nakumbuka katikati ya msimu wa 2018/2019 humu ndani kulizuka mjadala mkubwa sana uliojaribu kuangazia au kuonyesha ni upi upande sahihi ambao mashabiki wa manchester united wanapaswa waegemee kwa muda.
- wengine tulitaka bingwa awe liverpool bila ya kujali historia kubwa ya kiupinzani iliopo
- wengine walitaka bingwa awe manchester city licha ya kwamba hawa pia ni wapinzani wetu (wanaonekana kuwa ni wapinzani dhaifu kihistoria ya mafanikio)
kwa nini liverpool awe bingwa: Nilielekeza hoja zangu maeneo yafuatayo
- squad depth ya liverpool ni dhaifu hivyo basi hawatokuwa na nguvu ya kuleta ushindani kwa misimu miwili hadi mitatu kwa wachezaji walionao, itakuwa ni rahisi kuwaondoa kileleni pindi tutakapokuwa serious kwa soka la ushindani.
- FSG wanafanana na familia ya glazer kimatumizi na uendeshaji wa timu hivyo niliamini liverpool hawatokuwa na jeuri ya kufanya usajili wa nguvu kwa kila msimu ukilinganisha na manchester city
- aina ya wachezaji anaowapenda klopp ni wale wasiotambulikana kwa kiasi kikubwa sana kwenye soka la bara la ulaya(mwenyewe hujificha kwenye hoja ya mfumo), tofauti na guardiola anayevutiwa zaidi na top players waliokwisha tengenezwa huko watokwako.
kwa ufupi sikutaka kuwa mtumwa wa historia za wazungu na kwangu niliangalia zaidi nyakati tulizopo, man city nilianza kuwaogopa tokea siku ile waliofanikisha usajili wa
robinho kutoka real madrid na baadae
yaya toure kutoka barcelona
Siwezi kumuogopa
klopp asiyekuwa na uhakika wa bajeti ya usajili huku nikiendelea kumuombea mazuri guardiola mwenye uwezo wa kumsajili
athan ake kwa paundi millioni 40.
====================
fuentte, Bello na wadau wengineo niliowasahau bado munaendelea kuwa na msimamo wa kuwaombea mazuri zaidi manchester city kuliko liverpool hii inayosajili mchezaji wa daraja la kwanza?