Glazers ni moja ya matatizo ya United. Pesa yote unayoona inanunua wachezaji ni pesa inayotokana na mapato ya timu. On top of that Glazers waliinunua United baada ya kuchukua mkopo na deni lake wakalihamishia kwenye timu. Bado wakaona haitoshi wakaiweka Manchester United kwenye soko la hisa la NYSE, miezi michache nyuma walichukua gawio lao wakaweka mfukoni.
Budget inayowekwa kusajili wachezaji ni pesa timu inayotengeneza na siyo uwekezaji wa Glazers hata senti 5. Wao ndiyo wameweka structure za kusajili wachezaji wenye majina au ushawishi mkubwa ili timu ipate mapato zaidi bila kujali timu inafanya nini uwanjani.
Glazers ni tatizo kubwa sana kwa United walinunua timu ikiwa haina deni hata la sh 1. Sasa hivi wameibebesha mzigo wa madeni na bado wanachukua pesa kutoka kwenye timu, bado pia hawataki kununua wachezaji kwa wakati wanapohitajika pamoja na pesa yote timu inayotengeneza timu ni kwasababu mapato mengi wanachukua wao.
Wanavyoiendesha timu hao Glazers tajiri yoyote anaweza kufanya, Manchester United inajiendesha lakini inahitaji mtu mwenye mapenzi na timu, biashara ni sehemu ya football lakini wanachofanya Glazers ni kuitumia United kwa faida zao binafsi.
Maneno ya Mourinho, van Gaal na Rangnick yataishi milele.