Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ben Yedder no 9 Nzuri sana jamaa hajawahi Funga Goli chini ya 18 toka 2018, Monaco wamemchukua Belloti pengine akawekwa sokoni.
 
1. Lautaro Martinez
2. Andrea Belloti
3. Patrick Schick
 
Sijui kwa nini sajili za awamu hii zinanifurahisha except De Jong.

Fundi kaja. Huwa navutiwa sana na sajili zisizokuwa na mlengo wa kibiashara nyuma yake. Malacia & Eriksen - genius signings!

Hawa ni aina ya wachezaji wasiokuja na ego bali wanakuja kufanya kazi.
 

Attachments

  • Eriksen.png
    7 KB · Views: 15
Man Utd ni brand kubwa tu.

Automatically mchezaji anakuwa star.

Nimefurahishwa na sajili zenye tactics ndani yake..
 
Huwezi kuelewa.Hujui kama Ronaldo ndiye aliye mfukuza Ole kazi. Au mahaba yamedizi
Ama kweli mashabiki wa kibongo ni watu wasiojielewa na wala hawajui wanataka nini, msimu uliopita OLE OUT OLE OUT OLE OUT zilikuwa nyingi sana humu na huko ulaya kabla hata Man Utd haijajua kama kutakuwa na uwezekano wa kumsajili Ronaldo.

Leo u awezaje kusema kuwa Ronaldo ndiye aliye mfukuza Ole pale Man utd?

Njooni na hoja za maana mnapoamua kuelezea ni kwanini Cr7 ndiye chanzo cha kufeli kwa Man Utd msimu uliopita, na sio hoja za kijinga kama hizo.
 
Acha ujinga kijana.

Pale klabuni hakuna wa ku-replace magoli ya Ronaldo.

Hakuna mchezaji mwenye ari ya uchezaji kama Ronaldo.

Akipata timu yenye wachezaji sahihi anakupa magoli 25 bila shida pamoja na uzee wake.
Shida ni kwamba watu wameendekeza ushabiki wa ki-hoyahoya , mtu anakwambia eti Ronaldo ndo kfukuzisha Ole wakati hashtag za OLE OUT zilianza mapema tu hata kabla Ron hajaja Man Utd.


Mimi nataka apatikane mtu wa kueleza kwa kina (kiufundi) ni kivipi Cr7 kaifelisha Utd ya sasa, na je tatizo la midfield na backline (ambayo ndo uozo wa Utd), nayo tumtwishe Ronaldo?
 
Hapa sasa umeamua kuja na hoja za kichekechea kabisa na yoyote mwenye akili hahitaji kutumia muda mwigi kujua kwamba una nongwa zako juu ya CR7, either ni team Messi au whatever.

Hivi unawezaje kuhusianisha tukio la Mason kupiga demu wake na uwepo wa Man Utd pale Manchester? Hii hoja ni ya kitoto kabisa, kwahiyo ikitokea wapo wanaonyimwa unyumba nao itakuwa ni kwasababu ya Robaldo?


Mimi nipo hapa kusubiri atakeeleza kiufundi ni kwanini Ronaldo ndiye aliyeifelisha Utd licha ya kuchangia mabao mengi kuliko mchezaji yoyote, anahusika vipi na magoli mengi tuliyoruhusu msimu huu, anahusika vipi na midfield yetu iliyooza?


Nyinyi jengeni team tu ila hizi habari za kutafuta mtu wa kumuegemezea zigo la mavi ni utoto tu, Ile Utd ilikuwa imeoza kuanzia nyuma, katikati na huko mbele alibaki Ronaldo tu mwenye makali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…