So mpira umedunda!!?Leo man u asiposhinda kayataka mwenyewe. Game ya leo hata kama kocha hana mbinu wachezaji wanaweza kufosi na kulazimisha matokeo.
So sioni cha kujadili. Game man u anashinda ni swala la ngapi na jinsi gani atasecure ushindi.
Akifungwa itakua ni mambo ya Shakhtar na Real, Alaves na Barca na Locomotiv Moscow na Atletico.
Acha tuone kama mpira utadunda.
Man kamilikia mpira kwa zaidi ya 60% ila amepiga mashuti saba. Wenyeji kwa kumiliki mpira asilimia 37 wamepiga mashuti 6.
Timu nyingine ambayo inamiliki mpira ila haipigi mashuti mengi ni Arsenal, kwanini? Kwa sababu haina AM so inastruggle kupeleka mpira kwa wapiga mashuti na scorer ni mmoja tu.
Juzi Barca wakati anadraw na Alaves alimiliki mpira na alipiga mashuti zaidi ya 15.
Sasa swali; Man U haina AM? Haina scorer? Huu siyo mpango wa wachezaji kumfukuzisha kocha?
Steven Gerrard alijikosesha penati.
Arsenal ilisusa kuperform Europa.
Man u ikamsusia Jose.
The list goes on and on, Ole kashafikishwa huko au uwezo wake halisi ndiyo huu? Wiki kadhaa nyuma alisema fitness ni tatizo huu wimbo kuna member aliukariri bila hata kujiuliza. Baada ya games na PSG na RB akasema niliwaambia tatizo ni fitness sasa tunaanza kazi.
Anyway, chansi ya kufight bado mnayo kazeni unless kama wachezaji wanaconspire against Ole.