Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ukiwa kocha mkuu wa man utd usionyeshe moyo wenye huruma dhidi ya wachezaji.
  1. Tyrell malacia amemuacha mbali sana kiubora luke shaw hususan kwenye role ya inverted fullback.
  2. wiki mbili nyuma nilisema ukiwa na dalot, Maguire, Fred, shaw, rashford na mctominay ndani ya uwanja Kwa wakati mmoja fahamu unajitengenezea mazingira magumu sana ya kiuchezaji. Ni Imani yangu mwalimu amepata funzo Kwa mara nyengine
  3. David de gea hajazaliwa wala kukulia Spain, anatudanganya
  4. Tunahitaji mlinzi wa kulia, Tunahitaji midfield wawili akiwemo frenkie de jong na Tunahitaji winga mmoja
  5. Tutaamka tena kabla ya jogoo kuwika
hujakosea pamoja na bruno
 
Wewe unadhani tatizo kuu ni lipi?
Kuondoka kwa mtu kama Ferguson kwenye timu aliyoitumikia kwa zaidi ya miaka 20 na aliyeweka falsafa zake zilizoota mizizi haliwezi kuwa jambo dogo, ilikuwa ni lazima Man u iyumbe hata kocha angekuwa nani, na ndiyo maana watu wanaojua alama za nyakati kama Pep walikataa kumrithi Fergie co kwamba hawakuwa wanapenda la hasha bali walijua isingekuwa rahisi. Fergie alimpendekeza Pep na walipata kuongea wakiwa USA lkn licha ya kipindi kile Pep kutokuwa na timu lkn aligoma kwa kisingizio eti anapumzika kwanza.

Hii timu tuvumilie tu atakuja wa kutuvusha japo tutatakiwa tubadilike kabisa tuachane na falsafa za Fergie na pia kuna aina fulani ya wachezaji wapo pale inabidi wapewe mkono wa kwaheri, kocha aanze upya na wachezaji anaowataka japo tatizo lingine ninaloliona ni kila kocha anayekuja pale anakwambia ana kikosi kizuri baadaye mambo yanamuendea kombo.
 

Safi kabisa, nililiona hili, hivi ni timu gani pale EPL haina CDM na kocha akafurahia kabisa kuanza ligi?

Pep alikuwa na Fernandinho lakini alinunua Rodrì ili fernandinho anavyoisha Rodri awe amezoa,mnaona moto wa Rodri.

Huwezi kuwa na timu haielewi hata mchezàji gani anaichezesha ukategemea kitu toka kwenye hiyo timu zaidi ya hiki tunachoona kwa United.
Nilimshangaa sana EtH kwa kukubali mpaka anaenda Preseason na hana CDM.



Kwani kule si mlimfunga Liver 4 mpaka mkaomba ligi ianze
 
Man U inaweza isiwe na world class players, TRUE. Lakini still kwa hii bunch iliyopo sasa hivi sio ya kupigwa 6 na Brentford & Brighton huku yenyewe ikifunga goli moja tu.

Tuache lazyman's analysis.
Hawajafunga goli hata moja, ilikua ni own goli na brighton
 
Rangnick alivyotangaza kukubali kazi ya Austria nikasema timu inaenda chini zaidi ndiyo maana hata yeye hana imani nayo ameamua kuondoka na ile nafasi ya ushauri haitaki.

Nikajibiwa ushauri atafanya huku anakua kocha Austria. Baada ya siku kadhaa akajiuzulu huo ushauri. So mi narudia tena kusema kwamba timu bado haina project ya maana.

Mashabiki wa United Pogba alisema hawajui mpira. Ni ngumu kidogo kumpinga Pogba kwenye hili hebu kumbuka jinsi mashabiki walikua wanapiga kelele wanahitaji winga na winga ni Sancho.

Sancho amekuja. Ana magoli 3 katika mechi 30. Lakini huwasikii mashabiki wakisema kwamba wanahitaji winga yaani wanazuga kua tatizo la winga limeisha.

Wakaanza leta lawama kwamba wanahitaji DM. Mi ninavyojua Fred ni DM na Scot ni DM, ila mashabiki wanaamini Rabiot ndiyo dawa ya hii ishu. Sasa waulize hao mashabiki kama wamewahi muona Rabiot akicheza.

Rabiot alikua mzuri akiwa PSG, akaenda Juve akawa average, Juve na PSG zipo ligi mbili tofauti yawezekana alishine PSG kwakua PSG ipo farmers league. Akiwa Juve akawa hapangwi akaanza maneno yeye na mama yake wakawa wanaishambulia Juve mitandaoni.

Sasa mchezaji wa tabia hizi akija timu ambayo ipo hovyo tutarajie nini? Sasa jiulize ni kweli mashabiki walihitaji winga au walimhitaji Sancho? Na saa hii ni kweli wanahitaji DM au wanamhitaji Rabiot?

Narudia tena. Shida ya United ni kocha.
 
Mkuu unataka kuniambia hawa brentford wana wachezaji wakali kuliko hao uliowataja? Kwamba utd inahitaji iwe na de jong, Rabiot kuifunga Brentford?
Hii timu imefikia hatua haifundishiki.

Hili ndiyo lililowazi timu zinakuja zikjua kupress tu tayari tunapoteana.
 
Back
Top Bottom