Mndali ndanyelakakomu
JF-Expert Member
- Dec 14, 2016
- 13,992
- 31,695
Dunia inamjua karume
Mwka 1964 siku thelathini baada ya uhuru wa bandia wa Zanzibar, wanamapinduzi kumi na nne wakiongozwa na mpigania uhuru John Okello aliwaongoza kwenye mapinduzi ya Zanzibar yaliyokuwa na umwagaji mkubwa wa damu.
Baada ya mapinduzi kufanikiwa John Okello [kiongozi wa mapinduzi] alichukua jukumu la kutangaza mapinduzi kwenye radio Zanzibar, ikumbukwe pia wakati mapambano yakiendelea ..aliyekuja kuwa rais wa Zanzibar mzee Karume na Babu walikuwa mafichoni na hawakushika wala bisibisi kwenye mapinduzi na hata ukiangalia ile picha ya wanamapinduzi ya kwanza John Okello amevalia kipolisi na amekaa kama kiongozi rasmi.
Baada ya hali kutulia Okello anamtangaza Karume rais na Abdulrahman Babu kuwa Waziri mkuu. Na ndie aliyeenda kumpokea Karume kutoka alikokuwa amejificha kwa siku kadhaa.
Baada ya siku chache mzee Karume akamfukuza Zanzibar kama mbwa John Okello [Field Marshal] na bila kujali mchango wake anatokomea kusikojulikana na historiaa ya mapinduzi ikafutwa na nafasi ya Okello ikaja kuwa mkwezi, mpiga tofali ambaye alibahatika kupiga picha [akiwa amekaa kitini katikati tu kwa sababu ya kuwa na kipaji cha kuongea - (kumbuka kuwa hata kiswahili chake kilikuwa 0kibovu)]
Naomba kuchokoza mada kuhusu nafasi ya John Okello kwenye mapinduzi, kwa nini historia ilifunikwa?
Je aliishia wapi,..wapenda historia ya kweli wameshatamani hata kujua lilipo kaburi lake..kumbukeni wenzetu Kenya baada ya kugundua hila wanahaha kutafuta kaburi la Field Marshal Dedan Kimathi...mbona wapenda hitoria Zanzibar na Tanganyika kwa jumla hamumtendei haki JOHN OKELLO [FIELDMASHAL]?
==============
Video ikimwonesha Okello,Karume na Babu masaa machache baada ya Mapinduzi
Field Marshall John Okello, kiongozi wa mapinduzi.LEO KATIKA HISTORIA: 1964: Wazanzibari wapigania Uhuru waliipindua Serikali ya Sultan Jamshid bin Abullah na kuanzisha utawala wao huru chini ya Abeid Amani Karume. Miezi mitatu baadaye Zanzibar iliungana na Tanganyika kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
View attachment 1322493
Imekuwa kawaida kwa gazeti la Monitor la Uganda kuadhimisha mapinduzi ya Zanzibar kwa kutoa makala zinazomtambulisha Field Marshall John Okello kama kiongozi pekee wa mapinduzi ya Zanzibar.
Mwaka huu wametoa makala iliyoandaliwa na mwandishi Felix Ocen inayomtambulisha John Okello akiwa na miaka 25 akiongoza kikosi cha watu 600 kwa muda wa masaa tisa tu na kufanikisha kumpindua Sultani.
John Okello aliyeingia Zanzibar miaka minne kabla ya mapinduzi, alikuwa mzaliwa wa familia ya kawaida katika wilaya ya Alebtong kaskazini mwa Uganda.
Okello, baada ya harakati zake za mapinduzi aliandika kitabu alichokipa jina The Revolution in Zanzibar, lakini kilipigwa marufuku kuchapishwa na serikali zote za Afrika Mashariki.
Gazeti linasema kuwa Okello aliongoza D-Day na wafuasi wake bila uwepo wa watu tunaoambiwa waliongoza mapinduzi hayo yaani Abeid Karume na Abdurahman Babu. Hawa wawili walikuwa wamefukuzwa visiwani na utawala wa Sultan, na walishangazwa sana kusikia kuna mapinduzi Zanzibar.
Okello alifanya siri mpango wake wa D-Day mpaka ilipofika usiku wa tarehe 11 January 1964, alipowakusanya wafuasi wake na kuwaamuru kuivamia kambi ya silaha ya Ziwani wakiwa na silaha za jadi.
Baada ya kufanikiwa kuiteka kambi ya silaha huku walinzi wa kambi wakitoroka, Okello na wafuadi wake walielekea mji mkongwe wakiwa wamejiimarisha kwa silaha kali. Kwa masaa machache walifanikiwa kuuteka mji mkongwe huku Sultan akikimbilia Dar es salaam kuomba hifadhi kwa Nyerere, lakini Nyerere alikataa na ikamlazimu Sultani kuelekea Mombasa kisha Uingereza.
Mpaka kufika asubuhi, Okello na wafuasi wake walikuwa wameshikilia vituo vyote vya muhimu huku akiwaamsha wazanzibari kwa tangazo "This is John Okello, the Field Marshall of Pemba and Zanzibar. Wake up you imperialists, there is no more imperialist government. Wake up you Blacks, pick the weapons and clear out the remnants of the imperialist government.... I am giving the Sultan 20 minutes to kill his children and wives and later himself, or else Okello will do it."
Mpaka kufika jioni watu takribani 13,000 walikuwa wameuliwa, huku zaidi ya 12,000 wakiwa waarabu. Viongozi wote ambao hawakufanikiwa kutoroka zahama ya Okello walitangaza kujisalimisha na kumuunga mkono Okello.
Okello aliunda kikosi cha wapiganaji wa mapinduzi kilichoitwa "Freedom Military Force" au Jeshi la Uhuru. Pia aliunda baraza la kwanza la mapinduzi, lakini walipompendekeza kuwa rais wa baraza alikataa. Badala yake aliwaita akina Karume kutokea Tanganyika, akampendekeza Karume kuwa Rais na Babu kuwa waziri mkuu.
Mengine fungua link usome wenyewe.
How Ugandan led revolution that ended Arabs reign over Zanzibar
Hapa kuna maswali kadhaa.
1. Kwanini CCM wanatudanganya watanzania na kuidanganya dunia?
2. Kuna faida gani tunazopata kwa kukataa kumtambua Okello kama kiongozi na baba wa taifa la Zanzibar?
3. Kwanini viongozi wa Afrika Mashariki walimwogopa Okello?
4. Inaonekana Okello alitekwa na watu wasiojulikana wakati wa utawala wa Iddi Amini na hajulikani alipopotelea mpaka leo. Serikali ya Zanzibar imefanya juhudi zipi ili haki za huyu Field Marshall zipatikane zikiwepo za kupewa heshima anayostahili?
Nawasilisha
Swali ni je, ni nani aliyaongoza hayo mapinduzi kama wote hao unaowataja hawakuwepo? Wewe ndiye unatakiwa kuukubali ukweli ndugu yangu...ukweli utakuweka huru! Hakuna Muunguja angeweza kukohoa mbele ya Sultani Sayyid Jamshid bin Abdullah Al Said!Achenikusambaza habari za uwongo.
Karume hakuwahi kufukuzwa Zanzibar. Aliondoka siku mbili au Tatu kabla ya mapinduzi na aliondoshwa na waliokua wakiyaongoza mapinduzi.
Babu hakuwepo Zanzibar karibu wiki tatu kabla ya mapinduzi kwa kua alikua akitafutwa na vyombo vya usalma baada ya kutishia kufanya mapinduzi. Na alikua Bara alikohifadhiwa na Nyerere.
Weqe mzee ni wakupuuzwa kabisa.SoNotorious,
Hili la ''old guy wants to establish islamic connection in erything
(everything), hii sio sawa...''
Jibu la hilo ni dogo na fupi.
Ikiwa wewe una wengine zaidi waliofanya haya ambao si Waislam
tueleze weka taarifa zao hapa JF tutazisoma lakini usinilaumu mimi
kwa kuandika historia za watu ambao mimi nakua katika mitaa ya
Dar es Salaam nawaona na wengine wakiingia hadi majumbani kwa
wazee wetu.
Unauliza kwa nini Kambona na Hanga huwaoni kujitokeza hadharani...
Labda na mimi nikuongozee wengine kidogo ambao hawajajitokeza
hadharani hadi hii leo ingawa wako hai.
Hanga na Kambona wangelijitokeza hadharani kabla au baada ya
mapinduzi ingelijulikana kuwa Zanzibar ilivamiwa na mamluki kutoka
mashamba ya mkonge ya Sakura kwenda kupindua serikali ambayo
ilichaguliwa kihalali.
Isingeishia hapo dunia ingelitaka kujua nani alimtuma Kambona
kufanya yote aliyofanya na kusababisha mauaji ya maelfu ya watu.
Isingeishia hapo tu dunia ingelijua nani aulizwe kuhusu mauaji yale
yaliyotokea.
Hiki ndicho kilikuwa kitisho kikubwa.
Hii ndiyo sababu wote walikaa kimya pamoja na Victor Mkello,
Ali Mwinyi Tambwe na Jumanne Abdallah.
Lililowatisha ni kuwa hawakutegemea kiasi kile cha mauaji.
Okello hakuwa chochote.
Okello alikuwa mpiga tarumbeta tu pale Raha Leo.
Viongozi wa mapinduzi na waliopanga mapinduzi yale Dr. Harith
Ghassany kawaeleza katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri
Uhuru.''
La mwisho.
Utapata tabu sana ikiwa kila unapoona majina ya Waislam katika
historia ya Tanganyika moyo unakuchoma.
Huwezi kuibadili historia hii.
Siku moja nilikuwa nazungungumza na Hamza Aziz basi kidogo
nikamchokoza kuhusu mapinduzi nikamwambia, ''Baba hebu nieleze
ukweli.''
Sikiliza jibu lake:
''Mimi nimekula kiapo cha kutunza siri siwezi kusema kitu ama
sivyo watanifunga. Mimi sasa nina miaka 74...''
Wakati ule wa mapinduzi Hamza Aziz ndiye alikuwa Inspector
General of Police (IGP).
Huyu mzee iko siku atajilipua muangalieni sana na mtoe taarifa.Baraghash,
Mapinduzi yanataka mipango na hao wanaopanga mipango humo ndipo wanapotoka viongozi.
Hakuna ushahidi katika historia ya Mapinduzi Zanzibar kuwa Okello alikuwa na kamati au kitu
kingine chochote unachoweza kukiita kamati au nini kuwa Okello alikuwa anaongoza katika hiyo
mipango ya mapinduzi.
Baada ya miaka 40 ndipo Dr. Ghassany akaja na kitu ambacho hakikuwa kinafahamika katika hii
historia ya mapinduzi.
Dr. Ghassany akaeleza kuwa mipango ya mapinduzi pamoja na fedha za kukamilisha hayo mapinduzi
ilikuwa Bara na kiongozi mkuu alikuwa Oscar Kambona kwa upande wa Tangayika na Abdallah
Kassim Hanga kwa upande wa Zanzibar.
Wengine waliohusika katika mpango huu alikuwa Ali Mwinyi Tambwe, Victor Mkello, Jumanne
Abdallah na Mohamed Omari Mkwawa.
Hayo mengine ulosema kuhusu Okello na hotuba zake na mengine ni katika vituko vyake ambavyo kwa
hakika ni vichekesho kama vile alivyokuwa akiamini kuwa yeye ni ''Field Marshall.''
Nilikuwa nikuzungumza kuhusu Okello na Badawy Qullatein yeye alikuwa kila akimtaja Okello anacheka.
Naamini ushajua kwa nini Qullatein alikuwa akimuona Okello ni kichekesho.
Okello hakupata kufika Kipumbwi walikotoka wapiganaji wa mapinduzi wala hakuwa anajua kuwa huko
Sakura kulikuwa na kambi ya mamluki.
Itoshe tu hiki ni kioja kuwa Okello awe kiongozi wa mapinduzi lakini awe hajui Karume yuko wapi na
kumpata amtafute kupitia kwenye radio.
Yako mengi sana katika vichekesho vya Okello.
In Sha Allah taratibu tutaelezana.
Wewe mzee ni kafiriBig Gift,
Mimi naweza nikafanya mjadala wa Okello na nafasi yake katika Mapinduzi ya Zanzibar
1964.
Kiitabu kilichoandika historia ya kweli ya mapinduzi ni kitabu cha Dr. Harith Ghassany,
msomi wa Harvard na ni Mzanzibari.
Mohamed Omari Mkwawa akionyesha kitabu, nyumbani kwa Mwandishi Tanga 2010
Kitabu chake kinaitwa, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' (USA 2010).
Dr. Ghassany alinichukua mimi kama Mtafiti Msaidizi.
Kwa ajili hii nina mengi kuhusu Okello na ambalo ninaloweza kukwambia ni kuwa hakuwa
shujaa wa mapinduzi.
Nakushauri ufungue uzi mwingine In Shaallah tujadili.
Mwandishi na Dr. Harith Ghassany
Tatizo la huyo Mohamed Said ni moja tu...udini! Huku Bara anataka tuwatambue Wazulu na Wamanyema kuwa ndio wapigania uhuru wa Tanganyika lakini huko Visiwani hataki kata kata kumsikia Field Marshall John Okello, mkombozi wa Wazanzibari akitajwa. Utadhani Tanganyika tulihitaji watu wa kupigania uhuru kwa mtutu kutukomboa. Ukweli ni kwamba tulikuwa tunasubiri tu muda muafaka tuwe na wasomi wenye uwezo wa hoja tupewe uhuru mezani kwa sababuTanganyika haikuwa koloni.Wewe mzee ni kafiri
Tatizo la huyo Mohamed Said ni moja tu...udini! Huku Bara anataka tuwatambue Wazulu na Wamanyema kuwa ndio wapigania uhuru wa Tanganyika lakini huko Visiwani hataki kata kata kumsikia Field Marshall John Okello, mkombozi wa Wazanzibari akitajwa. Utadhani Tanganyika tulihitaji watu wa kupigania uhuru kwa mtutu kutukomboa. Ukweli ni kwamba tulikuwa tunasubiri tu muda muafaka tuwe na wasomi wenye uwezo wa hoja tupewe uhuru mezani kwa sababuTanganyika haikuwa koloni.
Huyu mzee iko siku atajilipua muangalieni sana na mtoe taarifa.
Kazeeka vibaya, na watu wengi hivi sasa wanampuuza si vijana au watu wazima.Tatizo la huyo Mohamed Said ni moja tu...udini! Huku Bara anataka tuwatambue Wazulu na Wamanyema kuwa ndio wapigania uhuru wa Tanganyika lakini huko Visiwani hataki kata kata kumsikia Field Marshall John Okello, mkombozi wa Wazanzibari akitajwa. Utadhani Tanganyika tulihitaji watu wa kupigania uhuru kwa mtutu kutukomboa. Ukweli ni kwamba tulikuwa tunasubiri tu muda muafaka tuwe na wasomi wenye uwezo wa hoja tupewe uhuru mezani kwa sababuTanganyika haikuwa koloni.
Okelo alivunja Miko ya waliomtuma,Kwadwo. Unataka watu wa Unguja na watu wa Pemba wamtambuwe Okello? Okello hakutambuliwa na ASP wala TANU leo atatambuliwa na Wazanzibari. Hebu nioneshe wapi alipotajwa na vyama hivyo kwamba yeye ndie shujaa. Okello alikua mdini na ndio kilichomponza eti anasema kwamba kapindua kwaajili ya Ukristo?.