Mazishi ya Bilionea SAMBEKE yatikisa mji

Mazishi ya Bilionea SAMBEKE yatikisa mji

Ebana Mangi huyo jamaa alikuwa na bilioni ngapi?
Mkuu unajuwa huyu mtu alikuwa pia akiogopa kufuatiliwa na maccm si unajuwa ukiwa na pesa na mtu kama yule wanaweza kukufilisi.
Sijui kiiasi cha pesa alizonazo,lakini ni ukweli amekopesha watu sana na ana assets zenye kufikia billion ya madafu.

Huyu jamaa tayari alikuwa ni mtu mishemishe.Usitegemee kuona figures za utajiri wake kama unavyoona kwenye forbes.
 
naskia kwenu hamchukuagi riba ila mnagawana faida na mlienmkopesha,. Ila kweli sawa na wale wanaoita kichaa mlemavu wa akili

Hujui kitu wewe ! Biashara imebarikiwa na Riba imelaaniwa !
Nenda Cyprus ukaone kivumbi cha Riba huko, .....mabilionea wa Russia wanalia huko !
Maneno ya Allah SWT hayarudi nyuma !

'Wale walao riba hawasimami ila kama anavyo simama aliye zungwa na Shetani kwa kumgusa. Hayo ni kwa kuwa wamesema : Biashara ni kama riba; Lakini Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara na ameiharamisha riba.........!

Mwenyezi Mungu huiondolea baraka riba, na huzibariki sadaka , na Mwenyezi Mungu hampendi kila mwenye kukanya na afanyae dhambi.
Quran: 2:275-276.
 
Mkuu unajuwa huyu mtu alikuwa pia akiogopa kufuatiliwa na maccm si unajuwa ukiwa na pesa na mtu kama yule wanaweza kukufilisi.
Sijui kiiasi cha pesa alizonazo,lakini ni ukweli amekopesha watu sana na ana assets zenye kufikia billion ya madafu.

Huyu jamaa tayari alikuwa ni mtu mishemishe.Usitegemee kuona figures za utajiri wake kama unavyoona kwenye forbes.
Hakika anastahili kuitwa bilionea
 
sasas mtu anayeweza kopesha bil 5 utamwitaje kama sio bilionea benk zenyewe hupati hicho kiasi huyu ni bilionea kabisaaaa

...Mkuu samahani, wewe binafsi ulikuwepo na kushuhudia mtu akikopeshwa Bilioni 5 ama ndio haya mambo ya kwenye vijiwe vya Gahwa mtu mmoja anasema jambo lisilo ma chemba ya ushahidi lakini makamanda wenzake wanalichukua na kulishadadia??:A S 39:
 
Jamaa hela anazo but sio za kua bilonea. 2tambue nini maana ya bilionea jamani. Kwa pesa za madafu au za mbelembele. maana tukisema bilionea hata hao wasanii tunaowapenda wakina pdidy na mwenzie Jiga huko majuu hawapo kwenye list ya mabilionea. Hizo Bilion $$$$$ zisikie tu kwa hao wakina Andrea Agneli Mzee wa FIATI, FERRALI, BUGATI. Hata huyo Silivio Belusconi sio bilionea ni Milionea tu. Najua Gang Chomba unalijua hilo. Nashangaa Sembuke yupo juu kuliko Boss wako BELUSCONI.?
Mkuu Una ufahamu wa uhakika kuhusu Silvio Berlusconi? Kwa sasa sijui lakini nakumbuka mapato yake ilikuwa 20 bilioni za Euro, watu aliowaajiri 60,000 kwa makampuni yake mfano Mabenki Mediolanum Banca, Mediaset ya Italy, Spain na France, Publishers kama Mondadori, mpira AC Milan, na biashara nyingi nyingine. Japo ukionda Forbes hawamtaji akiwa mwanasiasa ni lazima mali ionekane ni ya Familia. Angalia zaidi Mkuu
 
Hujui kitu wewe ! Biashara imebarikiwa na Riba imelaaniwa !
Nenda Cyprus ukaone kivumbi cha Riba huko, .....mabilionea wa Russia wanalia huko !
Maneno ya Allah SWT hayarudi nyuma !

'Wale walao riba hawasimami ila kama anavyo simama aliye zungwa na Shetani kwa kumgusa. Hayo ni kwa kuwa wamesema : Biashara ni kama riba; Lakini Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara na ameiharamisha riba.........!

Mwenyezi Mungu huiondolea baraka riba, na huzibariki sadaka , na Mwenyezi Mungu hampendi kila mwenye kukanya na afanyae dhambi.
Quran: 2:275-276.

amka kafanye kazi kushinda msktn sio tija!
 
amka kafanye kazi kushinda msktn sio tija!

Tumeambiwa tukishamaliza kuswali .... Basi tutawanyike katika ardhi kutafuta riziki !

'Itakapo kwisha sala, tawanyikeni katika nchi mtafute fadhila za Mwenyezi Mungu, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi ili mpate kufanikiwa'
Qur'an: Al Jumaa: 62: 10.
 
Kwa kweli mimi najua alikuwa ni mmiliki mwenza wa ASANTE TOURS yeye pamoja na Cuthbet Mbowe .pia alikuwa ndio mkopeshaji mkubwa wa hela ya riba hata kama ni bilion tano unapata. Vile vile alikuwa na mashamba makubwa ya ngano kule west kilmanjaro ambako ndiko alitokea kabla hajapata ajali.

Mkuu hapo kwenye RED nadhani ni Cuthbert Swai...
 
Kiongozi! Hivi huyu Bob Sambeke anamiliki nini hapa A town? Ama pale Moshi Mjini?
Ama ni ile ndege moja mbili aliyonayo?

Copy kwa

PakaJimmy
Filipo
Arushaone
Preta
Blaki Womani

Hebu mwenye kujua miradi ya huyu marehemu bilionea anayetajwa hapa kwamba ni BILIONEA.
Mi najua gari mbili aina ya landcruiser pickup anayomiliki na nyumbani kwake pale njiro!

issue ya kuwa bilionea ni nyingine. ila jamaa ana hela na assets za kutosha. Ana land cruiser nyingi na nyumba nyingi. Pia anakopesha hela instantly ukikamilisha vigezo. Ukizingua kwenye kulipa, ndo utamjua Babu Sambeke ni nani. Ananunua na kuuza Nyumba na Magari. Anauza baada ya kufanyia ukarabati mkubwa. Ni mtemi na ana connection kubwa na wakuu wa Polisi na viongozi wa Juu. Thats all i know about him
 
Last edited by a moderator:
Ni kulindana mkuu kwani hata ccm wenyewe ni wateja wake

Lakini viongozi wote wa JMT na chama, walikuwa wakimzika Bi Kidude kule Zanzibar ! Vipi kwa Bilionea, Mkuu wa Mkoa alikuwepo ?
 
Tumeambiwa tukishamaliza kuswali .... Basi tutawanyike katika ardhi kutafuta riziki !

'Itakapo kwisha sala, tawanyikeni katika nchi mtafute fadhila za Mwenyezi Mungu, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi ili mpate kufanikiwa'
Qur'an: Al Jumaa: 62: 10.

Hii ni pamoja na kutoa sadaka na kuinua uchumi kwa kujenga pia mashule na hospitali?
 
sasas mtu anayeweza kopesha bil 5 utamwitaje kama sio bilionea benk zenyewe hupati hicho kiasi huyu ni bilionea kabisaaaa
Ujinga huu, unaijuwa Billion 5 wewe? bond ni nini mpaka upewe na mtu personal pesa hiyo?

arusha na ms kuna matajiri wakubwa sana kuliko sehehu yyte tanzania na hawajiringishi ndugu yangu watu ndio huropoka kuhusu utajiri wao ila trust me kil and arusha ni miji tofauti sana tz.
Hata watu wa Morogoro wanaamini Tanzania hii hakuna Tajili zaidi ya Abood na Shabiby.

hapo umemwona mawalla ???lakini si umeona utajiri wake ??????kimya kimya mkuu
Uhalifu wowote ni lazima ufanywe kimyakimya. Billionea wa kweli asiyetutia Shaka ni Reginald Mengi biashara zake ziko wazi na nadhani hata kwenye soko la Hisa IPP Media itakuwa imeshaingia.
 
Ni heri ya mshamba anayejijua mshamba kuliko mshamba anayejidai mjanja!!!...yaani kifo cha sambeke kimethibitisha kama arusha ndo mkoa unaoongoza kuwa na washamba wanaojidai wajanja!
 
Alazwe pema peponi.kamanda babu.daima marehemu sifa zake nzuri.Mbona matajiri wengi Africa ni wezi bt style za wizi zinatofautiana.
 
Tatizo la watu wengi wamezoea pesa za mwisho wa mwenzi! Bila kalenda kusonga hawana fujo mtaani! Ubilionea unaoongelewa hapa ni wa tshs. Nashangaa mtu anapofanya comparison ya mabilionea wa forbes wanaokuwa rated kwa Usd.

kama ubilionea ni kuwa na zaid ya tshs.bilioni moja hlo halina shaka kuwa Bob alikuwa bilionea! Ni jambo la kawaiada kwa hao mazimba kutembea na cash ya 300 had 700 millions kwa transaction za dharura..sasa hapo akaunti itakuwa inasoma sh.ngap?
Ukiweka nyumba,viwanja na magar plus ndege na hela alizokopesha watu ni chapaa ndefu sana.

na hata haomabilionea wa forbes wanaoshika chat kuna watu wako na hela kuliko wao ila inakuwa ngumu kuwaweka kutokana na bussiness zao haziko open.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom