Mbeya: Mahakama imeahirisha kusoma hukumu ya Mdude Nyagali hadi Juni 28, 2021

Kwa muda huu saa10:30 asubuhi msafara wa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe umewasili hapa katika viwanja vya Mahakama Kuu Mbeya kusikiliza hukumu ya mwanachama wao Mdude, ambaye alishitakiwa kwa makosa ya madawa ya kulevya, uhujumu uchumi nk...
Mambo mawili makubwa nayaona hapa.Jambo la kwanza mahakamnai ni mahali pa heshima kuu kwa maana ya kuwa watu wanakwenda kuitafuta haki.

Hakimu ni mtu mkubwa sana kwani uamuzi wake unaweza ukaamua hatma ya binadamu mwingine.Kitendo cha HAKIMU kusema hukumu haitasomwa kwa sababu zilizo NJE ya uwezo wake ni cha kutiliwa mashaka ukiangalia hayo mawili yaliyotangulia.

Jambo la pili linahusu waandishi wa habari na hata Chama chenyewe cha Chadema.Hapakuwa na ripoti ya usikilizwaji wa kesi kama wale wa zamani tulivyoshudia wakati wa kesi ya kutaka kupindua nchi 1983 ambapo kila siku maendeleo ya kesi,mahojiano kati ya mawakili angalau yalitupa mwanga wa kujua kinachoendelea.

Humu ndani JF kesi ya mwanzilishi wa JF ilikuwa ikiripotiwa kila siku.Jambo hili linatupa shida ya kuhisi kuwa ni nani mkweli,Nyagali au serikali?
 
Mungu wa Mbinguni ikiwa uliweza kumtoa Petro katikati ya gereza tena chumba Cha ndani Kama maandiko yesamavyo, na ikiwa ulimponya Daniel na Simba wenye njaa Kali ukawafunga vichwa vyao, na pale alipokuomba Joshua jua lisimame na ukafanya hivyo.

Naamini hujabadilika kamwe wewe na mwanzo tena mwisho, asubuhi ya leo najitakaza kwa ajili ya Taifa langu Tanzania, najitakasa kwa ajili ya Rais wangu Samia Suluhu Hassani

Natubu kwa ajili ya jaji Mkuu wa Tanzania, natubu kwa ajili ya majaji wa mahakama kuu ya Mbeya pamoja na jaji atakaehukumu kesi ya mtumwa wako Mdude, Natubu pia kwa ajili ya Mdude.

Najua kila mwanadamu ana mapungu yake na kamwe anakuudhi na kukukosea, inuka eeh Bwana kwenye kiti Cha enzi geuza uso wako ukamwangalie mtoto wako Mdude Leo hii mahakani, simama Mungu wa Ibrahimu, Isack na Yakobo tazama wanao wote waliokusanyika mahamani wakisuburi hukumu watie nguvu wape uvumilivu na huruma pia wape, kafanye Jambo ambalo litaacha midomo ya watu ikiwa wazi ukimtetea waziwazi mtumushi wako Mdude.

Kwa jina la Yesu Kristo wanazareti Naomba nikiamini hivyo ameeni
Amen.
Ubarikiwe mkuu.
 
Watu wameingia gharama kutoka mbali halafu wana ahirisha kirahisi hivyo jamani?

Bongo aisee duh
 
IMG_20210614_115952.jpg



View attachment 1819015

Wamekumbuka kusali siku ya hukumu.

Hawako organized kabisa.

Walitakiwa wawe na makalenda ofisini na majumbani mwao wamuwahi kumuombea hakimu ili Mungu amtangulie kabla hajaandika hukumu. Hapa labda shetani kesha mtangulia hakimu.

hahaha chadema wakianza reality tv itanoga sana!
 
Back
Top Bottom