Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Recently kabla ya kupata ajali. Alikuwa anakopesha watu pesa, lakini collateral ilikuwa tittle ya kiwanja ama nyumba. Kwa taarifa ni kwamba wengi sana walishindwa kulipa. Na kwahiyo wakapoteza nyumba zao na viwanja vyao. Sometimes magari. Ni ukweli mtupu kuwa kuna watu wanaomchukia sana Babu Sambeke.
Yale yale ya Alex Massawe na nyoka wake wakina Papaa Musofe.
 
Wazee wa Moshi mnajikumbusha. Yule Alfred Masawe alikuwa wa wapi aliwahi kufungu Hotel moja Dar inaitwa AM Hotel niliwahi kulala siku moja, mapokezi kuna tangazo kubwa pale "Management haitahusika na upotevu wa mali ya mteja, tafadhali kabidhisha mali yako Mapokezi" Ukiweka mzigo tu usiku wanaume hao wanakuja kuuchukua na wanafanya kumkwangua receptionist kidogo, wazambia na Wacongo walilizwa sana pale, kumbe ni mwenye ndio alikuwa anapiga.
😂😂😂 Alex Massawe nasikia yupo bondeni kwa madiba. Yule jamaa alikua mafia sana
 
Huyo mzee alisha fariki kitambo, labla anae ongelewa hapa ni mwingine..
I know, nilimquote mtu aliyesema "alikuwa akimsaidia kuchambuwa madini" na kucheza na watoto wake sebuleni. Ndipo nikamuuliza kama alikuwa anamzungumzia Njiwa Hardware. Sikufahamu kama alijihusisha na biashara ya mawe baada ya kuanzisha zile hardwares zake.
 
Yesu alipolinganisha ufalme wa mbingu na tundu la sindano hamkumwelewa? Siyo matajiri wa Moshi tuu. Hata matajiri wengi wakubwa Duniani nao wamezulumu Sana tuu.
 
Late babu sambeke ni mmoja wa watu wa awali kabisa kumiliki pikipiki za mwendokasi moshi mjini!
Ndiye aliyekuwa mmowapo kama siyo mtu wa kwanza kabisa kuwa anaendesha pikipiki hiyo kwa tairi moja (Kunyanyua).

Alikuwa akijiskia tu, anakuja anatoa shoo ya ukweli kwenye huo mtaa. Pia alikuwa na boti yake alikuwa ameiandika na kuiita "Queen Duluthi", kila wakati utamuona ameifunga kwenye cruiser yake anaelekea kwenye ziwa Duluth kula bata nk. Enzi hizo pia kulikuwepo na party pale ziwa Duluth kila mwaka kama sikosei. Kiukweli yule jamaa hakuwa na hata chembe moja ya uoga kwenye damu yake. Mpambanaji wa ukweli na mchagga halisi!
 
Mkuu kuna lile ghorofa pale Rau upande wa kushoto mbele ya Chuo Kikuu cha Ushirika ukitokea YMCA ambalo hakuna kiumbe anaeweza kuishi pale,hivi status yake mpaka sasa lipoje maana kuna kipindi nilisikia Mama Anna Mkapa alitaka kulinunua. Hilo ghorofa lilikuwa la Mkibosho fulani hivi.
Labda ya yule mzee Mwacha? Yule mzee aliyekuwa na watoto wake kina Ben Mwacha the late.
 
Back
Top Bottom