Hii issue nilitegemea kuiona JF. Mwanzoni nilikuwa siielewi nikajipa muda kuijua na ni kubwa tofauti na nilivyotarajia.
Kwanza Marekani haina active anti aircraft missile systems, huwa inaamini hakuna mtu anaweza fanikiwa kuleta ndege kwenye anga lake. Ila ina layel of ballistic missiles defence system na hizi mifumo miwili ni tofauti kabisa.
Hilo balloon liko kama 60,000ft juu na zile panels zina ukubwa wa mabasi matatu kwa makadirio wanayosema. Kwa kuwa wameshaona halina hatari yoyote kwa raia basi hawana haja kushusha mavyuma makubwa kuhatarisha usalama wakati yalivyo juu hayaleti hatari yoyote. Bado wakitaka kulishusha ni ngumu kwa kuwa F-22 pekee ndio fighter yenye uwezo wa manouvre altitude hiyo na upande ule wa Montana hakukuwa na base yenye F-22. Bado shida nyingine ni kwamba hilo ni balloon lenye vyuma chini na air to air missile zinaweza penya kwenye puto zisiwe activated. Ukitumia cannon inabidi uwe na manouvre nzuri kulenga shabaha ila bado shells hazitagonga kitu kizito kulipuka na zitadondokea makazi ya watu. So mara zote US huwa inaziacha balloons zikiwa urefu mkubwa.
Limeonekana kabla halijaingia anga la Marekani ila Pentagon inavyosemekana ilihitaji kujaribu kunasa mawasiliano linayofanya ipate mwanga kidogo kuhusu China inavyowasiliana na satellites zake.
Na nchi zote hizi zina satellites ambazo hupita anga za adui na kuchunguza kwahiyo hakuna maajabu kwa balloon sanasana linaweza nasa mawasiliano kwa ukaribu zaidi na accuracy kubwa ndio maana security measures zimechukuliwa.
Jambo la msingi linaloiumiza kichwa Marekani ni namna gani ya kulishusha bila kuliharibu ili walisome.