tatizo lilianzia kwa mwalimu aliyepita hakuweza kuweka msisitizo juu ya mambo hayo matatu mbele ya hadhara na hata kwenye viwanja vya mazoezi, amekuja mwanadamu anayehitaji sifa hizo tatu wachezaji wanahisi uzito kubadilika.
bahati mbaya sana kwa wakati huu upepo umewavumia vibaya wachezaji wetu kwani hakuna chochote watakacho kilalamikia mbele ya hadhara au kwa kuvujisha taarifa kama wafanyavyo baadhi yao wakaaminiwa na kuungwa mkono kama ilivyotokezea hapo nyuma (kuanzia Ole hadi mourinho)
kwa sasa presha imehamia kwao na kwa ushahidi wa hilo
- jaribu kufuatilia mahojiano ya maguire hapo juzi (yeye kama nahodha inasemekana aliitisha mkutano rasmi wa wachezaji na kocha kuzungumzia mwenendo wa timu)
- fuatilia majibu ya bruno baada ya kuvumishiwa tetesi za kuhamia barcelona, umeona wapi mchezaji wa ulaya kujibizana na tetesi za magazeti ya kufungia maandazi
- fuatilia post ya fred hapo juzi akikemea taarifa za uongo zinazosambazwa juu yake
- fuatilia post ya rashford hapo juzi
- fuatilia maneno ya msemaji wa pogba alipokanusha habari za kwamba mteja wake amefikia makubaliano ya kupewa mkataba mpya wa paundi laki 5.
kwa sasa wana machaguo mawili yanayowakabili nayo ni:
- kufuata matakwa ya mwalimu (kocha ameendelea kusisitiza pressing 😛😛😛
- au kuendeleza ukaidi ndani ya uwanja baadae wapambane na matusi ya mashabiki na pundits.
tumemsikia evra akitoa duku duku lake
roy keane kama kawaida yake ameendelea kumpa za uso harry maguire
lou macari naye amebwatuka