Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Skizeni nyie takataka ..mumeona usajili tulofanya? Nani ayiogopi Chelsea hahahaha nacheka uku naogopa ..maana tunaenda kumwaga damu EPL ..hahaha aise mutupe kombe letu tu Yani
Tushawapeni kombe la gahawa, kachukueni kwa mzee Jaah pale mwembe hanga.
 
ETH atoe ELANGA na Rash hii game aweke Sancho+CR+Martial ninahasira sana na awa Arsenali walitukanda 3-1 kwel na ubovu wao wa msimu uliopita Aseno ni wakutukanda 3 sisi???.....Ngoja tuone
Tunawakanda Tena ,hamna timu ya kucheza na Arsenal
Hivi Kuna mchezaji wa nyumbu anaingia kwenye kikos Cha Arsenal kwasasa?

Kesho tunawapigia samba

Na vile mnarukaruka pale Kati ,Xhaka lazima amsalimie degea
 
June 2023 wachezaji wafuatao watakuwa out of contract.

1.Rashford

2.Phil Jones

3.Fred

4.Ronaldo

5.Shaw

6.Diogo Dalot

7.Tom Heaton

8.De Gea

And to be honest mimi nitambakisha tu De Gea tena kuwa golikipa namba mbili na kwa mshahara wa chini..wengine wote ningefagilia mbali.

How about you?
Huu ni mtihani mujarab kwa DOF na Coach.

Usishangae Phill Jones akaongezewa mkataba.
 
Hata mie degea naona anastahili kubaki pia na babu Ronaldo kwa mkataba wa mwaka mmoja mbele.
Hao wawili mishahara yao unaleta wachezaji wazuri hata watano.

Sometimes tujifunze kwa Real Madrid na Man City, wanabaki na majembe tu.

Wakiona utamu unakwisha wanakuonyesha mlango wa kutokea.

Sisi United tunawashikilia wachezaji ambao hawapati namba hata 'mid table' teams.
 
Uamuzi upo mikononi mwake, achague kubadilika au kuendelea na tabia yake ya kiuchezaji alionayo, hata akipewa mkataba mpya bila ya shaka utakuwa na punguzo la mshahara.

Changamoto ya David ni kukosa kwake kujiamini, kuna nyakati jana alijaribu kuanzisha mpira kwa eriksen bila ya presha mpaka nikawa nashangaa na alifanya hivyo takribani mara tano.

Zilizobakia zote alikuwa anaangua nazi kwa goal kick.

Binafsi nalisubiria pambano kati ya ten hag dhidi ya bodi ya klabu na refereee wakiwa ni wachezaji.

Mmoja wapo ni huyo de gea na mkataba mpya.
Siku wamiliki walipozuia kuuzwa kwa phill jones ndo nikajua tuna wamiliki wathenge sijawahi ona.
 
So far kuna improvement kwenye defence ya United,partneship ya Martinez & Varane wamekuwa wanaelewana sana na wanajipanga vizuri na defence yote (back four) wamekuwa unit ,mmoja akifanya kosa wenzake wanawahi ku-clear .Only weakness kwenye defence ni Dalot na amekuwa ana-improve na wenzake wanamsaidia .Casemiro akishasettlle huenda katikati patatulia Erikson akisogea mbele tuweze ku-dictate midfield na ku-create more chance
Tunahitaji 'casemiro' mwingine.

Tuna michuano mingi, sio siku akiumia tuanze kushika vichwa.
 
Arsenal kwa kifupi wame yakanyaga wanaingia kinyume nyume kwenye ghetto la OT, lazima arsenal awe wa mfano leo kujua tupo serious arsenal mje kabisa na jeneza.

Mmeya kanyaga wakina@Arone Ramsey leo lazima mdeki bahari leo lazima mpigwe dog style.

Manchester united inacheza leo na dunia nzima ina furaha


Prediction

Man united 3 vs Arsenal 0

12:30 jioni

Mpapaso leo ni lazima

#GGMU
1662258010831.jpg
 
Arsenal kwa kifupi wame yakanyaga wanaingia kinyume nyume kwenye ghetto la OT, lazima arsenal awe wa mfano leo kujua tupo serious arsenal mje kabisa na jeneza.

Mmeya kanyaga wakina@Arone Ramsey leo lazima mdeki bahari leo lazima mpigwe dog style.

Manchester united inacheza leo na dunia nzima ina furaha


Prediction

Man united 3 vs Arsenal 0

12:30 jioni

Mpapaso leo ni lazima

#GGMU
View attachment 2344990
Ally pipi

Hi picha imepigwa Leo saa 1 jion
IMG_20220903_151948.jpg
 
Ten Hag kuhusu Lisandro Martinez: "Nilimtaka kwa ajili ya kuanzisha mpira lakini pia ubora wake wa kukaba, ugumu wake, uzuri wa kujiweka mahali sahihi, akili yake, na upambanaji wake. Anafanya vizuri ila anatakiwa kufanya vyema zaidi.

====≈===
Imetafsiriwa na ukurasa wa man utd swahili
 
Back
Top Bottom