Mkuu hii hali ya timu kucheza vizuri kwa vipindi imeanza kwa Ole.
Msimu wa kwanza wa Ole timu ilikuwa tia maji tia maji mpaka alipomsajili Bruno.
Msimu wa pili wa Ole timu ilicheza vizuri mechi 18 za mwanzo baada ya hapo tukapoteana january na february nzima mpaka Man City akatupita.
Chini ya Ralf timu ilicheza vizuri mechi moja tu baada ya hapo ikarudi kwenye default setting yake.
Unazungumzia wakati wa Van Gaal by the way mpaka sasa ni wachezaji watatu kikosini walioachwa na Van Gaal ukiondoa Phil Jones ambaye mimi simweki kwenye kundi la wachezaji wa timu.
Hii timu yetu imekuwa kama mgonjwa wa Erection Dysfunction akipata viagara inasimama baada ya hapo inalala tena mpaka upate dose tena.
Erik ten Hag akitaka kufanikiwa na hii timu asiwaamini sana wachezaji aliowakuta aanze project mpya kwa kuingiza wachezaji wengi wa kwenye academy ambako kuna talents nyingi tu.
Wale wahuni wakipunguziwa game time watabadilika na wengine wataanza kujitoa wenyewe. Kama ulivyoona yule mhuni mkuu kakimbilia Juventus.