Sijawahi kuona vijana wajinga kama nyinyi.. Nilitarajia mpinge hoja za mtoa hoja kwa hoja. Matusi na kupuuza alichosema ni matumizi mabaya ya akili ndogo mlizonazo.... Naamini hata PolePole atashangaa kuona aina ya watu wanaotumika kujibu hoja za huku JF.
Hata hivyo sishangai, nimetumikia jumuiya ya Vijana kwa miaka mitano, Nawafahamu vizuri vijana wenzangu, hizi ndizo hoja zao hata kwenye vikao.
Ukisikia tamko lolote la jumuiya lisilo na matusi linalotolewa kwenda kwa mtu au kikundi cha watu wenye mawazo na msimamo tofauti na Chama, basi ujue limetolewa kwa shingo upande. Lazima litakuwa limetoka chini ya usimamizi kiongozi wa juu kuliko jumuiya yenyewe.
Rejea matamko yote ya jumuiya kwa miaka ya karibuni, anzia unguja mpaka kule bara.
Moja kati ya maeneo ambayo Polepole anatakiwa kuyafanyia kazi ni hawa vijana wa propaganda kwenye mitandao ya kijamii... Ukweli ni watupu sana kichwani.
Hata hizi mbinu za kuifungia JF ni matokeo ya hasira za wakubwa kufuatia kushindwa vibaya kujibu hoja makini za huku JF.