio sikivu hata kidogo tupe video tutajua nini cha kufanya! Huyu aliyefanya haya mauaji alitakiwa muda mrefu sasa awe anaishi Segerea. Hii video ikitoka hata kama serikali itakaa kimya ila aliyetelekeza haya mauaji hataliona jua akiwa uraiani.. Na serikali lazima itamuweka ndani hata kama haipendii...... NARUDIA TENA KUENDELEA KUNG'ANG'ANIA HII VIDEO NI ''VIOLATION OF PUBLIC INTEREST; TUMIENI NJIA YEYOTE HII VIDEO ITOKE TUIONE NA SI KUENDELEA KUIKALIA AS IF NI MKANDA WA SEND OFF.. HUO SI MKANDA WA SEND OFF.... MNATAFUTA CHUKI TUUU KWA VICTIM NA RAIA.. HUU NI USHAHIDI MUHIMU SANA WA UHALIFU ULIOTENDEKA THIDI YA BINAADAMA NA TUSIPENDA KUNG'ANG'ANIA CRIMINAL CASE FOR OUR POLITICAL REASONS...... "" TUKUMBUKE MUHALIFU ANAENDELEA KULA BATAA TUUU WAKATI UBISHI UNAENDELEA NA TUNAONGEZA CHUKI NA MACHUNGU KWA VICTIM WA HILI JANGA....
 
Back
Top Bottom