Mkuu hii hali ya timu kucheza vizuri kwa vipindi imeanza kwa Ole.
Msimu wa kwanza wa Ole timu ilikuwa tia maji tia maji mpaka alipomsajili Bruno.
Msimu wa pili wa Ole timu ilicheza vizuri mechi 18 za mwanzo baada ya hapo tukapoteana january na february nzima mpaka Man City akatupita.
Chini ya Ralf timu ilicheza vizuri mechi moja tu baada ya hapo ikarudi kwenye default setting yake.
Unazungumzia wakati wa Van Gaal by the way mpaka sasa ni wachezaji watatu kikosini walioachwa na Van Gaal ukiondoa Phil Jones ambaye mimi simweki kwenye kundi la wachezaji wa timu.
Hii timu yetu imekuwa kama mgonjwa wa Erection Dysfunction akipata viagara inasimama baada ya hapo inalala tena mpaka upate dose tena.
Erik ten Hag akitaka kufanikiwa na hii timu asiwaamini sana wachezaji aliowakuta aanze project mpya kwa kuingiza wachezaji wengi wa kwenye academy ambako kuna talents nyingi tu.
Wale wahuni wakipunguziwa game time watabadilika na wengine wataanza kujitoa wenyewe. Kama ulivyoona yule mhuni mkuu kakimbilia Juventus.
Angalia vizuri source zako mkuu
Msimu wa pili wa ole timu haikuanza vizuri, mechi za mwanzo tulipigwa 6 na spurs, palace, draw arsenal etc
Na hio january na feb haikuwa mbaya yes tulikuwa kwenye bad form ila at same time tulimfunga Soton 9, February mechi 4 tumeshinda 2 draw 2, Jan mechi 6 tulishinda 3 na draw 2 na tukafungwa na Shefield.
Baada ya hio Bad patch of form tukacheza vizuri tena.
Timu zote Uingereza zinapitia form kama yetu including Man city na Liverpool, sema tu Timu kama City wana depth kubwa.
Mfano Kuna Msimu Bernado silva anakuwa Player of the year, Msimu unaofuata anakalia Bench, unakuta msimu huu KDB yupo fresh msimu unaofuata majeruhi, wachezaji wao wengi Sterling, Aguero, Mahrez etc walikuwa wakirotate vibaya mno sababu ya depth yao.
Sisi je? Makocha wote watatu hakuna hata mmoja aliekuwa supported baada ya kuingia Top 4,
-msimu wa kwanza wa Ole alivyoingia top 3 kaletewa VDB, Cavani, Telles, Amad na Pelistri. Tukasikia Minong'ono kibao Kocha hakumuhitaji VDB, Cavani nae pia tetesi hakuwa kwenye mipango ya kocha.
-kwa mou vile vile Alivyoshika nafasi ya pili Alimtaka Maguire, akataka na Winga etc hakuletewa matokeo yake Alipewa Sanchez na Fred yaliyotokea tunajua.
-LVG alitaka pacy wingers na tuliona namna alivyomtumia Martial, nae hivyo hivyo alivyoingia top 4 target zake nyingi hazikuletwa aliletewa tu Babu Bastian.
Ingekuwa makocha wote hao wanapata Tagert zao ama wachezaji wanaofaa mifumo yao hata kama wangefeli isingekua disaster. Hata mchezaji akiumia ingekua timu haiathiriki sana.