Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Ukiondoa chakula cha msiba Migagawa yote ya karibu hakuna chochote!. Soda zote zimenunuliwa, maji yote yamenunuliwa, chakula chote kimenunuliwa!.

Nadhani waheshimiwa walloandamana na JK watakuwa wamepitishwa kwanza kupata ndipo waje!. Wale wenzangu na mimi ambao asubuhi hatukuiona na huu mchana ndio huu unapita, leo tutashiriki swaumu ya hiari kwa heshima ya shujaa wetu Regia!.


Itabidi mkimaliza shughuli za maziko muwahi mang'ula, ruaha na mkamba ili muweze "kufuturu" mapema iwezekanavyo.
 
Ukiondoa chakula cha msiba Migagawa yote ya karibu hakuna chochote!. Soda zote zimenunuliwa, maji yote yamenunuliwa, chakula chote kimenunuliwa!.

Nadhani waheshimiwa walloandamana na JK watakuwa wamepitishwa kwanza kupata ndipo waje!. Wale wenzangu na mimi ambao asubuhi hatukuiona na huu mchana ndio huu unapita, leo tutashiriki swaumu ya hiari kwa heshima ya shujaa wetu Regia!.

Pole sana Mkuu, Vumilieni!
 
LEO

attachment.php
 
Waombolezaji wa kweli na uhakika wako msibani leo. Hapa Dar nilijionea waombolezaji feki wengi tu. Wapo waliotaka waonekane kwenye Tv, wapo waliotaka umaarufu wa kisiasa tu, wapo waliotaka kuonesha mavazi na magari yao ya bei mbaya, wapo waliolazimika kuwepo kwa sababu ya nyadhifa zao, wapo waliokwenda kuwaona na kuwashangaa "wakubwa" wetu, wapo waliofuata mapochopocho tu, wapo waliokwenda kutengeneza pesa pia.
Thats life na hiyo iko kila mahali!. Ila kwa sisi tuliokuja kuzika, ukiondoa wale ambao ilibidi waje ama kwa nyadhifa zao au kwa kuwajibika sehemu zao, wengi wa tuliokuja huku Ifakara, tumekuja kwa mapenzi yetu kwa Regia!. Wengine kama mimi sio CCM sio Chadema, sio ndugu, sio rafiki wala hatuna uhusiano wowote na Regia ila tumekuja kwa sababu Regia ni mwanachama mwenzetu wa jf! tumekuja tuu kwa sababu tumeguswa!.
 
Regia siwezi siwezi mama kuendelea kuona watu wako wakibubujikwa machozi.

Nasikia mengi wanayokusema.

Sasa tunakuona uso wako kwa mara ya mwisho,imebaki historia.

Watu wanajipanga kutoa salamu za mwisho,mvua inanyesha kidogo.

Please open you eyes just foa minute Regia.

Nakulilia mama,niliumia hivi siku baba yangu mzazi aliponitoka.

Noooooo!
 
Matola,

Nafahamu na kuielewa concern yako, unaona sote hapa tunajaribu kuwahimiza walioko huko Ifa wajitahidi kutufahamisha kinachoendelea.
Ila mkuu umekuwa mkali sana, Josephine amesha acknowledge kuelewa concern yako na bila shaka ujumbe utamfikia mhusika

Labda nikung'ate sikio kwamba hata mabadiliko yaliyofanyika hivi karibuni na kuteuliwa Mh. Mnyika kuwa Mkurugenzi wa habari na uenezi ilichangiwa pia na concern za wanaJF. Tuwape muda kidogo tu wamalize shughuli za maziko, sina shaka kwamba Dr. Slaa atapita mtaa huu na kusoma mawaidha yetu.

WanaJF
nimesikia concern zenuzenu. Tunaomba radhi kwa usumbufu. Nimekwenda mwenyewe kwa wenye mitambo na nimekuta wakihangaika na network. Tunatambua umuhimu wa kuwajuza kinachojiri. Tutaendelea kuboresha mitambo. Nashukuru baada ya picha zimeanza ku postiwa. Tunawashukuru wana JF na wapenzi wote wa Regia kwa ushiriki wa kina kumsindikiza mpendwa wetu.
 
Back
Top Bottom