Triplets
JF-Expert Member
- Sep 27, 2007
- 1,146
- 206
jamani wadada na JF tukubali kuwa sometimes sisi waolewaji ndo huwa tunakuwa na matatizo, mambo ya kwenda umejiandaa kuidhibiti familia ya mume. unajua sio familia zote ambazo ni ngumu kuishi nazo ila kwa vile tunatoka kwetu tukiwa tumejiandaa jinzi ya kuwadibiti mama mkwe na mawifi ndo inakuwa balaa. wakati mwingine wifi au mama mkwe anaweza akakosea kitu kidogo, kibinadamu, ambapo hata mama au mdogo wako anaweza akafanya kitu kama hicho lakini sababu kafanya wifi/mama mkwe inakuwa balaa.
tujitahidi na sisi kuchukulia familia za waume zetu kama familia zetu, labda haya mzogo yatapungua
hii point mwanakwetu, sasa unakuta dada zako na mama yako mzazi wakija kwako heshima mkononi na wewe unawaheshimu lakini wakija mawifi ni kunyanya paa tu kwa kwenda mbele, mara akuamrishe mara akufokee, ukifanya kizuri akutoe kasoro...kuna wengine aah hawana shida na mtu kwa kwelli hao hata kuwachukulia kama dada inakuwa rahisi lakini kuna wengine balaa kweli kweli
mimi nakumbuka kuna shangazi yangu alikuwa kila akija nyumbani lazima aondoke na kitu, mama analalama weee lakini kumwambia hathubutu eti kwa vile ni wifi yake..