Mbowe: Polisi tukutane Mahakamani ila siwapi Ushahidi

Mbowe: Polisi tukutane Mahakamani ila siwapi Ushahidi

Wakuu, nimemsikiliza baba kundambanda akiimba kuhusu usalama wa taifa.Kweli polisi ni uhasama wa raia!Polisi+CCM=Policcm
 
Hivi katika hili nani anatakiwa kwenda Mahakamani, POLISI au MBOWE? Polisi ni taasisi inayofanyia uchunguzi sasa kama mwenye ushahidi asipokuwa na imani na Polisi yeye ndiye anapaswa kwenda mahakamani na siyo vinginevyo. Hakuna serikali yoyote diniani ambayo rais wake hushinikizwa na wanasiasa kuunda tume.
 
Safi sana Mbowe, licha ya kulinda msimamo wa Chama chako, hukuingilia pia waandishi wa gazeti lako kukuandika kuwa umewagomea polisi, magazeti ya serikali, na wamiliki wengine wa magazeti, na vyombo vingine vya habari jifunzeni mfano huu, unajenga uhuru na demokrasia nchini
 
Mbowe heshimu mamlaka,Mbowe heshimu roho za watu wa Arusha waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu ili waliyofanya wahukumiwe hapa duniani na akhera.Msuguano na polisi hautokupa umaarufu zaidi ya kuonekana mpuuzi mbele ya wenye kujitambua.
 
Chagonja ndio ambaye ilitakiwa wamuwekee masaa ya kuwakilisha uchunguzi wake na sio victims!!kweli nmeamini CIA na FBI walipofika Tz walistahili kuyafanya yote... Mliyosikia kwa sababu wanayohabari ya policcm,na ndo mana hadi Al-haji wa kanda maalum aliinamishwa akanuswa kwa nyuma na jibwaa-alipotoka hapo ikabidi akatawadhe apate udhu huku akiwa anajisonya mwenyewe kwa kudharirishwa

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mbowe heshimu mamlaka,Mbowe heshimu roho za watu wa Arusha waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu ili waliyofanya wahukumiwe hapa duniani na akhera.Msuguano na polisi hautokupa umaarufu zaidi ya kuonekana mpuuzi mbele ya wenye kujitambua.

Muda mwingine shirikisha kichwa ,kwani Mbowe ndo Chagonja?aliyeunda tume ndo awakilishe ushahidi na watu wakamatwe waliohusika ,hadi leo hii ushawahi hata kuambiwa wamefikia wapi uchunguzi wao zaidi ya kudanganywa FBI wametinga Arusha wakati US Embassy walikanusha kuwa ni uongo?shame on u

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mbowe heshimu mamlaka,Mbowe heshimu roho za watu wa Arusha waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu ili waliyofanya wahukumiwe hapa duniani na akhera.Msuguano na polisi hautokupa umaarufu zaidi ya kuonekana mpuuzi mbele ya wenye kujitambua.
Go to hell!
 
Muda mwingine shirikisha kichwa ,kwani mbowe ndo chagonja?aliyeunda tume ndo awakilishe ushahidi na watu wakamatwe waliohusika ,hadi leo hii ushawahi hata kuambiwa wamefikia wapi uchunguzi wao zaidi ya kudanganywa FBI wametinga Arusha wakati Us embassy walikanusha kuwa ni uongo?shame on u

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Polisi waende mahakamani kufanya nini? hivi mtuhumiwa na mtuhumu nani anakwenda mahakamani? MBOWE mwenyewe anasema Polisi ni watuhumiwa yeye aende mahakani, Polisi wanachokitaka ni ushahidi waufanyie kazi kama wao ndo watuhumiwa basi watasubiri wapelekwe mahakani.
 
Hivi katika hili nani anatakiwa kwenda Mahakamani, POLISI au MBOWE? Polisi ni taasisi inayofanyia uchunguzi sasa kama mwenye ushahidi asipokuwa na imani na Polisi yeye ndiye anapaswa kwenda mahakamani na siyo vinginevyo. Hakuna serikali yoyote diniani ambayo rais wake hushinikizwa na wanasiasa kuunda tume.


Mkuu huko duniani kuna utawala wa sheria hapa kwetu hakuna, polisi ni watuhumiwa watapewaje ushahidi? hata pale ambapo kuna ushahidi wa polisi kuhusika moja kwa moja sheria haichukui mkondo wake, kwa mfano kuna ushahid wa picha polisi wakimshambulia mwandishi MWANGOSI, haitoshi walimuua, kitendo cha RPC kuamrisha polisi kuwapiga waandishi wa habari tu ilikuwa kosa la jinai, kwaani waandishi wa habari walikuwa kazini kama polisi, sasa wewe unataka mbowe aende mahakamani, kesi zinafunguliwa mahakamani au polisi? ni nani atakayesoma mashtaka mahakamani? ni nani atapeleleza kesi hii kama siyo polisi? THINK BIG.
 
Mbowe heshimu mamlaka,Mbowe heshimu roho za watu wa Arusha waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu ili waliyofanya wahukumiwe hapa duniani na akhera.Msuguano na polisi hautokupa umaarufu zaidi ya kuonekana mpuuzi mbele ya wenye kujitambua.

Mamlaka isiyojiheshimu wala kufuata sheria ya nchi haistahili heshima hata kidogo. Haikuwa mamlaka hii iliyovunja haki za kibidamu na hata kukatiza uhai wa raia (Daudi Mwangosi) asiye na hatia kule Mufundi? Ni nini kimeitakasa ghafla mamlaka hii hata ipewe heshima unayodai?
 
Mbowe heshimu mamlaka,Mbowe heshimu roho za watu wa Arusha waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu ili waliyofanya wahukumiwe hapa duniani na akhera.Msuguano na polisi hautokupa umaarufu zaidi ya kuonekana mpuuzi mbele ya wenye kujitambua.


Unaweza kuwa mjinga usijhitambue na unaweza kuwa -------- usijitambue lakini uwezo wako wa kufikiri unaweza kunaksi ujinga na upumbavu wako, kwa kutoitumia hekima na akili uliyopewa na mungu wako. Tanzania ni nchi ya propaganda, watu wanaua au kuuliwa lakini sheria haichukui mkondo wake, Hivi km wewe ungekoswa koswa na bomu ungefanya nini? mwenye kazi ya kukamata na kushtaki ni polisi au mbowe? kama mbowe hataki kupeleka ushahidi polisi si wamshtaki mahakamani lili mahakama imlazimishe kuupeleka ushahidi mahakamani? Tatizo mehemko ya magamba inaongoza fikra zako.
 
Hivi katika hili nani anatakiwa kwenda Mahakamani, POLISI au MBOWE? Polisi ni taasisi inayofanyia uchunguzi sasa kama mwenye ushahidi asipokuwa na imani na Polisi yeye ndiye anapaswa kwenda mahakamani na siyo vinginevyo. Hakuna serikali yoyote diniani ambayo rais wake hushinikizwa na wanasiasa kuunda tume.

Hivi unaijua sheria au mambo yenu ya Lumumba? Polisi ndio waliomwita Mbowe na kumwagiza awape ushahidi. Mbowe amesema yeye hawapi ushahidi. Kama kitendo cha Mbowe kuwanyima polisi ushahidi ni kinyume cha sheria basi wa kwenda mahakamani siyo mvunja sheria, hapo Mbowe akafanye nini mahakamani?

Unaposema Mbowe aende mahakamani, amekwisha itwa? kwani mahakamani unaenda kwa kuamua tu?
 
Watanzania wenzetu ndugu wa Morogoro waliualiwa kwa usimamizi wa mkuu wa jeshi la polisi kanda ya DSM, huku wakijua sheria wakafanya makosa makusudi kwa kumshtaki kuua kwa kukusudia, wakati kwenye tukio la kuua hakuwepo, walijua kuwa mwisho itakuwaje, si jeshi hili hili la polisi? acheni kuchezea roho za watanzania. tumshukuru MUNGU kwa kuendelea kutupa roho za uvumilivu kama siyo woga, kwaani kwa matendo yanayofanywa na jeshi letu la polisi badala ya lulinda raia sasa linaua raia wake basi halina hadhi ya kuendelea kutulinda.
 
Polisi waende mahakamani kufanya nini? hivi mtuhumiwa na mtuhumu nani anakwenda mahakamani? MBOWE mwenyewe anasema Polisi ni watuhumiwa yeye aende mahakani, Polisi wanachokitaka ni ushahidi waufanyie kazi kama wao ndo watuhumiwa basi watasubiri wapelekwe mahakani.

Sasa mbona polisi wanashindwa kusubiri Mbowe afungue kesi? kwanini wao wanataka awapelekee ushahidi badala ya kuupeleka mahakamani? tangu lini mtuhumiwa akadai apelekewe ushahidi wa tuhuma zake nje ya mahakama?
 
Back
Top Bottom