Maswali yangu kwa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) kuhusu Tamko la Mkataba wa Bandari

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
1. Wanadai Serikali iachane na Mkataba wa Bandari kwa sababu wananchi wamegawanyika kuhusu mkataba huo!

Swali langu kwao, Ni jambo lipi nchi hii limewai kukubaliwa na asilimia 100 ya wananchi wote? Kwenye Mfumo wa vyama vingi, Mbona asilimia kubwa ya Wananchi walikataa mfumo huo ila Serikali wakauunga mkono! Je kwa nini hawakutoa tamko kipindi icho kutaka nchi iendelee kuwa ya Chama kimoja? Kwa tamko lao walilosema maamuzi ya wananchi yaheshimiwe basi wanaunga mkono Serikali i reverse maamuzi yake ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi na turudi kwenye mfumo wa Chama kimoja?

2. Kwenye tamko lao wanadai Mihimili ya dola iheshimiwe. Swali langu kwao! Juzi Mahakama Kuu wametoa maamuzi ya kutupilia mbali maombi ya watu walioshtaki mkataba wa Bandari.

Sasa kwa nini wanataka mihimili ya dola iheshimiwe na wao hawataki kuheshimu maamuzi ya Mahakama? Kama Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 hasa ibara ya 107A inasema Mahakama ndio Mhimili wa mwisho katika kutoa haki sasa kwa nini hawaheshimu maamuzi ya Mahakama alafu wanatoa tamko kusema Mihimili ya dola iheshimiwe?

3. Wao wanavyotoa tamko kutaka Serikali iachane na mkataba wa bandari kesho BAKWATA wakitoa tamko Serikali iendelee na mkataba wa Bandari wanataka Serikali imsikilize nani? Kesho kutwa mabudha wakitoa tamko pia wanataka Serikali imsikilize nani kati yao?

Kwa hali hii sasa nimejua kwa nini mapadre wa kanisa katoliki walishtakiwa kwa kuhamasisha mauaji ya kimbari Rwanda!


Pia soma
- News Alert: - Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC): Hatuungi mkono Mkataba wa Bandari. Sauti ya Watu ni sauti ya Mungu
 
Mkataba wa bandari ni mkataba wa kurudisha utawala wa sultan sio wa kuleta maendeleo

Alichofanya samia ni kusaidia waarabu kuja kutawala TANGANYIKA

Inaonekana samia na waarabu wanamipango mingi iliyojificha ambayo sio mizuri juu ya TANGANYIKA yetu ambayo sisi hatuijui
 
Watu wanaosapoti ule mkataba vilevile ulivyo wanapatikana jamii forums tu na mitandao ambayo watu hawajulikani majina yao halisi. Tangu hili sakata lianze sijawahi kukutana na ndugu, jamaa au rafiki anaye sapoti huu mkataba. Kila sehemu ninapoenda watu wote wanakandia sana. Hata mleta mada vijiweni au maofisini hawezi kuutetea. Ni kichaa peke yake atakubaliana na vile vipengele vinginevyo kama mtu ana maslahi binafsi au kashalamba ela za DP WORLD 🌎.
 
Watu wanaosapoti ule mkataba vilevile ulivyo wanapatikana jamii forums tu na mitandao ambayo watu hawajulikani majina yao halisi. Tangu hili sakata lianze sijawahi kukutana na ndugu, jamaa au rafiki anaye sapoti huu mkataba. Kila sehemu ninapoenda watu wote wanakandia sana. Hata mleta mada vijiweni au maofisini hawezi kuutetea. Ni kichaa peke yake atakubaliana na vile vipengele vinginevyo kama mtu ana maslahi binafsi au kashalamba ela za DP WORLD 🌎.
Hizo takwimu zako ni za wapi? Utafiti uliufanya lini?
 
8d288b62-7346-4610-a9a2-a328517f79cd.jpg
 
Mimi ni mwananchi lakini sijagawanyika labda watupe majina ya watu waliogawanyika,au wao ndiyo wamegawanyika kwa kunyimwa $ ? Watambue kesi zipo nyingi wasione wakina mdude wameachwa wakazani kesi zimeisha tuna kesi za aina nyingi za kuwasotesha rumande
Kuna makosa Serikali ilifanya na haya ndo yanafanya hawa wapuuzi wajione kama sehemu ya uongozi wa hii nchi.

Ni mambo ya ajabu kabisa. Eti wanatoa tamko kutaka serikali iachane na mkataba wa Bandari? Wao kina nani nchi hii? Kesho BAKWATA wakitoa tamko kutaka Serikali iendelee na mkataba??

Wanataka kuifanya hii nchi iingie kwenye matatizo hawa wajinga.
 
Back
Top Bottom