Mr Mike
JF-Expert Member
- Sep 5, 2016
- 222
- 466
Real Madrid kwangu mimi ndio timu pekee inayoweza sajili jina na likazaa matunda..Timu kama Madrid ipo juu kwenye soka Ulaya na Duniani kwa kufanya kazi bila kuangaliana usoni.
Unalipwa ufanye kazi ya watu kama kazi nyingine tu na siyo mchezo.
Hilo limewasaidia Madrid wachezaji wao wakongwe kuishi ktk misingi hiyo hata hawa madogo wakienda wanakuta ni kazikazi.
United alipoondoka SAF aliondoka na nguvu na ushawishi wake, kizazi cha wakina Rashford na Lingard kikakutana na mhuni kama Rooney (heshima kwake legend).
Sasa hivi timu imejaa mabishoo tu. Sancho, Rashford, Garnacho, Antony. Wakija madogo wengine nao wanakuta Carrington ni sehemu ya kula bata tu.
Mchezaji kama Pogba Pale Madrid wala asingekuwa anaongea shit..
Ibebe timu, ikubebe..
Imagine waliachana na Ronaldo ambaye bado alibeba kiatu Serie A..
Sancho tumefukuzia miaka miwili..
Anthony tumelipa €100
Then eti anacheza show off..
Nakumbuka Man City Vs nimesahau,,
Walikuwa wakiongoza magoli mengi sana, ikapatikana penalty..
Ederson akataka kwenda kuipiga ili nae aingie kwenye vitabu vya wafungaji..
Pep alikataa huo ushenzi..
Nidhamu kwa na heshima kwa mpinzani iwepo haijalishi unaongoza ngapi wala ni dakika ya ngapi..
