“Vita mpya ya Baridi” ya Marekani dhidi ya China itakuwa na madhara kwa Marekani yenyewe

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111452744150.jpg


Uhusiano wa pande mbili kati ya China na Marekani ni moja ya mahusiano muhimu sana duniani, na mwelekeo wa uhusiano huu unafuatiliwa sana na jamii ya kimataifa. Lakini pamoja na hayo, Marekani inaendelea na juhudi zake za kuikandamiza zaidi China katika maeneo mbalimbali kama vile siasa na diplomasia, uchumi, biashara, teknolojia na usalama wa kijeshi, mambo yanayodhihirisha waziwazi maana halisi ya vita baridi.

Kwanza kabisa, vita baridi ni hisia za kisiasa, na lengo kuu ni kudumisha umwamba wa upande mmoja na kukandamiza nchi ama pande nyingine ambazo ni dhaifu. Vita baridi pia haizingatii dunia ya usawa, ushirikiano na kunufaishana, ikimaanisha kuwa, kama ukiwa kiongozi wa mfumo fulani, hautakuw ana haja ya kusikiliza wala kujifunza, bali utafundisha, utahonga, na kutoa amri.

Hatua hii inaonekana wazi kwa nchi za Magharibi, hususan Marekani, ambayo imekuwa ikitoa amri na vitisho dhidi ya China. Marekani imeweka vikwazo vya kiteknolojia dhidi ya kampuni za China, na pia kujitahidi kwa kadri inavyoweza kuipaka matope China.

Mambo haya yote, badala ya kuipa shinikizo China, yamelisaidia taifa hilo kuongeza uvumbuzi na ubunifu wa kiteknolojia, na hatua hii imedhihirika baada ya kampuni kubwa ya mawasiliano ya China, Huawei, kuzindua toleo jipya la simu ya Huawei Mate 60 Pro.

Katika kuendeleza vita ya baridi, nchi za Magharibi hazikutilia maanani gharama halisi ambayo zitalipa kutokana na vitendo vyake vya kimwamba. Gharama hizi zinaonekana katika kuongezeka kwa shinikizo kwa sekta za kiraia, ikiwemo teknolojia na uchumi, huku nchi nyingine baki zikiendelea kuwa na umoja na kujitegemea zaidi, nadharia iliyoendelezwa miaka 50 iliyopita na kupuuzwa na nchi za Magharibi.

Kupanuka kwa BRICS na kuongezeka kwa nchi nyingine za Afrika, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kusini, ni hatua kubwa isiyotarajiwa katika ushirikiano wa pande na ncha nyingi. Hii ni kama vile nchi nyingine baki zinasema, ‘tunaweza kuendelea bila ya Marekani na Ulaya.’ Pia hatua hii inadhihirisha kuwa, ule umwamba wa nchi za Magharibi duniani, na kutaka maadili ya nchi hizo kutawala dunia kwa sasa haupo tena!

Lakini, vita baridi ya nchi za Magharibi dhidi ya China ni zaidi ya masuala yanayotawala vyombo vya habari, ambayo ni chip, biashara, suala la Taiwan ama Xinjiang ama Tibet. Vita hii inahusu mabadiliko ya kiujenzi katika njia ya binadamu ya kujiendeleza, na pia inahusu kama nchi za Magharibi zitajiunga na kuchangia maendeleo hayo, ama zitakuwa pingamizi la maendeleo katika dunia mpya.

Hakuna anayejua hali itakavyokuwa katika miaka 50 ama 100 ijayo, lakini kilicho wazi kwa nchi baki nyingine ni kwamba, licha ya vikwazo vyote, kuendeleza masikilizano na ushirikiano katika nguvu bora ni jambo lenye tija kuliko kuendeleza majibizano na nchi za Magharibi.
 
Back
Top Bottom