Songea ni moja ya mji ninaohusudu

Songea ni moja ya mji ninaohusudu

feyzal

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2016
Posts
8,903
Reaction score
18,280
Habari wakuu.

Ni miaka 5 sasa imepita tangu mara ya mwisho kuwepo katika mji wa Songea,ukweli ni moja ya miji midogo Tanzania ambao ulinivutia sana na kupenda maisha ya pale. Nimewahi ishi miji kadhaa kwa nyakati tofauti kama Mtwara mjini,Mafinga mjini,Njombe mjini,Mbeya Mjini,Tanga mjini nk. Ila songea ni miongoni mwa mji wa pekee niliopenda sio kwa majengo bali aina ya maisha ya pale.

1. Mji umepoa hakuna vurugu
2. Vyakula bei chee sana tena vingi vya asili
3. Kodi ya pango bei kitonga mno
4. Hali ya hewa sio baridi wala sio joto
5. Kuna mazao mengi ya biashara ukiwa mchakarikaji unapata cha kufanya(nimewahi uza dagaa nyasa).
6. Wenyeji wakarimu na wanapiga kazi sio wavivu kama Tanga,Mtwara.
7. Watu wa Songea wana heshima sana sio mtoto wala mkubwa.
8. Safari yake ina advanture kubwa na inavutia.

Madhaifu
1. Mji bado mdogo hauna maendeleo ya majengo mazuri
2. Sehemu ya starehe chache
3. Mzunguko wa hela kwa mjini mdogo ila ukiwa unasafirisha bidhaa utapata pesa.
4. Kuna vumbi sana
5. Nyumba nyingi ni chakavu sana

Waliokuwa Songea wekeni comment hapo je kwasasa mji upo vipi?
 
Habari wakuu.

Ni miaka 5 sasa imepita tangu mara ya mwisho kuwepo katika mji wa Songea,ukweli ni moja ya miji midogo Tanzania ambao ulinivutia sana na kupenda maisha ya pale. Nimewahi ishi miji kadhaa kwa nyakati tofauti kama Mtwara mjini,Mafinga mjini,Njombe mjini,Mbeya Mjini,Tanga mjini nk. Ila songea ni miongoni mwa mji wa pekee niliopenda sio kwa majengo bali aina ya maisha ya pale.

1. Mji umepoa hakuna vurugu
2. Vyakula bei chee sana tena vingi vya asili
3. Kodi ya pango bei kitonga mno
4. Hali ya hewa sio baridi wala sio joto
5. Kuna mazao mengi ya biashara ukiwa mchakarikaji unapata cha kufanya(nimewahi uza dagaa nyasa).
6. Wenyeji wakarimu na wanapiga kazi sio wavivu kama Tanga,Mtwara.
7. Watu wa Songea wana heshima sana sio mtoto wala mkubwa.
8. Safari yake ina advanture kubwa na inavutia.

Madhaifu
1. Mji bado mdogo hauna maendeleo ya majengo mazuri
2. Sehemu ya starehe chache
3. Mzunguko wa hela kwa mjini mdogo ila ukiwa unasafirisha bidhaa utapata pesa.
4. Kuna vumbi sana
5. Nyumba nyingi ni chakavu sana

Waliokuwa Songea wekeni comment hapo je kwasasa mji upo vipi?
Ruvuma inaenda kufunguka miaka 10 ijayo.

Kuna BOOST kubwa huko kusini la GAS, URANIUM, na MIGODI.

Wachina wamejaa huko.
 
Back
Top Bottom