Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ten Hag on Cristiano Ronaldo: "What the talk - if you ask about that - is between Cristiano and me. The statement is also clear, I think. He remains an important player in the squad."

#RonaLdoOUT
#GlazerOUT
#GGMU

manutd
 
Ana miaka 37 lkn anataka apewe muda wa kijana mwenye 20s, hilo ni tatizo kubwa sana.
Pole pole point zetu zinaingia. Angekua ole angeacha hadi kikosi apangiwe.

Ronaldo anavuna mkwanja mrefu, aache attitude mbona akiwa fresh anaweza kula dili la kocha mchezaji mambo yakaenda fresh. Vimechi vya hapa na pale.

Sasa unaanza kumpandia kocha kichwani ili iweje? Yeye ndio Boss, wewe ni mchezaji kama jina kubwa anzisha timu yako.

Mathieu Flamini yupo na USD billions 14, kimya kimya maisha yanaenda bila makamera hela ambayo sidhani Ronaldo atakuja ishika kwa attitude hiyo.

Maana umaarufu wake anautumia kujipatia kipato, ila attitude itafanya waone huyu kumuhimili kazi.

Messi alitulia zake hata Mbappe alipomuudhi akaachia mashabiki.

Dogo Greenwood uchoyo kidogo, jamaa kamnaga na kumuunfollow kabisa.

Wengine wana bahati asee.

500k per week alafu analeta ushubwanda na upo ligi inayofuatiliwa sana duniani.

Basi aende Saudi Arabia or Ureno uchochoroni awe anaonekana UEFA tu.

Ten Haag kaza. Bado Bruno aonywe.
 
January aende timu apendayo na fan boys wake. Kutujazia nzi bure.

Tupo na timu hadi kieleweke,

Eti mtu anakwambia Ronaldo ni mkubwa kuliko Man United, basi aanzishe timu ya Ronaldo, tuone itafika wapi?

Mkubwa kivipi? Vikombe?

Ballon D'or?
 
Na asije akafanya masikhara pia kumuongezea hata mmoja hawa wanaomaliza mikataba. Hata waonyeshe ubora kiasi gani msimu huu hii mifuko iende tu. (Rashford, Degea, Fred, Dalot, Jones, Tuanzebe, Ronaldo, Shaw, Heaton)

Hao wote hapo wanaweza kuwa kaburi lake siku za usoni akijikoroga kumpa hata mmoja mkataba mpya. Ukimuondoa Ronaldo ssb ya umri waliobakia wote hawana ubora wa kucheza United. (inconsistency performance)

Rashford, Dalot na Shaw hao ni uhakika 100% wataendelea kuwepo United beyond 2023. De Gea sababu ya falsafa ya kocha, huyo Nampa 50/50 itategemea na evaluation ya kocha mwisho wa msimu. Fred nae itategemea na upatikanaji wa De Jong, ila nae (Fred) uwezekano wa kuendelea kuwepo beyond 2023 ni mkubwa sana. Hao wengine Sina comment
 
Rashford, Dalot na Shaw hao ni uhakika 100% wataendelea kuwepo United beyond 2023. De Gea sababu ya falsafa ya kocha, huyo Nampa 50/50 itategemea na evaluation ya kocha mwisho wa msimu. Fred nae itategemea na upatikanaji wa De Jong, ila nae (Fred) uwezekano wa kuendelea kuwepo beyond 2023 ni mkubwa sana. Hao wengine Sina comment
Ni kweli ila hao wachezaji wote wanaomaliza mikataba yao mshabiki yeyote wa United aliyemkweli na nafsi yake anafahamu fika ni wachezaji wa hovyo wasio na uhakika wa kucheza kwa kiwango kizuri kwa muda mrefu.

Sifa namba moja ya kuwa na timu inayoshinda makombe ni kuwa na wachezaji wenye performance consistency. Swali la msingi hapa unaweza kuwaamini Rashford, Dalot, Shaw na Fred warejee msimu ujao kama key players?

Kama jibu ni hapana, basi fahamu hawa wachezaji hawafai kuwa hata squad players kwa ssb wana mishahara mikubwa sana. Na siku zote ukijaza wachezaji wenye mishahara mikubwa kikosini wanaku-limit kuleta talents mpya.

Leverage pekee ya Rashford kwa Ten Hag ni mchezaji pekee United anayeweza kucheza nafasi mbili kwa ufasaha japokuwa hayupo clinical akicheza kama mtu wa mwisho ila ana-fit ktk mfumo wake. Kwa upande wa Dalot naamini amempunguzia stress ya kutafuta #2 mpya yeye anafundishika focus kubwa itaenda idara nyingine.
 
Back
Top Bottom