Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tatizo lenu mnafata sana mkumbo yani unasema Zidane alikuwa na kismati, UCL 3 kwa misimu mitatu mfululizo unaita kismati!? Mnaangalia mpira gani? Kwahiyo pale Madrid wachezaji walikuwa wanajichezea tu bila mbinu za kocha sasa kwanini wachezaji wa United wameshindwa tu kujichezea kuifunga hata Leicester City kama mpira ni kukusanya wachezaji tu na kujichezea.
Sawa ni kocha mzuri, alivyorudi kwa mara ya pili alikwama wapi?
 
Issue si mafanikio bali rebuild itakayohitajika pale mambo yatakapo paranganyika. LVG, Mou, Ole, kila kocha ana style yake na kila kocha amesajili wachezaji wake sababu mfumo wa aliyemtangulia ni tofauti na wake. Conte akija nae ana wachezaji wake tofauti, na wachezaji wake Makocha wengine hawawezi kuwatumia, mfano Chelsea Alimuacha Victor Moses kama Key player na Marcus Alonso, nani Duniani anaweza Kushinda Epl na Victor Moses kama Key player? Ilibidi kufanyike Rebuild kubwa wakati wa lampard mpaka kuja kuwa na mafanikio ya Tuchel.

Timu zinazoendeshwa vizuri wanakuwa na makocha wao na kocha mpya akija Rebuild si kubwa sana, Angalia Bayern nadra sana kuona Core ya Timu imebadilika ila makocha wanabadilika, Barca ya Zamani, Juve, Man City etc
Kwa sasa United ina wachezaji ambao wakipata kocha mzuri timu itasonga mbele ,ukileta kocha ambae ni yes man (like OGS) hiyo rebuild itachukua hata miaka 20.Wachezaji wengi viwango vyao vimebaki pale pale sababu kocha anayewafundisha hakuwa na ubavu wa kuwaeleza ukweli (Shaw,Bissaka,Maguire,Martial,Pogba,Rashford,McTominay ) wanahitaji kocha wa kuwa-push

Lampard alikuwa anatumia mfumo tofauti na Tuchel kaja na mfumo tofauti lakini progress inaonekana
 
Kwa sasa United ina wachezaji ambao wakipata kocha mzuri timu itasonga mbele ,ukileta kocha ambae ni yes man (like OGS) hiyo rebuild itachukua hata miaka 20.Wachezaji wengi viwango vyao vimebaki pale pale sababu kocha anayewafundisha hakuwa na ubavu wa kuwaeleza ukweli (Shaw,Bissaka,Maguire,Martial,Pogba,Rashford,McTominay ) wanahitaji kocha wa kuwa-push

Lampard alikuwa anatumia mfumo tofauti na Tuchel kaja na mfumo tofauti lakini progress inaonekana
ila wakati chelsea wanatafuta kocha waliangalia wachezaji wao na kutafuta nani ana connection nzuri zaid, Tuchel amemfundisha silva, Rudigger german connection, havertz na werner wajerumani. toka wanatafuta kocha tetesi tayari walikuwa wanataka kocha ambaye atanusuru investment zao, hivyo ilibidi kocha awe angalau anajua kijerumani
source halisi hapa ila ni paid article

nagelsmann alikuwa pia kwenye Shortlist ila sababu Bayern walikuwa na mazungumzo nae hakuja.
 
Aisee hii timu hii,team rebuild imekuwa ni kazi Sana kwetu,kujenga timu ni kazi sanaaa huwa ndo Mana kila siku nawapongeza Sana Bayern Munich wale jamaa wanajua wanachokifanya Tena ni kwa miaka mingi Sana...
Pep aliiharibu Buyern ndio majuzi tu imerudi kwenye ile style yake.
 
Mkuuu nimekuambia uwe unaangalia Ronaldo akicheza kwa jicho la tatu.. Ronaldo ni mzigo kwenye team.. tena mzigo mkubwa.. kama jana amefanya nn cha maana... Ronaldo games zake n za Norwich City.. Newcastle City.. Burnley.. etc
Afanye cha maana kwani anacheza peke yake uwanjani.Timu nzima imelemewa wewe unamwona ronaldo tu.Man hakua na muinganiko wowote ndo maana hakuna move ya maana waliyoifanya sasa huyo ronaldo ataonekanaje.
 
Habari njema sana hizi.
Screenshot_20211026-121052_Instagram.jpg
 
ila wakati chelsea wanatafuta kocha waliangalia wachezaji wao na kutafuta nani ana connection nzuri zaid, Tuchel amemfundisha silva, Rudigger german connection, havertz na werner wajerumani. toka wanatafuta kocha tetesi tayari walikuwa wanataka kocha ambaye atanusuru investment zao, hivyo ilibidi kocha awe angalau anajua kijerumani
source halisi hapa ila ni paid article

nagelsmann alikuwa pia kwenye Shortlist ila sababu Bayern walikuwa na mazungumzo nae hakuja.

So now sababu ni lugha na sio mfumo wa kocha ?

Conte alichukua ubingwa Inter na wachezaji walionekana magalasa hapa United (Young,Darmian,Sanchez,Lukaku) Perisic

Roman yupo aggresive anachoangalia ni perfomance kama usipo-deliver anakufukuza regardleas atakulipa kiasi gani
 
So now sababu ni lugha na sio mfumo wa kocha ?

Conte alichukua ubingwa Inter na wachezaji walionekana magalasa hapa United (Young,Darmian,Sanchez,Lukaku) Perisic

Roman yupo aggresive anachoangalia ni perfomance kama usipo-deliver anakufukuza regardleas atakulipa kiasi gani
Conte pia amespend sana Inter mpaka club ina deni kubwa sana.

Kwa miaka 5 iliopita Conte anashika nafasi ya 3 duniani kwa Spendings kubwa Nyuma ya Pep Na velverde. Amespend Takriban Euro 677 million, Roughly Euro milioni 120 kila msimu, hivyo si kweli kwamba anatumia Magarasa. Amesajili watu Kama Lukaku, Achraf Hakimi, Barella, Eriksen, Vidal, Godin etc wote hawa wapo regarded kama mastaa.

Na Abramovich pia amejitahidi sana kuleta mpira unaovutia Chelsea ila kila kocha wa ushambuliaji anazingua Chelsea kuanzia kina Scolari miaka hio mpaka sarri na Lampard, makocha walioipa Ubingwa Chelsea Uefa ni Di Matteo na Tuchel, ligi wenye Mafanikio ni Mou na Conte, wote hawa ni watu wanaoprioritize defense kwanza kabla ya ushambuliaji, na Ndio DNA ya Chelsea miaka na Miaka ukabaji ndio eneo ambalo Chelsea wanajivuania Kuanzia Makelele Hadi Kante.

Hivyo Mkuu DNA ni muhimu ni vyema kuangalia Strength zetu zipo wapi na aje Mtu kutokana na uwezo wetu.
 
Back
Top Bottom