"Lakini inaonekana bodi ya Man united haiko serious na usajili katika timu yao ni kama wanajaribu kubahatisha bahatisha."
Hapo ndiyo tatizo kubwa la United lilipo, shida kubwa inaanzia kwa wamiliki wao ndiyo walitengeneza mfumo wenye watu wasiojua mambo mengi kuhusu football. Watu hao ndiyo wakanunua wachezaji wengi wenye uwezo mdogo wengine wakaletwa kwasababu za kibiashara tu, wengine wala hayakuwa mahitaji ya makocha waliopita. Hayo yote ndiyo yametufikisha hapa tuna kikosi kimejaa majina tu. Hawa wachezaji ndiyo wanatutesa kwasababu hawauziki na hatuwezi kusajili bila kupunguza idadi ya wachezaji tulionao.
Na bado hiyo haitoshi wamiliki hawaweki pesa kwenye timu, wao wanachota tu faida. Msimu huu tumepata kocha mwenye malengo ya kueleweka lakini bado support ya wamiliki ni hamna kitu.
Hata hili la Ronaldo kubaki nina uhakika ni maelekezo kutoka juu, Ronaldo ni brand inayowasidia Glazers kutunisha mfuko. United siyo timu inayofanya cha maana uwanjani lakini bado inafamya vizuri kibiashara kwasababu ya akili wanayotumia Glazers kuliteka soko la mashabiki wa United.
Siku Glazers wakiondoka ndiyo itakuwa mwanzo mpya wa Manchester United. Mimi nimeshachoka kulaumu wachezaji, huu ndiyo uwezo wao walionao sisi tunataka wafanye kama thamani ya pesa tuliowanunulia ila hawa ni average players tukubali tu hali hilisi. Ila rebuild chini ya Glazers itakuwa ni kutwanga maji kwenye kinu.
Maneno ya Mourinho na Van Gaal yataishi milele.