Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu Chief,hii mbona iko wazi kabisa. AWB hana asili ya kusaidia mashambulizi hivyo inamlazimu Lindelof akafanye hiyo kazi naye atafanya majukumu ya kiulinzi kwa niaba yake. Tofauti na Dalot,yeye akili yake iko kwenye kushambulia zaidi hivyo hutamuona Lindelof akienda mbele wakati tayari Dalot kashaacha nafasi huku nyuma.

Kwa upande wa mbinu uko sahihi kwamba AWB anafaa kufanya man marking kwa winga anayehatarisha usalama wetu kuliko Dalot. Ingawa kwa kiasi fulani matumizi ya fullbacks yamebadilika hivyo sisi hatuwezi kufanya tofauti na wenzetu wakati hatupati matokeo chanya kwa mbinu hizo. Hoja ya msingi ni kwamba kama uchezaji wa AWB utaendelea kubaki hivyo daima alitakiwa kuwa squad player na sio starter kama Ole alivyokuwa anatuaminisha.

Ni imani yangu endapo mwalimu mpya akija na akapewa nafasi 5 za kuboresha kwenye kikosi chetu,hata eneo la RB ni miongoni mwa hayo maeneo.
Bissaka Huwa ana shambulia na kurudi kukaba.

Dalot Huwa mara nyingi ana shambulia TU,anacheza kama wingaa kuacha gape na kufanya namba 4 akabe nafasi yake.
 
1. Man city
2. Liverpool
3. Arsenal
4. Chelsea


Mbio zipi ambazo zipo wazi?
Ligi haijaisha Mkuu. Hayo uliyo yaandika ni matamanio Yako TU .

Ndo utamu WA Epl,hautabili mpaka mwisho WA safari... Dadeq
 
Manchester United waliamua kuachana na mpango wa kusajili mchezaji kwenye hili dirisha dogo la usajili kwa sababu ya ugumu wa kufanya biashara ya mchezaji,

sababu nyingine ya msingi ni kwa pande zote mbili kufikia makubaliano ya kutokusajili mchezaji hususani wa kiungo kwa dhumuni la kutokuingilia mipango ya kocha wa kudumu ajaye.

kwa mfano taarifa zinadai ralf rangnick alimuhitaji haidara wa Leipzig au yule kiungo wa Borussia aliyekwenda Juventus.

jaalia kocha ajaye akasema haidara haendani na falsafa yangu hivyo auzwe unadhani ni sahihi?

ndio maana klabu haikuhangaika na usajili ila ikaruhusu kuondoka kwa baadhi ya wachezaji kwa mkopo kwa kipengele cha kutokuuzwa.

kocha ajaye ndiye atakayeamua khatma ya kila mchezaji kuanzia wale walioishiwa mikataba kama pogba na wale walio kwa mkopo.

jitahidi kufuatilia taarifa.
Kocha alimtaka haidara baada ya kuona maji yamemfika shingoni.Lakini alikabidhiwa timu alisema Hana haja ya kufanya usajiri wowote,timu Ina watu wenye vipaji.Kukatokea mzozo wa martial kupigwa benchi Siku nyingine kutokucheza kabisa,kocha akasema anae hitaji kuondoka aondoke mlango uko wazi ndo maana martial na beek wakatembea.Uwe makini unapo fatilia tarifa.
 
Sijasema umeanza leo. Ila kwa falsafa ya modern football hautaleta matunda....
Angalia vilabu vilivyofanikiwa zaidi kwa miaka 10 ilopita pale England, angalia falsafa zao kwenye recruitment, angalia squad zao, angalia miongozo & maamuzi ya viongozi wa uwanjani & locker room....
Compare na United, I hope you see the difference. Hiyo ndo point yangu


Sent using Jamii Forums mobile app
Hao walio fanikiwa ni falsafa zao huwezi kusema man utd iige kutoka kwao ingali man utd Ina falsafa yake Mkuu.

Utaiga vingapii???
 
Baada ya international break, nyumbu zitaanza kuingia kwenye heat.

Akianza kucheza mashabiki wake duniani kote wataanza kulia mooo mooo, wanalilia dume.
Wataanza kulia lia Sana kama wachezaji hawajawaona kwenye timu zao za taifa wakicheza,Ila ngoja wafike kwenye club Yao.watakupa list yao kuwa hawasitahili kuichezea timu yaoo

Pogba,Shaw,magwaya,Cr7,Scott,baily
 
laurie whitewill ameandika(huyu ni tier 1 kwa taarifa za man utd): klabu imepanga kusajili wachezaji wanne kupitia maeneo tofauti. (1) viungo wawili, mmoja ni eneo la ulinzi na mwengine ushambuliaji (2) winga wa kulia, teh teh teh (3) mshambuliaji na kipaombele kikuu ni harry kane bila ya kujali kocha ajaye, mazungumzo ya usajili wake yalifanywa kati ya ed woodward na daniel levy msimu uliopita. gharama za usajili wake itakuwa ni paundi million 100 au zaidi. kama dili litashindikana ndipo wataangalia mshambuliaji mwengine kama vile nunez wa benfica anayegombaniwa zaidi na arsenal.(4) jorge mendez yupo kwenye mchakato wa kutafuta mshambuliaji mbadala wa harry kane kwa timu ya ..... (5) usajili wa kane pia utategemea na mipango ya man city wanaomgombania haaland au kane. fuentte hiyo namba tatu umeisoma vizuri?
Nimekuelewa sana mkuu.
Wao wana kamsemo kao kuwa PREMIER LEAGUE PROVEN! Lakini leo hii wachezaji wanaokinukisha pale city (bernado,laporte,cancello,dias,gundogan,etc),liverpool (diaz,alcantara,keita,etc),chelsea (kovacic,joginho,mendy,havertz,etc) pamoja na ile pool ya Wolverhampton wanderers hawakuwa wachezaji waliotokea ligi yao.

Kane sio mchezaji mbaya kamwe ila kusajiliwa bila kuangalia mahitaji ya mwalimu kisa uingereza wake ndipo tatizo la man utd linakuja. Na hapa ndipo kauli ya LvG inapopata umaarufu zaidi.
Tujipe muda mkuu.
 
Huyo ni RR au Sosha?

Maana RR hata kabla haja kabidhiwa timu alikuwa anajinadi Sana kuwa timu Ina vipaji.Badae akaanza kulalamika wachezaji hawafati maelekezooo.Inafurahisha Sana.
sosha mkuu
 
Adjustments.jpg
 
Hamna kikosi cha kumfunga Leicester city


Magwaya ni mzima wa afya kufuatia hiyo game
 
Hamna kikosi cha kumfunga Leicester city


Magwaya ni mzima wa afya kufuatia hiyo game
Unataka Nini? Deal na mechi zako Mkuu! Nani kakwambia una kikosi Cha kumfunga crystal palace ambaye city alishindwa kumfungwa home and away??
 
halafu badae uanze kulalamika kocha alimchukua Dyabala wa Nini wakati Kuna Bruno,Mata,Pogba,Fred,Elanga wanaweza kucheza nafasi anayo cheza Dyabala
Mchezaji yoyote awe bora vipi akija team yoyote akawa flop hakuna ambaye hataacha kulalamika hiyo ni fact, Akija kocha mpya akamuhitaji utasema kuna hawa wanacheza nafasi yake? Yaani kabisa unamuhesabu Mata katika wachezaji chief na aaminiwe 1st 11? Anyway nikuulize katika hao uliotaja hapo yupi anaweza muweka bench Dybala aliye fit kabisa kama wanafika / kuzidi watatu?
 
Back
Top Bottom