Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ana miaka 37 lkn anataka apewe muda wa kijana mwenye 20s, hilo ni tatizo kubwa sana.
Pole pole point zetu zinaingia. Angekua ole angeacha hadi kikosi apangiwe.

Ronaldo anavuna mkwanja mrefu, aache attitude mbona akiwa fresh anaweza kula dili la kocha mchezaji mambo yakaenda fresh. Vimechi vya hapa na pale.

Sasa unaanza kumpandia kocha kichwani ili iweje? Yeye ndio Boss, wewe ni mchezaji kama jina kubwa anzisha timu yako.

Mathieu Flamini yupo na USD billions 14, kimya kimya maisha yanaenda bila makamera hela ambayo sidhani Ronaldo atakuja ishika kwa attitude hiyo.

Maana umaarufu wake anautumia kujipatia kipato, ila attitude itafanya waone huyu kumuhimili kazi.

Messi alitulia zake hata Mbappe alipomuudhi akaachia mashabiki.

Dogo Greenwood uchoyo kidogo, jamaa kamnaga na kumuunfollow kabisa.

Wengine wana bahati asee.

500k per week alafu analeta ushubwanda na upo ligi inayofuatiliwa sana duniani.

Basi aende Saudi Arabia or Ureno uchochoroni awe anaonekana UEFA tu.

Ten Haag kaza. Bado Bruno aonywe.
 
January aende timu apendayo na fan boys wake. Kutujazia nzi bure.

Tupo na timu hadi kieleweke,

Eti mtu anakwambia Ronaldo ni mkubwa kuliko Man United, basi aanzishe timu ya Ronaldo, tuone itafika wapi?

Mkubwa kivipi? Vikombe?

Ballon D'or?
 
Na asije akafanya masikhara pia kumuongezea hata mmoja hawa wanaomaliza mikataba. Hata waonyeshe ubora kiasi gani msimu huu hii mifuko iende tu. (Rashford, Degea, Fred, Dalot, Jones, Tuanzebe, Ronaldo, Shaw, Heaton)

Hao wote hapo wanaweza kuwa kaburi lake siku za usoni akijikoroga kumpa hata mmoja mkataba mpya. Ukimuondoa Ronaldo ssb ya umri waliobakia wote hawana ubora wa kucheza United. (inconsistency performance)

Rashford, Dalot na Shaw hao ni uhakika 100% wataendelea kuwepo United beyond 2023. De Gea sababu ya falsafa ya kocha, huyo Nampa 50/50 itategemea na evaluation ya kocha mwisho wa msimu. Fred nae itategemea na upatikanaji wa De Jong, ila nae (Fred) uwezekano wa kuendelea kuwepo beyond 2023 ni mkubwa sana. Hao wengine Sina comment
 
Rashford, Dalot na Shaw hao ni uhakika 100% wataendelea kuwepo United beyond 2023. De Gea sababu ya falsafa ya kocha, huyo Nampa 50/50 itategemea na evaluation ya kocha mwisho wa msimu. Fred nae itategemea na upatikanaji wa De Jong, ila nae (Fred) uwezekano wa kuendelea kuwepo beyond 2023 ni mkubwa sana. Hao wengine Sina comment
Ni kweli ila hao wachezaji wote wanaomaliza mikataba yao mshabiki yeyote wa United aliyemkweli na nafsi yake anafahamu fika ni wachezaji wa hovyo wasio na uhakika wa kucheza kwa kiwango kizuri kwa muda mrefu.

Sifa namba moja ya kuwa na timu inayoshinda makombe ni kuwa na wachezaji wenye performance consistency. Swali la msingi hapa unaweza kuwaamini Rashford, Dalot, Shaw na Fred warejee msimu ujao kama key players?

Kama jibu ni hapana, basi fahamu hawa wachezaji hawafai kuwa hata squad players kwa ssb wana mishahara mikubwa sana. Na siku zote ukijaza wachezaji wenye mishahara mikubwa kikosini wanaku-limit kuleta talents mpya.

Leverage pekee ya Rashford kwa Ten Hag ni mchezaji pekee United anayeweza kucheza nafasi mbili kwa ufasaha japokuwa hayupo clinical akicheza kama mtu wa mwisho ila ana-fit ktk mfumo wake. Kwa upande wa Dalot naamini amempunguzia stress ya kutafuta #2 mpya yeye anafundishika focus kubwa itaenda idara nyingine.
 
Rashford, Dalot na Shaw hao ni uhakika 100% wataendelea kuwepo United beyond 2023. De Gea sababu ya falsafa ya kocha, huyo Nampa 50/50 itategemea na evaluation ya kocha mwisho wa msimu. Fred nae itategemea na upatikanaji wa De Jong, ila nae (Fred) uwezekano wa kuendelea kuwepo beyond 2023 ni mkubwa sana. Hao wengine Sina comment
Ugomvi wangu mkubwa na Rashford ni incosistency. Rashford akiwa ktk ubora wake ni mchezaji pekee ninayemuamini akiwa uwanjani kuliko mchezaji yeyote pale United.
 
Mara nyingi nilikuwa namsapoti Ronaldo ila kwa kitendo alichofanya jana uzalendo umenishinda naona wachezaji wana morali ya juu ya kupambana kitimu yeye analeta mentality za ufather na kumpangia kocha hata kipindi yuko Real Madrid jamaa wakishinda wenzake hata timu ukishinda bila yeye kufunga hana hata raha hata kwenye kushangilia anashangilia kinyonge kiufupi mbinafsi sana na anapenda mafanikio binafsi ..
 
Naunga mkono hoja. Hofu yangu kubwa sana huyu Bruno ni loyal follower wa Ronaldo. Ila kwa namna yoyote ile Ronaldo anapaswa kuondolewa kikosini mwezi wa kwanza kabla hali haijawa mbaya zaidi dressing room.
Bruno ni loyal follower wa Ronaldo lakini Bruno ni very disciplined na anaipenda United.

Kumbuka kabla ya kuja Ronaldo Bruno alikuwa ndiyo mchezaji aliyekuwa na influence kikosini na ndiye aliyekuwa akiamua matokeo ya mechi nyingi za United.

Kuja kwa Ronaldo kuliua sana influence ya Bruno kikosini na kuna wakati huwa na associate kushuka kiwango kwa Bruno na ujio wa Ronaldo.

Kuondoka kwa Ronaldo kutaifanya timu icheze kwa uelewano mkubwa zaidi na Bruno atarudi tena kwenye ubora wake. Kuja kwa Ronaldo kulimuondoa Bruno kupiga free kicks, kulimwondoa kupiga penalty lakini pia kulimweka kwenye spotlight ya kukosolewa zaidi timu isipofanya vizuri ili kulinda legacy ya CR7.
 
Ile Trap aliyotega conte ya kumsifia cr7 ili aanzishwe iwe rahisi kumkaba, jana Ten kairuka vizuri tu

Matokeo mliyopata jana
Ni ushindi kwa ARSENAL, technically wazee wetu mnazidi kubariki hiki kikombe cha ligi msimu huu tukibebe

Pongezi za dhati kwa Fred, Nilishawai kumuelezea humu.
Kwamba leo mzima, kesho kichaa anapiga watu mawe


Haaland kiatu
Arsenal ndoo
Endelea kuota.
 
Back
Top Bottom