fuentte
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 3,210
- 9,206
Kwa mtizamo wangu.Nimejaribu kupanga first eleven yetu bila kuangalia fitness na injury..yaani kama tusipo sajili tena our strongest XI itakuwa ndo hiyo..sio kikosi cha kucheza game za ufunguzi za ligi or something.
Swali langu ni kuwa ni kikosi kinachoweza kutupa ubingwa chini ya mbinu za Ole??.
Tatizo la Ole hajawahi kuwa muwazi linapokuja suala la mapungufu ya timu yake kama alivyokuwa Mourinho bali hutoa jibu la pamoja tu kuwa timu imefanya vizuri bila kusemea uwezo wa wachezaji katika nafasi zao. Hivyo inakuwa ngumu kujua kama anaridhika na alichonacho kulingana na mbinu zake au la.
Lakini tumefundishwa kitu tangu ujio wa Bruno kuwa wachezaji wenye kiwango na kiu ya mafaniko ndio wanambeba Ole,hivyo basi kutokana na kundi alilonalo inawezekana akafeli kwa sababu zile zile zilizomfelisha mwaka jana.
.Mbavu ya kulia haipandishi timu
.Kuchezesha Mc Fred Inampunguzia nguvu na idadi kwenye eneo la ushambuliaji.
