Kwa jana sikuangalia game ya united kwa utulivu wa kutosha lakini kwa kiasi fulani Mctominay amecheza vyema ukilinganisha na zama za Ole. Na sio hapo tu,tangu game ya Liverpool na Soton dogo ameongeza kujiamini kwenye umiliki wa mpira,anaachia mara moja na anacheza rafu zenye akili kidogo.
Naomba siku ambayo Case atatulia kwenye timu,tuone combo yake na Fred the Red (yaani kuihamishia anchor ya Brazil United). Kwangu mimi hii itawezekana endapo mwenendo wa Bruno utaendelea kuwa wa kubahatisha kama wadau wengi wanavyopiga kelele dhidi yake kwa sasa,hivyo itakuwa mid 3 ya fred,case na eriksen.
Mbali na Maguire,wadau tumemsahau mapema sana the ice man Lindelof. Nilipenda kuona pacha yake na martinez in case varane pancha zikianza kumrudia ili kuwa na uhakika kuwa maguire hatarudi uwanjani hivi karibuni.
Katika defense,martinez ndio kabadilisha kila kitu hivyo nategemea kuona ubora wa lindelof anaouonyesha akiwa na timu yake ya taifa,sweden pindi watakapocheza pamoja.
Kwa game ya jana,sikujua kwanini Eriksen kawa man of the match. Mwenye uelewa anisaidie tafadhali.