Matokeo ya Uchaguzi mdogo Igunga (matokeo ya awali)

Matokeo ya Uchaguzi mdogo Igunga (matokeo ya awali)

Status
Not open for further replies.
Na wao ITV wana viherehere.wanavyoshupalia matokeo ya igunga kana kwamba ni uchaguzi wa nchi nzima.yaani si jambo zuri hata kidogo.ni sawa na kuchochea mapinduzi.ni ushabiki wa kijinga kabisa.mbona MV ISLANDER ilipozama hawakuwa na vihelehele namna hii.shikeni jembe mkalime toka kwenye TV .CCM hata kwa kuchakachua LAZIMA ishinde.
 
wazee...........mbona kama ccm wanaongoza??
au bado hamuamini??.....maana gap la vi jijini kama kubwa vile??!!
 
Jamani mshindi wa Bongo Star Search nani? Mwenye link tafadhari, nijipoze na BSS. Bela kawa wangapi?
 
Magamba kwisha!!! Madereva wa CDM waliopo Igunga wamepewa hali ya standby -- watafute mafuta wajaze ili magari yaingie mitaani kusherehekea. Hii si utani, imetoka katika vikao vya juu vya CDM ambao wamekuwa kimya muda mrefu wakijumlisha data za kutoka kwa mawakala wa chama walio vituoni.

Peoplesssssssssss!!!
 
Hawa jamaa wa Star Tv naona nao wanapita JF wamemtaja Mwanangwa! kwa ile post yake ya Derby mbili!
 
unauliza au unataarifu kile unachofahamu<? mbona hueleweki! sisi kwetu "UNgeleja" umekatika toka saa kumi na mbili tupo gizani hatuponi TV.
 
hakuna matokeo ya uhakika,matokea mpaka sasa ni yale ya kata 4 zilizotangazwa na radio one,na ambazo wamedai ccm zote wanaongoza hizo kata 4 bado kata 22,radio one hawajatangaza kitu toka saa moja na dk 50 mpaka sasa.

Hahaha, Igunga mjini kwa macho yako na source yako mwenyeweeee, CCM kata 4 CDM kata 1, unajua matokeo ya vijijini?
 
wenye watoto wanaofanya mtihani wa form four na wanasoma Igunga
jamani waambieni ccm wasichakachue maana watoto wenu watafeli
kwa minyukano ya kutafuta haki huko.
 
Habari za Makumbusho mkuu; safari hii hakuna mikono yenu tena kwenye uchaguzi?????????????

kwa mujibu wa updates nilizonazo ni kwamba uchakachuaji kwenye uchaguzi wa jimbo la igunga ni mdogo sana hivyo matokeo yatakayokuja tuyaheshimu.wand wa igunga wameamua hivyo!tuwe na subira na tuheshimu matokeo,tusonge mbele huku tukiamini change is coming!
source:secret service
 
Tatizo la chadema ndio hilo..kila siku mnasingizia kuibiwa! Kuweni na demokrasia ya kweli..kubalini kushindwa.
Jipangeni kisera na kichama pia. Bado mpo nyuma sana. Mmahitaji kama 4O yrz muwe kwenye level ya CCM

mzee wa arseno pole
 
tatizo la wadau wengi humu ni chadema ambao hawataki kuandalia hali halisi, ukweli chadema wameshinda vituo vingi, ila vinawapiga kura wachache, ikaokea kata zile zenye wapiga kura maelfu, chadema wameshindwa kwa tofauti ya kura zaidi ya mia 5 kwa kata moja, mdau wa kwanza ukijumlisha utapata CHADEMA kura 4692, CCM kura 5975 tofauti ya 1283, tayari kuna mijitu humu yameshaanza kusema CCM wanaiba. tukubaliane na hali halisi hakuna cha wizi wala nini. kama DP wameshinda wapewe haki yao
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom