Mawifi jamani, hivi wana nini?

Mawifi jamani, hivi wana nini?

Binamu taratibu! Utaniharibia mingo.

Mpwa nimeikumbuka hiyo offer nikaona SI VIBAYA kwenda kufaidi kidogo! ngoja tumsikie

wewe unazungumzia wachaga wa miaka ipi....1905?...

Mrs, sijui huyo anawazungumzia wa wapi, anyway steriotype dhidi ya hawa watani zangu hazijaanza leo wala hazitaisha. Hivi huko kwao ukiwa MVIVU ndo utaonekana wa maana? KAZI ni kipimo cha utu! Hii nchi ingekabidhiwa wachagga kwa miaka 10 tu halafu tuone,, ebo!
 
Inategemea na mawifi wenyewe, umri wao na tabia zao. Mimi nina dada wawili, mmoja early 50's na mwingine late 40's, nawaheshimu sana. Nitashangaa sana kama nitapata mke atakayeona ni kero kuwaamkia kama ninavyowaamkia mimi. Nafikiri kikubwa ni uhusiano kati yako na mumeo zaidi kuliko uhusiano wako na hao mawifi. Lakini nafikiri pia ukijihusiaha katika kuwakorofisha watu ambao mumeo anawaheshimu, utaweka uhusiano na mumeo katika njia panda.
 
Mpwa nimeikumbuka hiyo offer nikaona SI VIBAYA kwenda kufaidi kidogo! ngoja tumsikie



Mrs, sijui huyo anawazungumzia wa wapi, anyway steriotype dhidi ya hawa watani zangu hazijaanza leo wala hazitaisha. Hivi huko kwao ukiwa MVIVU ndo utaonekana wa maana? KAZI ni kipimo cha utu! Hii nchi ingekabidhiwa wachagga kwa miaka 10 tu halafu tuone,, ebo!


sema na wewe mr wangu, NA ACYE FANYAKAZI NA ACLE.... amezoea hao wa huko kazi yao kukaa vibarazan na vikanga kifuani anamsubiria baba nanilii aje na pweza jioni.....
 
sema na wewe mr wangu, NA ACYE FANYAKAZI NA ACLE.... amezoea hao wa huko kazi yao kukaa vibarazan na vikanga kifuani anamsubiria baba nanilii aje na pweza jioni.....


Na akirudi mikono mitupu, utasikia 'leo maji yalijaa, tusubiri maji mafu'....
 
Hata kama wewe wifi yao kimeo wabaki kimyaa unamwangamiza kaka yao vp bana? Damu nzito kuliko maji ukiwa kimeo utanyooshewa kidole na mawifi mpaka utakapo jirekebisha ebo.

Taratibu hommy!

Wewe si unasema hivyo kutokana na ukimeo wako na umedata sana wewe. Huthamini na hujali ndugu zako wewe wifi akiwa anamchuna kaka ako lazima ukomae sio eti kaolewa tu jamaa nyumba anaenda kujenga ukweni wapi na wapi bana.

Kaka unaua sasa!

Yeah lazima wamsaidie ndugu yao bana sio kesho na kesho kutwa ana fulia janamke linakimbia na kufuata mme mwenye pesa si akili zenu mnazijua wenyewe mawazo kwenye mkwanja tu na si tru love.

Homeboy menichekesha sana mkuu.....naona hutotugoti na kule home huwa wanatumind sana!

siku hizi sio watu wa kanda ya ziwa tu, hata kanda ya kaskazini mawifi wana kiherehere sana, wanajidai kuwaonyesha kaka zao njia, unamuignore mpaka anondoka bila kuaga, ukiona anakusumbua sana unamwambia za saa hizi, unapanga safari unaondoka asubiri kaka yake aje amsalimie kwa unyenyekevu,

Pretty, please usichukue huo ushauri hapo juu....utakuponza,ukipishana na wifi or anybody tafuta suruhu sio visa......ndoa yako haitodumu.......! Fuata ushauri wa Nyamayao, Fixed point at least wanauzoefu mzuri wa kusolve problems za aina hiyo....!

wifi/mama mkwe sio watu wa kuwazembe kuanzia mwanzo, utakavyowarembea ndivyo watakavyo kuburuza, mbele ya mama mkwe na mwanae yaan mr cku moja nilimtolea uvivu wifi hatokaa arudie maisha yake yote na heshima za kumwaga mpaka sasa.......ukiteleza tu utamwona mpaka mumeo mtarajiwa mchungu tena ukute ndio wae wakaka wa kuckiliza ndugu zao kuliko wewe oohh utakwisha....uczubae.

Yes, mwanamke lazima uhakikishe unaitetea ndoa yako, lkn si kwa kuwanunia mawifi, ma/mkwe etc tell them wapi wanaenda wrong, kama wanabusara watakusikiliza tu......! Always tumia busara zaidi, kuliko nguvu na jeuri kukabili matatizo yako, mumeo atakuheshimu sana!

jamani wadada na JF tukubali kuwa sometimes sisi waolewaji ndo huwa tunakuwa na matatizo, mambo ya kwenda umejiandaa kuidhibiti familia ya mume. unajua sio familia zote ambazo ni ngumu kuishi nazo ila kwa vile tunatoka kwetu tukiwa tumejiandaa jinzi ya kuwadibiti mama mkwe na mawifi ndo inakuwa balaa. wakati mwingine wifi au mama mkwe anaweza akakosea kitu kidogo, kibinadamu, ambapo hata mama au mdogo wako anaweza akafanya kitu kama hicho lakini sababu kafanya wifi/mama mkwe inakuwa balaa.
tujitahidi na sisi kuchukulia familia za waume zetu kama familia zetu, labda haya mzogo yatapungua

Natamani wanawake wote wangekuwa na ufahamu huu......! Many thanks FP!
 
Habari zenu wanaJF,
Hivi mawifi wana nini lakini? Natarajia kujitosa kwenye ndoa, lakini wifi ananiletea vituko mapema kabla ya kufika huko. Mama mkwe wangu ananipenda lakini wifi yangu maneno maneno. Ana kazi na familia yake lakini bado tuu ananisema, eti anataka nimpigie magoti ninapomsalimia, anawaambia watu kaka yake anaoa binti wa mjini hawana heshima.
Hivi unapomsalimia mtu ukimpigia goti ndio heshima?Wadada mliolewa hebu nipeni mbinu za kumdhibiti huyu wifi.

Najihisi mwenye bahati mbya.......
 
Karibu sana wifi yangu kwetu goti ni lazima ndiyo culture yetu,umependa boga penda na maua yake

Nimeshakaribia wifi na ahsante. Mtu ukiwa na ndoo ya maji kichwani sharti upige goti ukimsalimia mtu, hii kweli haki?Wifi hizi mila nyingine mhhhhhhhhhhhhhh!!
 
Pretty pole shoga! kwani huyo wifi yako ni mkubwa kwa mumeo mtarajiwa ama ni mdogo?
2. Huyo wifiyo anakaa na huyo mumeo mtarajiwa ama mtakapo owana mtakaa nae nyumba moja?

-Nina wifi 2 shost, mmoja mkubwa na mwingine mdogo.
-Wifi ana familia yake/mji wake.
 
Nimeshakaribia wifi na ahsante. Mtu ukiwa na ndoo ya maji kichwani sharti upige goti ukimsalimia mtu, hii kweli haki?Wifi hizi mila nyingine mhhhhhhhhhhhhhh!!
Hiyo ya ndoo kichwani du hapana.Ila ukiwa unamsalimia mtu aliekuzidi umri unapiga goti sana sana mama mkwe,baba mkwe ila kusema ukweli hizi mila za kisukuma hata mimi sizipendi nakumbuka eti mtu unampa maji ya kunywa yaani unapiga goti hadi amalize kunywa.
Thank God sijaolewa usukumani
 
Hiyo ya ndoo kichwani du hapana.Ila ukiwa unamsalimia mtu aliekuzidi umri unapiga goti sana sana mama mkwe,baba mkwe ila kusema ukweli hizi mila za kisukuma hata mimi sizipendi nakumbuka eti mtu unampa maji ya kunywa yaani unapiga goti hadi amalize kunywa.
Thank God sijaolewa usukumani

Wasukuma wa wapi hao wenye mila hizo?
 
Hiyo ya ndoo kichwani du hapana.Ila ukiwa unamsalimia mtu aliekuzidi umri unapiga goti sana sana mama mkwe,baba mkwe ila kusema ukweli hizi mila za kisukuma hata mimi sizipendi nakumbuka eti mtu unampa maji ya kunywa yaani unapiga goti hadi amalize kunywa.
Thank God sijaolewa usukumani

Nashukuru kaka yako muelewa, yeye mambo ya kupiga magoti wala hapendi. Hao wengine nitaweka kichwa ngumu tu.
 
Ndio, magoti ni heshima. Kama umempenda mume wako mtarajiwa basi upende na mila na desturi zao. Kwani ugumu upo wapi? Kwani unaweza kuamka asubuhi bila kumwamkia mzazi wako? of coz kwa mila za kiafrika ndivyo ilivyo tunawasalimu wazazi, walimu na wakubwa zetu. Basi usisite fanya utazoea.Usione kama anakuwa mbaya ni mila na desturi za kwao.
 
Nashukuru kaka yako muelewa, yeye mambo ya kupiga magoti wala hapendi. Hao wengine nitaweka kichwa ngumu tu.

Pretty mpendwa nilitaka nifunge domo langu kwenye mada hii ila niliposoma hii nimeona bora nikueleze niliyofundishwa na mama yangu.

Kitu cha kwanza kabisa unatakiwa ujue msimamo wa mumeo (wa kiukweli sio wa mdomoni), je ni wale wanaosikiliza ndugu au ana msimamo wake? unaweza kujifanya kichwa ngumu mwenzio akakubadilikia ukashangaa.

Waheshimu ndugu zake wote hata watoto kwani ameishi nao kipindi kirefu kuliko alivyoishi na wewe, so wewe huwezi ukaja from nowhere ukaanza kumuonyesha ubaya wa ndugu zake. Hata kama ni wabaya mwache aseme mwenyewe na hata akisema nyamaza kimya kwani anaweza kuwa anakupima vilevile.

Hakuna binadamu asiye na maudhi, uvumilivu ni kitu cha muhimu sana, usiwape tu nafasi ya kukuudhi sana.

Hewala si utumwa, kwani ukipiga goti akafurahi wewe inakupunguzia nini? Unapaswa kukataa vitu tu ambavyo vinakudharaulisha. Sio vizuri kufanya vitu vinavyokufanya uonekane tofauti sana nao. Angalau wakuone kama mwenzao hata kwa asilimia fulani.

Ongea inapobidi, mama mkwe na wifi sio mashoga zako. Ongea kidogo sana sikiliza sana, wakisema mtu usitie neno. Sijui kama unajua kitu kinaitwa kucheka kichina, huku ni kusmile kumridhisha mtu. Mara nyingi wakiongea we cheka kichina, usi-support sana maongezi smile tu waone kama uko nao. Ishi maisha yako usitake sana ukaribu wa kuzidi, ni kusalimiana na kusaidiana.

Muhimu waheshimu, sio kuwa wewe ni mke basi wewe ni bora hapana. Mama ana nafasi yake kama mama na ndugu wana nafasi zao kama ndugu wewe huwezi kuzireplace na kila moja ina umuhimu wake. Muhimu usiwaruhusu tu kukuingilia katika mambo yako ya ndani ya ndoa, na usiwaambie kwa hasira ikitokea wakifanya hivyo, waambie tu kwa utaratibu na kwa heshima

Niamini watakuheshimu
 
Ndio, magoti ni heshima. Kama umempenda mume wako mtarajiwa basi upende na mila na desturi zao. Kwani ugumu upo wapi? Kwani unaweza kuamka asubuhi bila kumwamkia mzazi wako? of coz kwa mila za kiafrika ndivyo ilivyo tunawasalimu wazazi, walimu na wakubwa zetu. Basi usisite fanya utazoea.Usione kama anakuwa mbaya ni mila na desturi za kwao.

Kusalimia mzazi au mtu mkubwa yeyote aliyonizidi umri ni wajibu, lakini kupiga magoti sio kigezo cha heshima.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom