Mbeya: Mahakama imeahirisha kusoma hukumu ya Mdude Nyagali hadi Juni 28, 2021

Nasema hivi, kama dhalimu alijua Mdude anauza unga, kwanini aliagiza atekwe kwanza badala ya kumpeleka mahakamani?
Una uhakika dhalimu wako ndio alimteka?

Mdude ndio huyo yupomahakamani kwa hiyo kama ana hatia mahakama itaamua
 
Kwa hiyo hukumu imeshatoka?
Kushindwa kwa Hakimu kusoma hukumu ni dhahiri kuna mtu mwema ameingilia kati. Labda ni Mungu tulie mshirikisha au Mamlaka ya juu.
Hiyo tu ni ushindi kuliko ushindi wenyewe wa tarehe 28.
 
Kushindwa kwa Hakimu kusoma hukumu ni dhahiri kuna mtu mwema ameingilia kati. Ether Mungu tulie mshirikisha au Mamlaka ya juu.
Hiyo tu ni ushindi kuliko ushindi wenyewe wa tarehe 28.
Mungu siyo optional..
 
Kwa muda huu saa10:30 asubuhi msafara wa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe umewasili hapa katika viwanja vya Mahakama Kuu Mbeya kusikiliza hukumu ya mwanachama wao Mdude, ambaye alishitakiwa kwa makosa ya madawa ya kulevya, uhujumu uchumi nk

Wafuasi wa CHADEMA wamewasili hapa tangu saa 2 asubuhi na kukaa makundi makundi

Lakini mshitakiwa Mdude amewasili hapa katika viwanja vya mahakama mnamo saa tatu 3 akiwa chini ya ulinzi mkali na aliingizwa mahakamani na kupumzishwa kwenye chumba maalum akisubiri kesi yake kuitwa hizi ni picha.

Hizi ni picha za hali halisi mahakani hapa hapa.

=========

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya imeahirisha kusoma hukumu ya kesi ya kada wa Chadema, Mdude Nyangali iliyokuwa itolewe leo Jumatatu Juni 14, 2021.

Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer amesema ameiahirisha kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake na kubainisha kuwa hukumu hiyo itasomwa Juni 28, 2021.

Mdude anakabiliwa na shtaka la kusafirisha heroin gramu 23.4 mwaka 2020.

Akizungumza nje ya mahakama mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amewataka wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu mpaka tarehe iliyopangwa.


PIA, SOMA: Hukumu ya Mdude Nyagali ni leo 14|06|2021

View attachment 1818319
View attachment 1818320
View attachment 1818325
View attachment 1818331
View attachment 1818334

View attachment 1818347

View attachment 1818350

View attachment 1818351
View attachment 1818445
Behold! The ruling is coming from the top heavens.
 
Muwe mnafatilia mambo, karejee misukosuko yake ya 2017, ameshatekwa mara kadhaa, kuteswa na kutupwa na akaokotwa wa wanakijiji akiwa na majeraha. This time awali mlimkamata kwa kutoa lugha chafu, mkaona hamna namna nzuri ya kufanikisha uharamia wenu, ghafla mkampa shitaka la uhujumu uchumi nalo ghafla mkaliondoa. Ghafla mkaweka charge sheet biashara za dawa za kulevya.

Serikali ya mwendazake hata ungekuwa CLEAN kiasi gani, alikuwa anaweza kukufanya atakavyo (He was a sadist). Mdude ni mfano tu wa watanzania wengi wenye mawazo kinzani ambao kuwa kwao upinzani ni JINAI kwa nyie CCM na hayati Mwendazake!

Mungu ametuepusha na ANGUKO.
Yule hakuwa kiongozi maana alikuwa zaidi ya shetani kabisa
 
Daaa huyu kiboko sanaaa walimtesa sanaa....kumlawiti pia aliporudi akaendelea vile vile
 
Misukosuko ya wapinzani (watu wenye hoja kinzani) haijaanza kwa Mdude, hata Gwajima aliambiwa anatumia na kuuza kabisa!

Mdude alianza kupata uonevu tangu 2016 hadi sasa, awali kuna mashtaka amewahi kuishinda serikali mahakamani. Ndiyo JIWE akaona atumie mbinu OVU ikiwemo kwanza kumteka na kumtesa kisha kutupwa akiwa hoi. Akiwa katika wimbi la majeraha akapewa kesi ya kutoa lugha chafu, ghafla ikafa ikaja ya uhujumu uchumi, nayo ikafa ikaja ya dawa la kulevya! Tatizo unaandika ukiwa umeshiba ugali wa shemeji na bando la dada yako, hujui how things work kwenye tawala za KIDHALIMU kama alivyokuwa JIWE!
Usimjibu huyu
 
Makamanda tukubali ukweli kuwa Mdude alitumika na akabwagwa kama takataka.

Leo kwenda mahakamani na kujazana kisha kutwanga maphoto sio tija. Ukweli ni kuwa alitumika na kubwagwa.
IMG_20210614_195900.jpg
 
Hili jamaa bwana,thread zake zote ni kama jitu ambalo halijakanyaga darasa kabisa. Kwa hiyo ulitaka wafanyeje, wakavamie gereza? Hii ni thread ya tatu au ya nne kuhusu suala hilihili. Kama umeajiliwa kuwa uvccm mtandao hakika unalipwa pesa ya bure.
 
Hili jamaa bwana,thread zake zote ni kama jitu ambalo halijakanyaga darasa kabisa. Kwa hiyo ulitaka wafanyeje, wakavamie gereza? Hii ni thread ya tatu au ya nne kuhusu suala hilihili. Kama umeajiliwa kuwa uvccm mtandao hakika unalipwa pesa ya bure.
Alitumika na alitoswa.
 
Back
Top Bottom