Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Miaka hiyo kulikuwa na watu wanaojua kutake risk kwelikweli....get rich or die trying. Huwa siwalaumu watu wa aina hii. Dunia nzima wapo. By the way katika generation ninayoiheshimu ni generation ya 60s na 70s hao ndio walikuwa WANAUME. Ni kama unavyosoma stories za kina Godfather n.k. Kizazi chetu lonyalonya hatuwezi hata kujaribu michongo migumu, waoooga kama kuku.

In every fortune there is crime.
 
Sawaya alishafungwa miaka 7 kwa wizi wa matairi kwenye godown miaka ile
True, ila sasa hivi yuko vizuri sana. Pia ana mashine yake ya kutengeneza kokoto somewhere kuelekea Dar maeneo ya kati, sina uhakika kama ni upareni ama Tanga. Ila anawasupply hao watu wa constructions na hizo materials. Fursa ni nyingi sema uongozi mbovu.
 
Haruni masubaru,
Alikula kuberi mpaka akakonda
Wanawe nao akili kama za baba yako
Gereji bado ipo
Duuh!Haruni! Alikuwa lambalamba sana jamaa. Yeye ulevi wake mkubwa Zaidi ya hiyo kuberi ni mademu. Alikuwa hakosi Safary Rally, enzi hizo mara zote akipata nafasi ya kwanza na gari yake ikiwa namba 1. Kuna wakati pia Babu Sambeke aliingia na yule chotara walikuwa wakimuita John Jeep. Waliikuwa namba 4. Walipata ajali mbaya sana. Ndipo chanzo cha sura ya babu Sambeke kuwa na makovu. John Jeep yeye alitenguka kiuno. Ila wote pia walikuwa wanapita na mademu kwa kasi ya ajabu. Walikuwa players mbaya.
 
Sawaya.
Huyu nae alkuwa na garage.
Nafikiri kuna kipindi ilikuwa kwenye frem za uwanja wa majengo (huenda lilikuwa ni duka la spares. Sikumbuki vzur)
Alikua na gereji kule mbuyuni aka bomambunzi
Zaman ilikua pale majengo juu
Alianza kuuza saruji,akanunua mitsubishi rosa basi ikiitwa Neema,then nissan ud concord kama Sawaya,akatoa bus za hyundai zikachemsha mbio za dar wakati ngorika,mkwema,shabaha,na dar express wana scania 92 2-series
Akarudi scania kama wenzio na 93 gear 10 ligi ikanoga wakat huu ana lorry mende anapiga huo mpaka wa kenya kama sebuleni kwake

Yaliyofuata ndio tunayaona sasa!
 
Miaka hiyo kulikuwa na watu wanaojua kutake risk kwelikweli....get rich or die trying. Huwa siwalaumu watu wa aina hii. Dunia nzima wapo. By the way katika generation ninayoiheshimu ni generation ya 60s na 70s hao ndio walikuwa WANAUME. Ni kama unavyosoma stories za kina Godfather n.k. Kizazi chetu lonyalonya hatuwezi hata kujaribu michongo migumu, waoooga kama kuku.

In every fortune there is crime.
Maisha yamebadilika sana, na kila zama na wakati wake...

Zamani baadhi ya wafanya biashara walikuwa wana roho ngumu sana, kuna jamaa mmoja ni jirani yangu alikuwa ni mwizi balaa wa magari, alishirikiana na askari wa kenya, huyu jamaa biashara ya wizi kaachana nayo, sasa hvi ana maduka ya kuuza bia za jumla na migahawa..

Nawafahamu vijana wengi sana moshi na arusha wamefungwa magereza ya kenya kwa uwindaji haramu, kuna mtanzania mmoja alidakwa anawinda tembo alinyofolewa kidevu na sime askari wa kenya wanaroho ngumu
 
Sambeke ananikumbusha group yake ya wakina Michael Casmiri Mushi wa Uru Ongoma walivyokuwa wanapiga watu puu mamilioni ya hela miaka ya 80s na 90s pale Kariakoo Mnadani kwa kuuziwa nyumba,viwanja fake na magari kwenye karatasi. Bila kusahau nyoka wake wakina Golo wa KCMC.
Sambeke alikua mafia sana afu gari zake ni Land Cruiser tu hasa VX
 
Huyu mama yuko vizuri sana. Kweli penye nia pana njia. Na ukifanya kazi kwa bidii utafanikiwa tu. Almuradi uwe na malengo. Malengo ni namba moja! Wengi tu waliotajwa humu wamepambana sana tu pamoja na kwamba watu wengine wansema kuna waliopata kwa njia za kishirikina. Wengi tu ni mifano hai ya kupambana. Na kama siyo utaratibu wa kawaida wa serikali kuanzia mwalimu Nyerere wa kuwashikia chini wachagga, ingekuwa habari nyingine. Ni kweli walibinywa sana na serikali na ni kweli wengi walitajirika sana especially kipindi cha Mwinyi kwa biashara za magendo toka Kenya. Kwasababu ya ujamaa wetu, bidhaa nyigine kama sabuni tu ilikuwa anasa kubwa! Bia je?
Enzi za biashara ya kitobo kila mchaga mjini moshi lazima amiliki Toyota Stout kwa ajili ya kubebea mizigo ya magendo
 
Matajiri wengi wa kichagga siwatilii maanani kwani utajiri wao unapatikana kwa njia za hajabu sana hata nduguze Mshana Jr (wapare) na ni tata mno, bila umwagaji damu na matunguli biashara haifanyiki. Nawapotezea tu.
 
Back
Top Bottom