Forgotten
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,630
- 11,096
Yametimia Wolves ni aidha uwafunge moja au wakufunge moja au msifungane.Game ya leo itakuwa siyo la kitoto Wolves wapo radhi mechi iishe 0 - 0 ila siyo uwafunge kirahisi, hii mechi tutashinda tukiwa na defense nzuri ni mechi tunayoweza kupata goli 1 tu na ili upate hizo points 3 ni lazima uwe na walinzi wazuri.
Nakumbuka mechi ya kwanza msimu huu tuliwafunga Wolves 0 - 1 ila ni mechi iliyokuwa inaisha kwa droo au kufungwa kama tu Wolves wangekuwa makini. De Gea alituokoa dk za mwanzo kabisa uso kwa uso na Jimenez, Bissaka akaokoa mpira kwenye mstari baada ya Fred kufanya makosa katikati ya uwanja kwa kushindwa ku-control mpira. 2nd half De Gea akatuokoa baada ya corner ya Wolves kwa kufanya double saves.
Mechi ya kwanza tulishinda kwasababu ya form ya Greenwood akifunga mechi ya kwanza na ya pili kuokoa point moja mbele ya The Saints na kutupa alama 3 muhimu katika mechi tuliyocheza vibaya dhidi ya Wolves. Shuti la Greenwood lilimzidi nguvu goalkeeper ndiyo ikawa pona yetu.
Mechi ya leo Greenwood na McTominay ni watu muhimu kuanza, ndiyo wachezaji pekee kikosini wenye mashuti makali yanayokuwa on target. Kama mechi iliyopita mashuti ya McTerminator nje ya box ni muhimu sana na leo.