radika
JF-Expert Member
- Jul 15, 2014
- 20,450
- 32,290
Kibarua cha Kuirejesha Manchester United juu kimekuwa kigumu sana..
naweka akiba ya maneno ila..Only Pep Can Do That..
Our Ten Hag tutamuonea tu..
huwezi beba ubingwa wa EPL na wachezaji dizaini ya Sancho, Rashford, Antony, and co..
Manchester United inahitaji 5 Worldie kubeba EPL..as of now ni Only Casimiro..ndie World Class Player..
yule bwana hamis77 huwa tunamuona snitch ila kiuhalisia yupo sahihi..
Imagine Manchester United wame spend karibu £250M.. ila mpira bado hauna uelekeo..
Mchukue Rashford mpeleke Real Madrid, Bayern Munich, Manchester City, PSG, tuone atamweka nani benchi?
Safari bado ni ndefu..tuwe na subira..ingawa bila watu sahihi wa usajili safari ni ndefu zaidi..
ETH anaweza vizur sana kama akipata nguvu ya wamiliki Pep mwenyewe hatoboi na wakina Martial mpe heshima ETH
Chaguo la kwanza kabla hajaja lilikuwa Frenkie De Jong ma boss wa wa hii timu waliishia kupiga soga tu sajili zilizokamilika zilikuwa zimebak siku mbili au moja dirisha kufungwa ina maana pre season kocha hakupata machaguo yake mfumo ushaanguka hapo
Pep msimu wa kwanza alipigania top 4 tena city imetimia haswaa kuna David silva, Kdb,Kun Aguero ,Yaya Toure , Raheem Sterling ,Kompany & Fernandinho tena hao ni top player ambao united hamna hata mmoja mwenye uwezo huo kwa kipind kile hivyo bas kapata nguvu ya wamiliki yupo pale
Mwez wa kwanza aliomba striker wakat Martial kaumia hakupata ikabidi kocha aangalie option nyingine ya mkopo wa Wout Weghorst
Eriksen anaumia wanampa mkopo wa Marcel Sabitzer timu gani iliyo serious na mashindano wanafanya huo upuuzi? Manchestet united inang'ang'ana na mikopo tena iliyojifia
Mwezi wa kwanza kulitakiwa kununuliwa striker kisha mwez wa 6 anaongezwa mshambuliaji mwingine sasa mwez wa 6 anaweza kununuliwa mshambuliaji mmoja tu akiumia timu inarudi kwa sancho,rashfotd na martial + antony kocha gan anatoboa?
Pep anamuachia Jesus anamchukua halland
Manchester united wanamuachia Ronaldo wanamchukua Wout Weghorst
Huyo Pep anatoboa?


Kinachotokea sasa ndio makocha wote wazur walikipata chini ya wamiliki wa hii timu
Mourinho alilalamika sana kuhusu usajili kuna watu humu walimponda sana mourinho ila alikuwa sahihi leo tunaona kwa Martial kinachotokea
Wao wanaangalia nani anauza jez sio nani anapiga kazi
Solskjaer alitaka kumsajili Moises Caicedo kwa £4.5 Mwez 12 mwaka 2020 waligoma wakasema hela ni nyingi sasa uliza bei yake na hii kutokana na kutokuwa na jina kipind kile biashara isingeenda kwenye jez
Mpe heshim ETH hata Pep hatoboi chini ya uongozi wa hii timu.