Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mata angepitishwa hivi tu, sioni umuhimu wake, kama wazee mbona tunae Cavan anatosha kulea vijana.
hii ishu ya juan mata tulishawahi kuizungumza na PTER humu ndani, kwa ufupi man utd wana mipango naye juan mata baada ya kustahafu soka ila bado haijajulikana ni kazi gani wanataka kumpa.
  1. kocha kama ilivyo kwa michael carrick
  2. balozi wa klabu

hivyo basi uwepo wa juan mata klabuni unatokanwa zaidi na sababu za kiuongozi kuliko sababu za kiuchezaji. Juan mata anaonekana kuwa ni mwanadamu mwenye taswira ya upole, uvumilivu, aliyeridhika, mpinga fitna(hajawahi kuanzisha mgogoro wowote dhidi ya mwalimu), mwingi wa ihsan na ikhlaq nafsini mwake.

Naweza kusema huu ni msimu wa nne kumshuhudia Juan akikosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza lakini sijawahi kukutana na malalamiko yeyote kutoka kwake kupitia media tofauti ukilinganisha na wachezaji wengineo wenye changamoto inayoshabihiana na ya kwake kwa kuanzia utawala wa mourinho ambaye tuliamini havutiwi na uchezaji wa mata (rejea sakata lake pale chelsea) mpaka huu utawala wa Ole gunnar. Si hivyo tu pia juan amekuwa akichezeshwa nafasi asiyoipendelea kiuchezaji tokea asajiliwe manchester united lakini ameendelea kujitolea kwa moyo wake wote pindi anapopewa nafasi.

nimeona vugu vugu kubwa la usajili wa wachezaji vijana kutoka Spain kwa miaka hii ya karibuni kama vile:
  • alvaro fernandez: mlinzi wa kushoto kutoka real madrid na amepandishwa timu ya miaka 23 licha ya kuwa na miaka 17.
  • marc jurado: anatokea barcelona, amezaliwa miaka 16 iliopita
  • armau puigmal: anacheza timu ya miaka 23 (hajaongezewa mkataba mpya hivyo ameshaondoshwa)
  • Mateo Mejia
  • alejandro ganacho: miaka 16 na amesajiliwa kutoka atletico madrid
uwepo wa mata utaweza kuwa ni kichocheo cha kuendeleza huu mkakati wa kusajili vijana kutoka spain, vijana watamchukulia juan kama ni mlezi wao pale Manchester kutokana na uzoefu wake na haiba yake.
 
kazi nyengine ya lee grant ni hii
teh teh teh
1625303848567.png
 
Baada ya De gea kuonyesha decrine,
OLE aliamua kumpa nafasi Henderson ili ajue uwezo wake.
Ndio maana Henderson kacheza mechi za EPL.
Huku de gea kacheza za Europa.

Sasa hapo sioni kosa la OLE, labda wewe ulitaka afanye nini mkuu.??
Jombaa, nafasi ya golikipa #1 kwa sasa haifahamiki ni ya nani kwa Ole. Kuna tetesi za chini zinasema kuna uwezekano wa mmoja kuondoka kati Dean au David, japokuwa issue kubwa kwa David hakuna anaweza kumlipa mshahara wake na amebakiza miaka miwili. Na ndio maana Heaton kasajiiwa kama golipa #3.

Nafasi golikipa sio ya kujaribiwa. Ole anapaswa aonyeshe wazi wazi golikipa wake #1 ni nani, unapofanya michezo ya mmoja akibokoa mchezo huu mwingine anachukua nafasi yake mchezo ujao hii kitu inawashusha hali ya kujiamini baina yao. Binafsi, napenda Dean awe ndio mlinda mlango mkuu, ana kiu ya kufanikiwa kuliko David aliyeshinda mataji mengi.
 
Me mwenze huyu mwamba sijawahi kumuona langini hata siku moja.
Hata mwaka tulio msajili siujui, sijui tulimsajili kutoka Club gani, yani naishia kumuona mitandaoni tu.

Hawa wanaandaliwa kuwa watumishi wa timu wa muda mrefu ndio maana wanapewa mikataba manchester united ilivurugika sana baada ya kocha wa kudumu kustaafu kwa hiyo hizi taratibu zinaandaliwa kwa utaalam sana unaona wakina mata wanapewa mikataba miaka ijayo utawasikiwa wapo kwenye under 17 huko wanafundisha
 
Nje ya mada,,,,,,,,,,, Jamani wananchi leo wamenifurahisha.
Sifatilii ligi ya Bongo lakini likija swala la Simba vs Yanga lazima niache kazi zangu na kuifuatilia hiyo game.
Kwakweli Yanga naipenda mpaka kumoyo, sema soccer la kibongo ndio la kisenge.
Asanteni wananchi leo mumenifurahisha.
 
A typical Manutd assist

Luke Shaw picks a loose ball and crossed to Harry Kane who heads a third goal....

Can England win this game without Manutd Luke Shaw? We seriously doubt


Ukraine 0-3 England 2nd half.
 
Sancho mmepigwa kweupe kabisa, yaani goli 4 hakuna ata assist moja
 
Back
Top Bottom