Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,923
- 6,570
Kilichopaswa kuwa siku ya mwisho ya kumuaga dereva bodaboda Emmanuel Mwanry kiligeuka kuwa tukio la taharuki na sintofahamu katika Kijiji cha Ngirinyi, Kata ya Levishi, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro.
Mamia ya waombolezaji waliokuwa wamekusanyika tangu mchana kwa ajili ya mazishi ya marehemu walijikuta wakisubiri kwa saa nyingi huku shughuli nzima ikikwama kutokana na msimamo mkali wa kundi la vijana waliokuwa wakishinikiza kuachiwa kwa wenzao 10 wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi.
Kadiri muda ulivyokuwa ukisonga, hali ya huzuni ilianza kuchanganyika na hasira.
Vijana hao walichukua hatua isiyo ya kawaida kwa kulichukua jeneza lenye mwili wa marehemu na kuliweka juu ya gari la Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dk. Christopher Timbuka, kama ishara ya kupinga kile walichodai ni kutotendewa haki.
Tukio hilo lilisababisha taharuki miongoni mwa waombolezaji na wananchi waliokuwa eneo la mazishi, huku shughuli zote za maziko zikisimama kusubiri suluhu ya mgogoro huo.
Baadhi ya waombolezaji, waliokuwa wamekaa eneo hilo kwa zaidi ya saa sita wakisubiri mazishi kuendelea, walianza kutawanyika baada ya kutokuwepo kwa mwafaka kuhusu hatima ya mazishi hayo.
Mmoja wa vijana hao, Nickson Nkya, alisema hawakuwa tayari kuruhusu maziko yaendelee hadi wenzao waliokamatwa waachiwe huru.
“Hatuwezi kumzika mwenzetu mpaka wenzetu waliokamatwa waachiwe.
Pia tunataka pikipiki ya marehemu irejeshwe, tunaamini haki bado haijatendeka na hatuwezi kukubali kuendelea kuonewa,” amesema Nkya.
Msimamo huo uliendelea kushikiliwa na vijana hao huku familia ya marehemu, viongozi wa eneo hilo na waombolezaji wakisubiri kuona kama kungepatikana suluhisho ambalo lingewezesha mazishi kuendelea.
Hadi wakati wa tukio hilo, mazingira yalibaki ya sintofahamu, huku mwili wa marehemu ukiwa bado haujazikwa na jamii ikisubiri hatua zitakazochukuliwa ili kumaliza mvutano huo na kumpumzisha marehemu katika safari yake ya mwisho
Mamia ya waombolezaji waliokuwa wamekusanyika tangu mchana kwa ajili ya mazishi ya marehemu walijikuta wakisubiri kwa saa nyingi huku shughuli nzima ikikwama kutokana na msimamo mkali wa kundi la vijana waliokuwa wakishinikiza kuachiwa kwa wenzao 10 wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi.
Kadiri muda ulivyokuwa ukisonga, hali ya huzuni ilianza kuchanganyika na hasira.
Vijana hao walichukua hatua isiyo ya kawaida kwa kulichukua jeneza lenye mwili wa marehemu na kuliweka juu ya gari la Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dk. Christopher Timbuka, kama ishara ya kupinga kile walichodai ni kutotendewa haki.
Tukio hilo lilisababisha taharuki miongoni mwa waombolezaji na wananchi waliokuwa eneo la mazishi, huku shughuli zote za maziko zikisimama kusubiri suluhu ya mgogoro huo.
Baadhi ya waombolezaji, waliokuwa wamekaa eneo hilo kwa zaidi ya saa sita wakisubiri mazishi kuendelea, walianza kutawanyika baada ya kutokuwepo kwa mwafaka kuhusu hatima ya mazishi hayo.
Mmoja wa vijana hao, Nickson Nkya, alisema hawakuwa tayari kuruhusu maziko yaendelee hadi wenzao waliokamatwa waachiwe huru.
“Hatuwezi kumzika mwenzetu mpaka wenzetu waliokamatwa waachiwe.
Pia tunataka pikipiki ya marehemu irejeshwe, tunaamini haki bado haijatendeka na hatuwezi kukubali kuendelea kuonewa,” amesema Nkya.
Msimamo huo uliendelea kushikiliwa na vijana hao huku familia ya marehemu, viongozi wa eneo hilo na waombolezaji wakisubiri kuona kama kungepatikana suluhisho ambalo lingewezesha mazishi kuendelea.
Hadi wakati wa tukio hilo, mazingira yalibaki ya sintofahamu, huku mwili wa marehemu ukiwa bado haujazikwa na jamii ikisubiri hatua zitakazochukuliwa ili kumaliza mvutano huo na kumpumzisha marehemu katika safari yake ya mwisho