Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Game ya leo itakuwa siyo la kitoto Wolves wapo radhi mechi iishe 0 - 0 ila siyo uwafunge kirahisi, hii mechi tutashinda tukiwa na defense nzuri ni mechi tunayoweza kupata goli 1 tu na ili upate hizo points 3 ni lazima uwe na walinzi wazuri.

Nakumbuka mechi ya kwanza msimu huu tuliwafunga Wolves 0 - 1 ila ni mechi iliyokuwa inaisha kwa droo au kufungwa kama tu Wolves wangekuwa makini. De Gea alituokoa dk za mwanzo kabisa uso kwa uso na Jimenez, Bissaka akaokoa mpira kwenye mstari baada ya Fred kufanya makosa katikati ya uwanja kwa kushindwa ku-control mpira. 2nd half De Gea akatuokoa baada ya corner ya Wolves kwa kufanya double saves.

Mechi ya kwanza tulishinda kwasababu ya form ya Greenwood akifunga mechi ya kwanza na ya pili kuokoa point moja mbele ya The Saints na kutupa alama 3 muhimu katika mechi tuliyocheza vibaya dhidi ya Wolves. Shuti la Greenwood lilimzidi nguvu goalkeeper ndiyo ikawa pona yetu.

Mechi ya leo Greenwood na McTominay ni watu muhimu kuanza, ndiyo wachezaji pekee kikosini wenye mashuti makali yanayokuwa on target. Kama mechi iliyopita mashuti ya McTerminator nje ya box ni muhimu sana na leo.
 
Mzungo wa kwanza tena wakiwa kwenye fomu kwelikweli karibia timu kubwa zote zilishindwa kuwafunga ila sisi tuliwatandika tena nyumbani kwao.
Sasa leo wapo machinjioni unategemea tuwaache?
Sawa ngoja tuwaone wanaume wa shoka nyumbu fc.
 
Jamaa nyeupe anaiitaga nyeupe, sio mnafiki
jamaa namuelewa sana, ni mashabiki wachache sana wa ASANI-ALI wenye caliber yake na ndio maana anapata tabu sana kwenye jukwaa lao.
Yaani computerarsenal akikosoa ubora wa wachezaji wao au timu kwa ujumla mashabiki wenzake wote wanamjia juu na kumuita mamluki.
 
Mzungo wa kwanza tena wakiwa kwenye fomu kwelikweli karibia timu kubwa zote zilishindwa kuwafunga ila sisi tuliwatandika tena nyumbani kwao.
Sasa leo wapo machinjioni unategemea tuwaache?
Hapo machinjio gani hapo ..watu wanakuja mpk wanawagonga goli 5 hapohapo ndo unapaita machinjioni
 
gengeni press
IMG-20211228-WA0003.jpg
 
Leo Maguire ayupo ila hatari iliyopo anacheza jones ndo inatakiwa aanze maana hakuna mtu mwingine wa kuanza tofauti na jones baily,lindelof wote injury kwaiyo tumtegemee jones kuanza leo baada ya miaka kibao kutokuingia uwanjani.
 
Back
Top Bottom