Hadi tunaitwa wapumbavu asee.
Huyo jamaa atagharimu morale ya timu ikiwa hizi taarifa zinaenea alafu wachezaji wanaziona, ukute mchezaji kajituma alafu unakuta anayechukua pesa ndefu analeta ujinga na ukosefu wa heshima na hafanywi kitu.
Siku hizi ukute Ronaldo anataka afunge bila kujali hali ya timu ili kutuprove wrong, kwa hiyo sisi tunalalamika hafungi au tunalalamika anapoteza timu kuweza kuchukua Ushindi with consistency. Sio kila yeye afunge, tunapoteza muda mwingi kumpa mipira afunge wakati tukitanguliwa goli ndio imeisha hivyo.
Jamaa asepe tulete watu wa kazi kila mchezaji ajisikie kuitumikia kuleta ushindi, sio kila mchezaji akijaribu kufunga akose mara utasikia Angempasia Ronaldo, Madogo wana Dharau hawamheshimu Ronaldo, sasa kwa lawama hizo tutakua na timu inayojituma kweli?
Yaani hata Confidence ya Bruno kwenye penalty ishaisha, now akikosa utasikia Angempa Ronaldo what the f*ck?
Kama vipi Ronaldo aje kusaidiana na Maguire kwenye Ulinzi.
Maana kila kitu yeye.
Matatizo ni mengi ila tunaweza amsha moto kukiwa na morale ya kueleweka.
Morale ikifa kila mchezaji ni takataka.