Mbowe: Polisi tukutane Mahakamani ila siwapi Ushahidi

Mbowe: Polisi tukutane Mahakamani ila siwapi Ushahidi

Nakubaliana na wewe baadhi ya mambo, ingekuwa vyema na busara kwa mbowe au chadema kuutoa ushahidi huu kwa umma, vyombo, vya habari na wanaharakati ili hatua stahiki zichukuliwe.. Kuendeleza ubishi na vyombo hivi vya dola ambavyo historia inaonyesha sio sikivu na serikali yetu hufanya kazi kwa matukio. Kulirefusha hili jambo ni kuurefusha msiba wa ndugu zetu na kuendelea kutupa machungu bila sababu yeyote ya msingi. Please please Mhe Mbowe, Chadema na Serikali yetu please spare some courtesy to our brother and sister by letting the truth to come out. Acheni kuwatesa ndugu zetu kwa kuukalia ukweli be serious Let them rest in peace..... Kwa mtu yeyote aliyepoteza ndugu kwenye msiba huu hizi zote ni sarakasi.. Wekeni ushahidi humu kama tulivyoupata wa Mwangosi na tutajua mnafiki ni nani... kuendelea kulivuta jambo hili kutapunguza hata nguvu ya huo ushahidi maana wapiga propaganda watasema CDM iliukalia ushahidi makusudi ili iuchakachue na hili litakapotokea huo ushahidi utakosa credibility na watu hawatauamini na wataufanya mzaha...... TUNAOMBA HAYA YAFIKIKE MWISHO WAKE.. KAMA KWELI CHADEMA WANA USHAHIDI HUU NA WAMEUKALIA WANAFANYA MAKOSA MAKUBWA SANAA KWA WAHANGA WA TUKIO HILI NA HAWAWATENDEI HAKI HATA KIDOGO MAREHEMU NDUGU ZETUU... NA MNAWAPA NAFASI YA KUTENGENEZA PROPAGANDA ZA KUUZIMA UKWELI PALE UTAKAPOTOLEWA HADHARANI.. TUNA KILA HAKI YA KUJUA NINI KILICHOTOKEA SIKU ILE, SI MBOWE WALA SI POLISI MWENYE MAMLAKA YA KUTUNYIMA KUUJUA UKWELI HUU.. MBOWE NA CHADEMA LAZIMA MUWE NA DEDLINE MLIYOJIWEKEA HAMUWEZI KUKAA NA USHAHIDI WA MAUAJI YA RAIA NA KUTUNYIMA HAKI YA HABARI ETI KWA SABABU RAIS HATAKI KUUNDA TUME... TO HELL NA TUME YAO... TUNAHITAJI KUJUAAA.. WEKA VIDEO DUNIA NZIMA IONE UDHALIMU ULITENDAKA DHIDI YA RAIA WASIOKUWA NA HATIAA.. ZAIDI YA HAPO WOTEE MNACHEZA NGOMA ZA KWENU KWENYE MAKABURI YA NDUGU ZETU... AND YOU DESERVE PURNISHMENT

Chadema haifanyi kazi ya Jeshi la police, tumeshatoa ushauri kwa serikali na kwa Rais Kikwete waunde tume huru ya kijaji kuchunguza mauji yote ya kisiasa yaliyofanyika kwa wananchama na viongozi wa chadema hawataki, kwanini tutoe ushahaidi kwa watu wasioweza kuchukua hatua ya kukomesha mauji haya, wanafanya mambo kinafiki tu, na watu wanakufa rais Kikwete hata hajali hata pole kwa Chadema au kwa wananchi wa Arusha hakutoa, hivi nyie watu mna akili ngumu kiasi gani kushindwa kuelewa hii serikali ya akina Mwigulu ndo inahusika na haya matukio? Halafu mnashabikia eti chadema itoe ushahidi, ushaidi iutoe kwa nani? Kikwete akishindwa kuchukua hatua tunapeleka ushahidi wetu kwenye vyombo vya kimataifa na tutamshitaki kikwete na serikali yake huko..
 
Unapokuwa na Rais anayewaza ndoa tu badala ya maendeleo ni hatari kwa taifa

images

Mungu wangu.!?
------ kwa kupenda penda mbu.n.e.!!!
Akili zake zinawaza mambo ya chumbani tu.!!
 
Hivi katika hili nani anatakiwa kwenda Mahakamani, POLISI au MBOWE? Polisi ni taasisi inayofanyia uchunguzi sasa kama mwenye ushahidi asipokuwa na imani na Polisi yeye ndiye anapaswa kwenda mahakamani na siyo vinginevyo. Hakuna serikali yoyote diniani ambayo rais wake hushinikizwa na wanasiasa kuunda tume.
Hapa ni kwamba kuna watu wamepoteza maisha (uhai) ambao unapaswa kulindwa na huyu unayemtetea (RAIS) kama taasisi. Na moja ya vyombo vya taasisi hii ni Polisi, na hawa wanatuhumiwa kuwa wamehusika katika mauaji haya.Halafu hawahawa polisi wanaotuhumiwa na wenye jukumu la kuchunguza pamoja na kukamata wahalifu na kuwapeleka ktk vyombo vya sheria (mahakamani) wanamlazimisha raia anayewatuhumu na waliyetaka kumdhuru awapelekee ushahidi wa tukio hilohilo wanalodaiwa kuhusika!!.Hivi katika mazingira haya ni nani sasa aamue??

Hapa nionavyo mimi ni kuwa SI JESHI LOTE la polisi limeharibika kwa kiwango tunachoweza kuaminishwa. Lakini pia ni UKWELI USIOPINGIKA kuwa ndani ya jeshi la polisi kuna mtandao mkubwa wa maofisa jeshi hili ambao wanatumika kwa maslahi ya kisiasa hasa maslahi ya chama tawala.Na hapa ndipo Rais kama mtu wa mwisho katika mamlaka za nchi hii anapaswa kuingilia kati ili kuweka mambo sawa ndani ya utawala wake, kukaa kimya hata yeye anaweza kuanza kutiliwa shaka vilevile na ikifikia hatua watu wasimwamini hata Rais wao,basi hapo tutakuwa tunaelekea kwenye kuparanganyika kama taifa!

Umesema kama Mbowe na CHADEMA hawaiamini polisi wao ndiyo waende mahakamani, that's good. Swali ni hili, kwa nini polisi wanamuandama na kumuona yeye kama ni mhalifu? Kwa nini wanahaha hivi? Kwani wasiwekeze nguvu zao kuchunguza tukio zima na kwa maana hiyo waliodai kuwa na ushahidi wa hili ni wengi akiwemo Lukuvi (waziri wa serikali) na Mwigulu Nchemba Naibu katibu mkuu wa CCM ambacho nacho kinatuhumiwa pia?? Je hawa nao si wanapaswa kitwa mara kwa mara polisi kama kweli polisi wanafanya uchunguzi serious wenye nia njema?? Hapa si Bure,kuna kitu polisi wanataka kuficha na CDM wamekiona labda!!
 
Chadema haifanyi kazi ya Jeshi la police, tumeshatoa ushauri kwa serikali na kwa Rais Kikwete waunde tume huru ya kijaji kuchunguza mauji yote ya kisiasa yaliyofanyika kwa wananchama na viongozi wa chadema hawataki, kwanini tutoe ushahaidi kwa watu wasioweza kuchukua hatua ya kukomesha mauji haya, wanafanya mambo kinafiki tu, na watu wanakufa rais Kikwete hata hajali hata pole kwa Chadema au kwa wananchi wa Arusha hakutoa, hivi nyie watu mna akili ngumu kiasi gani kushindwa kuelewa hii serikali ya akina Mwigulu ndo inahusika na haya matukio? Halafu mnashabikia eti chadema itoe ushahidi, ushaidi iutoe kwa nani? Kikwete akishindwa kuchukua hatua tunapeleka ushahidi wetu kwenye vyombo vya kimataifa na tutamshitaki kikwete na serikali yake huko..

The problem ya wale mnaoshabikia huu mnyukano hamuoni kwamba hiii sii issue ya CDM Vs serikali peke yake wapo third part wanaoumia na huu msuguano. Luck for you two you have nothing to loose but the victim this shenanigan is painful every step you take.. Tunajua polisi ni waajiriwa wa kudumu wa serikali na wao hata ukweli usipotoka watapata mshahara kama kawaida,, kwa viongozi wa chadema your the victim.. Hiii ni kesi ya jinai, kama hamuwaamini polisi na since sioni hata dalili za kuundwa tume utueni huo mzigo, wekani ushahidi wazi kila mtuu auonee. Kuendelea kulumbana na polisi ni kujenga chukii na wahanga wa mlipuko huu na kutowatendesa haki wale waliopoteza maisha yaoo.. polisi tunawajua, they have nothing to loose... Hili jambo lazima liwe na mwisho.. KWANGU PANDE ZOTEE MBILI MNA-MAKOSA NA SINCE HAMUAMINIANI TUPENI HUO USHAHIDI SISI NA DUNIA NZIMA TUUONE.. FANYENI KAMA ILIVYOKUWA KWA MWANGOSI USHAHIDI UPO KWEUPE NA HAKUNA UBISHI NA PLEASE MSIINGIZE SIASA KWENYE HILIII MAANA.. YEYOTE ANAYECHEZA NA HILI ANATAFUTA CHUKI TUU.. KUMBUKA KUNA WATU WAZIMA AMBAO NI WAZAZI WAMEKUFA NA KUNA WATOTO WAMEPIGWA RISASI. TUAMBIENI MBAYA WETU NI NANI ILI TUCHUKUE HATUA WENYEWE... Mbowe kukalia huo ushahidi ni makosa maana anavunja sheria. Sheria ni taratibu tulizoweka sisi watanganyika ili kuleta haki na usawa. Tukiweka siasa pembeni hebu fikiria ingekuwa binti yake Mbowe AU binti yako kauwawa katika tukio lile angeendelea kukalia huo ushahidi na kusema mpaka rais aunde tume?!! Hii ni kesi ya jinai kaka na tuache siasa kama haimani mahakama avipe ushahidi vyombo huru vya habari, wanaharakati, balozi za njee ili haki itendeke.. Hii ni kesi ya ngedere unang'ang'ania Nyani aanzishe Mahakama kweli kutakuwa na hakii..?!! CHADEMA HII VIDEO KAMA MNAYO SI MALI YENU NA KUENDELEA KUING'ANG'ANIA NI "VIOLATION OF PUBLIC INTEREST".. TUMIENI NJIA YEYOTE HII VIDEO ITOKE MIKONONI MWENU IWE MALI YA UMMA MZIMA; TUIONE NA SI KUENDELEA KUKALIA USHAHIDI AS IF NI MKANDA WA SEND OFF.. HUO SI MKANDA WA SEND OFF.... MNATAFUTA CHUKI TUUU KWA VICTIM NA RAIA TUSIOPENDA KUONA CRIMINAL ACT ZINAGEUZWA NA KUWA SIASA.... TUJIFUNZE KUUITA UHALIFU NI UHALIFU HATA KAMA UMEFANYIKA KWENYE KUMBI ZA SIASA, KUINGIZA USHABIKI WA SIASA KATIKA HILI KUTACHANGIA SANA KESII HII YA JINAI KUGEUZWA NA KUWA POLITICAL GAME NA TUNAJUA IKISHAFIKIA HUKO THEY NEVER TAKE IT SERIOUS, THEY WILL FIND A POLITICAL SOLUTION FOR THE PROBLEM.. JE NDIO TUNACHOKITAFUTA?!!
 
Savimbi alitamka kwamba anao ushaidi wa mkanda wa video cdm wakipanga utekaji lakini hajawahi andikiwa barua apeleke huo ushaidi mpaka bukobaboy alipoweka youtube....MBOWE HAKUNA KUPELEKA USHAIDI KWA WATUHUMIWA.
Mkuu King Kong III, siyo hivyo tu Mwigulu alidai Arusha mkichagua CHADEMA mtakufa, na watu wamekufa yeye wala hata haguswi kwa lolote, credibility ya police ni zero kwa hili.
 
mapambano baridi kati ya polisi na hawa wanaojiita makamanda wakati hata mgambo hawajapitia.mi naweza kusema sio jambo la kuchekea.
polisi ndio chombo chetu sisi wazalendo.na polisi wanatakiwa kukulinda wewe utake usitake.
mbona hiki kibuli kinataka kuzidi kupita kiasi.unajua libya na syria ilianza kama hivi.
 
mkuu kigezo kimojawapo cha kuwa polisi ni kufeli kidato cha nne au cha sita.

Du kwa hiyo unataka kuniambia kuanzia mwema na wengine wote hapo kati mpaka Advera ni waliofeli??!!
 
kwaNini ushahidi upelekwe polisi, kwani wao ni mahakama. Kisheria Kuna mbinu za kutoa vielelezo so kukurupuka tu kwani ushindi WA Jedi ni vielelezo. Mh. Mbowe tuku pamona mini kama mfusi Wako.
 
Kwa maana hiyo kama Mbowe asingekuwa na ushahidi, ndo basi tena, uchunguzi wa tukio la Soweto ungebaki kuwa historia bila kukamatwa mtu yeyote? Wale mapolisi waliokuwepo uwanjani wakati tukio likitokea hawakuona lolote? Mwigulu na Lukuvi si pia wanao ushahidi kuwa ni CDM imejilipua, mbona hawabughudhiwi na Polisi ili nao watoe ushahidi wao?

Asante Mkuu,

Magamba na polisism kujichanganya hawaachi. Hivi wamesahau NAPE, LUKUVI, ....walisema wazi cdm imejilipua. Wakachukue ushahidi huko.

I strongly recommend CDM not to provide witness of the soweto event till the president has done his part. Magamba wanafanya wataz wajinga. Juzi wamelipua na kua-apologize baada ya kuona walichokusudia hakikukamilika...
 
kwaNini ushahidi upelekwe polisi, kwani wao ni mahakama. Kisheria Kuna mbinu za kutoa vielelezo so kukurupuka tu kwani ushindi WA Jedi ni vielelezo. Mh. Mbowe tuku pamona mini kama mfusi Wako.

sasa kama alitaka kupeleka mahakamani kwanini alilopoka au we ujui kwamba polisi inamtuhumu mtu kuanzia kauli yake.
ndo mana tunasema matamko yamezidi.chama gani hakijui kuficha nyaraka.
we unajua kabisa kwamba we ni mpinzani alafu unatumia kauli za jazba.na hizo damu mpaka ziwaumbue.
 
The problem ya wale mnaoshabikia huu mnyukano hamuoni kwamba hiii sii issue ya CDM Vs serikali peke yake wapo third part wanaoumia na huu msuguano. Lack for you two you have nothing to loose but for the victim this shenanigan is painful every step you take.. Tuanjua polisi ni waajiriwa wa kudumu wa serikali na wao hata ukweli usipotoka watapata mshahara kama kawaida,, kwa viongozi wa chadema your the victim.. Hiii ni kesi ya jinai kama hamuwaamini polisi na sioni hata dalili za kuundwa tume utueni huo mzigo weka ushahidi wazi kila mtuu auonee. Kuendelea kulumbana na polisi ni kujenga chukii na wahanga wa mlipuko huu na kutowatendesa haki wale waliopoteza maisha yaoo.. polisi tunawajua they have nothing to loose... Hili jambo lazima liwe na mwisho.. KWANGU PANDE ZOTEE MBILI MNA-MAKOSA NA SINCE HAMUAMINIANI TUPENI HUO USHAHIDI DUNIA NZIMA TUUONE.. FANYENI KAMA ILIVYOKUWA KWA MWANGOSI USHAHIDI UPO KWEUPE NA HAKUNA UBISHI NA PLEASE MSIINGIZE SIASA KWENYE HILIII MAANA.. YEYOTE ANAYECHEZA NA HILI ANATAFUTA CHUKI TUU.. KUMBUKA KUNA WATU WAMEKUFA KUNA WATOTO WAMEPIGWA RISASI TUAMBIE MBAYA WETU NI NANI TUCHUKUE HATUA WENYEWE... Mbowe kukalia huo ushahidi ni makosa maana anavunja sheria. Sheria ni taratibu tulizoweka sisi watanganyika ili kuleta haki na usawa. Tukiweka siasa pembeni hebu fikiria ingekuwa binti yake Mbowe AU binti yako kauwawa katika tukio lile angeendelea kukalia huo ushahidi na kusema mpaka rais aunde tume?!! Hii ni jinai kaka na tuache siasa kama haimani mahakama avipe ushahi vyombo huru vya habari, wanaharakati, balozi za njee ili haki itendeke.. Hii ni kesi ya ngedere unangangania Nyani aanzishe Mahakama kweli kutakuwa na hakii..?!! CHADEMA HII VIDEO KAMA MNAYO SI MALI YENU NA KUENDELEA KUINGANGANIA NI "VIOLATION OF PUBLIC INTEREST".. TUMIENI NJIA YEYOTE HII VIDEO ITOKE TUIONE NA SI KUENDELEA KUKALIA USHAHI AS IF NI MKANDA WA SEND OFF.. HUO SI MKANDA WA SEND OFF.... MNATAFUTA CHUKI TUUU KWA VICTIM NA RAIA TUSIPENDA KUONA CRIMINAL ACT ZINAGEUZWA NA KUWA SIASA..
Unaposema fanyeni kama mlivyofanya kwa Mwangosi una maana gani, baada ya mkanda kuonyeshwa unajua kilichoendelea, Chadema huwa hawakosei mara mbili, kama unaona Mbowe kuukalia mkanda ni kinyume cha sheria kawaambia mpelekeni mahakamani mengine ni blahblah tu endelea kufurahisha jamvi.
 
mapambano baridi kati ya polisi na hawa wanaojiita makamanda wakati hata mgambo hawajapitia.mi naweza kusema sio jambo la kuchekea.
polisi ndio chombo chetu sisi wazalendo.na polisi wanatakiwa kukulinda wewe utake usitake.
mbona hiki kibuli kinataka kuzidi kupita kiasi.unajua libya na syria ilianza kama hivi.
Kumbe unajua kilichotokea waambie polisi kuwa hawana uwezo wa kuua wananchi wote.
 
IKIWA leo ni siku ya mwisho aliyopewa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Jeshi la Polisi nchini kuwasilisha ushahidi wa kuhusika kwa jeshi hilo na mlipuko wa bomu uliotokea mwezi uliopita mkoani Arusha, kiongozi huyo amegoma kuutoa.

Jeshi la Polisi kupitia Mkurugenzi wake wa Makosa ya Jinai Julai 17 lilimwandikia Mbowe barua yenye kumbukumbu namba AR/IR/6223/2013 ikimtaka kupeleka ushahidi wake leo kabla ya saa nane mchana, kiongozi huyo amewataka polisi kumpeleka mahakamani kwani hatawapa ushahidi huo.

Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Mbowe alisema kamwe hawezi kwenda kinyume cha msimamo wa chama chake walioamua kutoukabidhi ushahidi huo kwa polisi hata kama watawapa vitisho kama walivyozoea.

Alibainisha kuwa alipokea barua iliyomtaka aende polisi leo na ataitikia wito huo, lakini hatapeleka ushahidi wanaoutaka, kwakuwa wao ni watuhumiwa.

Alisema CHADEMA ilimwandikia Rais Jakaya Kikwete barua ikimwomba kuunda tume huru ya majaji kwa ajili ya tukio hilo, ambayo wataikabidhi ushahidi wao.

Aliongeza kuwa masuala muhimu yagusayo chama na masilahi ya taifa yanafanyika kulingana na maamuzi ya vikao, hivyo yeye hawezi kwenda kinyume cha kilichoamuliwa.

Kwa mujibu wa Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, suala la Arusha linahusisha viongozi, wanachama na wapenzi wa CHADEMA, hivyo lilifikishwa kwenye vikao na kufanyiwa uamuzi wa kutopeleka ushahidi polisi.

“Nina mambo mengi ya kukutana na polisi, nitaitikia wito wao lakini kuhusu kupeleka huo ushahidi ni msimamo wa chama kwamba hatupeleki… waende mahakamani, wachukue hatua za kisheria au waamue lolote.

“Tunasubiri kauli ya rais ya ama ataunda tume ama hataunda tume huru ya kimahakama yenye majaji. Lakini pia ninamsubiri mwanasheria wa chama ambaye anakuja kutoka Tabora, polisi nitaenda tu,” alisema Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Barua ya polisi
Jeshi la Polisi kupitia Mkurugenzi wake wa Makosa ya Jinai Julai 17 lilimwandikia Mbowe barua yenye kumbukumbu namba AR/IR/6223/2013 ikimtaka kupeleka ushahidi wake Julai 23 (leo) kabla ya saa nane mchana.

“Kutokana na mahojiano uliyofanya na Polisi Mkoa wa Arusha mnamo Juni 20, 2013 kuhusu mauaji yaliyotokana na ulipuaji wa bomu huko Soweto, Arusha ulidai kuwa unao ushahidi unaobainisha wahusika wa tukio hilo.

“Kwa mujibu wa kifungu cha 10 (2) na (2A) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai nchini, sura 20 kama ilivyorekebishwa mwaka 202, unaamriwa kufika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai tarehe 23 Julai, 2013 saa nane mchana bila kukosa na ulete ushahidi huo.

“…Unatahadharishwa kuwa kushindwa au kukataa kufika na kuleta ushahidi huo ni kosa la jinai chini ya sheria iliyotajwa,” inasomeka sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Hussein Laisseri, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai.

Juni 15, mwaka huu wakiwa kwenye mkutano wa wazi uliokuwa ukihutubiwa na Mbowe katika viwanja vya Soweto mjini Arusha wakati wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani wanne, bomu la kutupwa kwa mkono lililipuka na kusababisha vifo vya watu wanne na kuwajeruhi wengine 70.

Awali jeshi hilo lilituma viongozi wake wa juu mkoani Arusha kwa ajili ya uchunguzi, ambapo waliwahoji watu kadhaa akiwamo Mbowe, kwamba alisema alimwona aliyelipua bomu hilo kuwa ni askari polisi na kuweka bayana kwamba hawezi kuutoa ushahidi huo kwa polisi kwa madai kuwa watauharibu.
Investigation by police officer: 10. (2) Any police officer making an investigation may by order in writing require the attendance before himself of any person living within the limits of the station of that police officer or any adjoining station, who, from information given or in any other way appears to be acquainted with the circumstances of the case, or who is in possession of a document or any other thing relevant to investigation of the case to attend or to produce such document or any other thing, and that person shall attend and produce a certified copy of the document or any other thing as so required: Provided that where a police officer receives any certified copy of a document or any other thing he shall issue to the person from whom he received such document or that thing a receipt thereof. (2A) Any person summoned to attend or to produce a document or any other thing relevant to investigation of the case under subsection (2), who refuses or wilfully neglects so to do or who being a witness at such investigation refuses to answer any question put to him or to produce any document or any other thing relevant to investigation commits an offence and shall be liable on conviction to a fine not exceeding five hundred thousand shillings or to imprisonment for a term not exceeding three years or both.
 
Hapa ni kwamba kuna watu wamepoteza maisha (uhai) ambao unapaswa kulindwa na huyu unayemtetea (RAIS) kama taasisi. Na moja ya vyombo vya taasisi hii ni Polisi, na hawa wanatuhumiwa kuwa wamehusika katika mauaji haya.Halafu hawahawa polisi wanaotuhumiwa na wenye jukumu la kuchunguza pamoja na kukamata wahalifu na kuwapeleka ktk vyombo vya sheria (mahakamani) wanamlazimisha raia anayewatuhumu na waliyetaka kumdhuru awapelekee ushahidi wa tukio hilohilo wanalodaiwa kuhusika!!.Hivi katika mazingira haya ni nani sasa aamue??

Hapa nionavyo mimi ni kuwa SI JESHI LOTE la polisi limeharibika kwa kiwango tunachoweza kuaminishwa. Lakini pia ni UKWELI USIOPINGIKA kuwa ndani ya jeshi la polisi kuna mtandao mkubwa wa maofisa jeshi hili ambao wanatumika kwa maslahi ya kisiasa hasa maslahi ya chama tawala.Na hapa ndipo Rais kama mtu wa mwisho katika mamlaka za nchi hii anapaswa kuingilia kati ili kuweka mambo sawa ndani ya utawala wake, kukaa kimya hata yeye anaweza kuanza kutiliwa shaka vilevile na ikifikia hatua watu wasimwamini hata Rais wao,basi hapo tutakuwa tunaelekea kwenye kuparanganyika kama taifa!

Umesema kama Mbowe na CHADEMA hawaiamini polisi wao ndiyo waende mahakamani, that's good. Swali ni hili, kwa nini polisi wanamuandama na kumuona yeye kama ni mhalifu? Kwa nini wanahaha hivi? Kwani wasiwekeze nguvu zao kuchunguza tukio zima na kwa maana hiyo waliodai kuwa na ushahidi wa hili ni wengi akiwemo Lukuvi (waziri wa serikali) na Mwigulu Nchemba Naibu katibu mkuu wa CCM ambacho nacho kinatuhumiwa pia?? Je hawa nao si wanapaswa kitwa mara kwa mara polisi kama kweli polisi wanafanya uchunguzi serious wenye nia njema?? Hapa si Bure,kuna kitu polisi wanataka kuficha na CDM wamekiona labda!!

Swali lingine ni kwamba kuna kesi polisi wanachunguza miaka na miaka bila kukamilika na hata wakati mwingine mahakama kulazimika kuzifuta kutokana na kukosa ushahidi. Kwa nini ushahidi wa Mbowe upewe kikomo (July 23, 2013)? Ni kwa maana kwamba ushahidi huu ulikuwa umekamilika? Kulitangazwa dau la mihela kwa yule atakayepeleka ushahidi kuhusu wahusika wa bomu. Je, na wao wamewekewa muda au bado zoezi linaendelea? Kuna pia baadhi ya vigogo wa CCM walidai waliorusha bomu ni Chadema wenyewe. Je, na hawa wanaamriwa wapeleke ushahidi wao au vipi? Why has everything narrowed down to Mbowe only?
 
Jamani naomba kujua kamanda mbowe ameshaenda polisi? Na ilikuwaje alipoenda
kujisalimisha kwa hao manyangau maana mpaka sasa hatujajua sisi tulio a town maana saa nane sizimeshapita?
 
Haswaa hata mimi nimekuwa nikizitafuta habari hizi bila mafanikio, kimya kimetawala
 
Back
Top Bottom