Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,746
- 218,335
Mdude Nyagali, mmoja wa wazalendo waliokamatwa na polisi mamluki jana wakati wamemsindikiza Wakili Mwabukusi, bado angali anasota rumande kwa makosa yasiyofahamika.
Bali taarifa zilizotufikia ni kwamba Kamanda Mdude amekataa amri ya Polisi kwenda kumpekua nyumbani kwake hadi pale amri hiyo itakapotolewa na Mahakama.
Ikumbukwe kwamba Jeshi la Polisi liliwahi kudhalilika Mahakamani baada ya kubainika kumbambikia Mdude madawa ya kulevya kwa lengo la kumkomoa.
Msiondoke JF kwa sababu mtumishi wenu Erythrocyte nitaendelea kuwaletea kila kitu kutoka kituo cha Polisi Mbeya.