Sanyambila
JF-Expert Member
- Jan 24, 2018
- 339
- 457
Kwa muda huu saa10:30 asubuhi msafara wa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe umewasili hapa katika viwanja vya Mahakama Kuu Mbeya kusikiliza hukumu ya mwanachama wao Mdude, ambaye alishitakiwa kwa makosa ya madawa ya kulevya, uhujumu uchumi nk
Wafuasi wa CHADEMA wamewasili hapa tangu saa 2 asubuhi na kukaa makundi makundi
Lakini mshitakiwa Mdude amewasili hapa katika viwanja vya mahakama mnamo saa tatu 3 akiwa chini ya ulinzi mkali na aliingizwa mahakamani na kupumzishwa kwenye chumba maalum akisubiri kesi yake kuitwa hizi ni picha.
Hizi ni picha za hali halisi mahakani hapa hapa.
=========
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya imeahirisha kusoma hukumu ya kesi ya kada wa Chadema, Mdude Nyangali iliyokuwa itolewe leo Jumatatu Juni 14, 2021.
Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer amesema ameiahirisha kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake na kubainisha kuwa hukumu hiyo itasomwa Juni 28, 2021.
Mdude anakabiliwa na shtaka la kusafirisha heroin gramu 23.4 mwaka 2020.
Akizungumza nje ya mahakama mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amewataka wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu mpaka tarehe iliyopangwa.
PIA, SOMA: Hukumu ya Mdude Nyagali ni leo 14|06|2021
Wafuasi wa CHADEMA wamewasili hapa tangu saa 2 asubuhi na kukaa makundi makundi
Lakini mshitakiwa Mdude amewasili hapa katika viwanja vya mahakama mnamo saa tatu 3 akiwa chini ya ulinzi mkali na aliingizwa mahakamani na kupumzishwa kwenye chumba maalum akisubiri kesi yake kuitwa hizi ni picha.
Hizi ni picha za hali halisi mahakani hapa hapa.
=========
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya imeahirisha kusoma hukumu ya kesi ya kada wa Chadema, Mdude Nyangali iliyokuwa itolewe leo Jumatatu Juni 14, 2021.
Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer amesema ameiahirisha kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake na kubainisha kuwa hukumu hiyo itasomwa Juni 28, 2021.
Mdude anakabiliwa na shtaka la kusafirisha heroin gramu 23.4 mwaka 2020.
Akizungumza nje ya mahakama mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amewataka wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu mpaka tarehe iliyopangwa.
PIA, SOMA: Hukumu ya Mdude Nyagali ni leo 14|06|2021