Vyama vingi vinavyokuwa mpinzani wa utawa kihistoria vinatokana na tabaka la wafanyakazi. Pamoja na kwamba tabaka la chini walio wengi ndio wanaoishi vijijini, lakani wenye uelewa mkubwa juu ya haki zao ni wale wanaoishi mijini kuliko vijijini. Hali hiyo si kwa Tanzania, na Afrika tu, ila ni kwa dunia yote.
Uchaguzi wa Marekani ambao Obama alishinda, ukiangalia kwa ukubwa wa eneo alishinda eneo dogo sana la state kubwa ambazo zina mfumo wa maisha ya kimjini kuliko state ambazo ni za wakulima ambazo zina wapiga kura wachache. State kama za Califonia, NJ, Pennslivania, New York, Virginia ambazo population ya watu ni mfumo wa maisha ya mijini zaidi kuliko shamba. State nyingine zilizobaki ndizo zenye mfumo wa watu wanaoishi maisha ya shamba na ndiko wakaoshinda Republican.
Mfumo wa ugawanyaji wa majimbo ya uchaguzi Tanzania hauwiani na idadi ya watu, ila wanaangalia ukubwa wa eneo. Eneo kubwa utakuta linagawanywa majimbo kadhaa ya uchaguzi bila kuangalia uwiano wa idadi ya watu. Hilo nalo ni tatizo ambalo siku za usoni linatakiwa kufanyiwa kazi.
Chadema inaendelea na tatizo lile lile la kuwa na mvuto mkubwa wa watu ambao si wapiga kura kwa hoja ya kutojiandikisha kupiga kura ila kushabikia tu. Hilo ndilo tatizo kubwa ambalo linaiangusha Chadema. CCM inatumia mwanya huo kwa kuimarisha nguvu ya wapiga kura kwa kuanzia shina kuwatumia viongozi wa mashina ufuatiliaji wa wapiga kura, na hivyo kuwa na hakika ya ushindi kutokana na wanachama wao kuipigia kura CCM, ndio maana unaona hata wakuu wa wilaya wako makini kutembelea vijijini na kufanya mikutano ya siri kwa ajili ya kupima upepo na kuhamasisha wapiga kura mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba.
Katika hili la Igunga hakuna uchakachuaji wa wazi, na inaweza ikawa ni hali ya kufikiriaka zaidi kuhusu uchakachuaji kuliko kuangalia hali halisi ya mfumo wa CCM kuthibiti wapigakura wake na Chadema kudanganywa na umati wa vijana wasiojiandikisha kupiga kura, hili ndilo tatizo la dhahiri.
Tatizo hili lilitokea tangu uchaguzi mkuu uliopita na hata enzi zile za mzee wa Kiraracha, badala ya kuhamasisha watu mitaani kujiandikisha kupiga kura Chadema wanasimama majukwaani kunadi sera, Kwa siasa mbinu za kuwapata wapiga kura ni muhimu zaidi.