"Mgeni sio kwamba ananunua ardhi, na sio kwamba anapewa umiliki wa 100% hapana anapewa kibali cha kuwekeza kwa miaka kadhaa. Kwa mtu anayetoka Tanzania Bara ambaye anataka kufanya Uwekezaji Zanzibar anatumia utaratibu huo huo" Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Ally Mwinyi.

View attachment 2028001
Kiukweli hata mimi sipendi kabisa kuona Tanganyika inaendelea kuungana na Zanzibar. Binafsi huwa sioni faida zozote za huu muungano na wala sijawahi kuwaona wazanzibari kama raia wenzangu, nawaonaga sana tu na Wakenya, Wanyarwanda au Waganda. Pande zote mbili za muungano zina malalamiko, zinabaguana na hazipendani hivyo nadhani ni wakati muafaka kabisa wa kuvunja huu muungano na kukubali kwamba jaribio la kwanza la Nyerere limefeli kabisa.
 
Jamani Zanzibar ni kama 2460sq km
Bara 947, 303 sq km
Zanzibar × 390 ndio unapata bara.
Zanzibar wakilegeza kwenye umiliki wa ardhi wanaweza kujikuta ni taifa lisilo na ardhi.
Hivi vi kilometer elfu mbili ya Zanzibar vinawezamilikiwa na mtu mmoja..

Mambo mengine tuangalie jameni
 
Bila hicho kipengele cha ardhi leo hii nchi hii ingekuwa moja. Watu wangekuwa wameingiliana hadi ingekuwa hakuna tofauti ya mzanzibari na mtanganyika. Walifanya makosa sana na hicho kipengele. Eti ardhi ndogo? We ukiwa na laki na mwenzako ana milioni moja na akikuambia mchange mtumie pamoja unaanza je kukatalia kuweka laki yako mezani!!!! Ubinafsi wa kijinga.

Muungano uendelee, tunafaida nao.
 
Kwisha habari yenu Ardhi ya ZANZIBAR NI ndogo Sana isipolindwa Kesho na keshokutwa tutakua na uhaba mkubwa WA Ardhi Kwa vizazi vyetu Watanganyika ttzo lenu si Ardhi mnamamia Kwa maelfu ya maekar tatizo lengu ni umaskin WA akili ndio maana mnahama huko kuja kututilia nzi huku
Mbona wazungu wananunua kweli ardhi Zanzibar kwa sasa au kwa sababu wao mabeberu
 
Rais Mwinyi ni Mzanzibar na anamiliki ardhi bara. Watanganyika sijui nani katuloga
Tafuta asili ya Mwinyi mzee upate majibu ni mtu wa wapi upande wa baba yake..
Ile katika ambayo hata yeye aliikuta kule hakuyaanzisha yeye yale
 
Watanzania kwa idadi tunakadiriwa kufikia milioni 65 na ndani yake kuna idadi ya Wazanzibar 1.5 milion. Eneo la Zanzibar, utamaduni na ukale wa Zanzibar,ni sahihi kabisa sababu Tanzania bara tuna maeneo ambayo hayakaliwi mahekta na mahekta na ni mapori matupu nadhani ukiwa unasafiri na unaona how Tanzania bara ni kubwa, pili kwa mkwanja walionao wabara wanaeza nunua ardhi ya Zenji yote na watu wenye historia ya Zanzibar wasiwepo tena,Wazanzibar karibuni bara maeneo ya kumwaga mje mlime na mfuge ni Tanzania yenu.
 
Pumbafu kabisa hiki ki muungano Uchwara Cha mbwa mwitu na kondoo kifutiliwe mbali kabisa,
Chetu Chao, Chao Chao sisi hakituhusu!
Hivi watanganyika tunafeli wapiii?
The late Nyerere alipenda sana kulifafanua hili kwamba nasi tukiamua kuvamia na kuchukua maeneo kama tunavyojikatia huku Bara si tutamaliza ardhi yao na mwishowe kuwameza kabisa?
 
"Mgeni sio kwamba ananunua ardhi, na sio kwamba anapewa umiliki wa 100% hapana anapewa kibali cha kuwekeza kwa miaka kadhaa. Kwa mtu anayetoka Tanzania Bara ambaye anataka kufanya Uwekezaji Zanzibar anatumia utaratibu huo huo" Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Ally Mwinyi.

View attachment 2028001
Mungu ibariki Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
 
Bibi Tozo mwisho wake ni 2025, baada ya hapo akapumzike kwenye nchi yake tu.
 
Kwani huu Muungano tukiurarua ukavunjikilia mbali sisi huku bara tutapoteza nini?
Wenzetu wanafaidi matunda ya pande zote!!
Watanganyika tunawekewa kila aina ya mikingamo upande wa pili.
Ni heri ufilie mbali tujue moja.
Ni ujinga kuwa na Muungano wa kisanii kama huu
 
Muungano wa kipumbavu kabisa. Terms za muungano zifanyiwe reviews, la sivyo tutatumia udhaifu wa muungano huu kwenye harakati za kuasi serikali.
 
Jamani Zanzibar ni kama 2460sq km
Bara 947, 303 sq km
Zanzibar × 390 ndio unapata bara.
Zanzibar wakilegeza kwenye umiliki wa ardhi wanaweza kujikuta ni taifa lisilo na ardhi.
Hivi vi kilometer elfu mbili ya Zanzibar vinawezamilikiwa na mtu mmoja..

Mambo mengine tuangalie jameni

Watakuua humu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom