Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Karibuni kwenye #VPN PARTEY 😂😂😂
IMG_20201101_220140.jpg
IMG_20201101_220140.jpg
 

Attachments

  • IMG_20201101_220140.jpg
    IMG_20201101_220140.jpg
    88.4 KB · Views: 8
Huyu kocha kwakweli mm sina imani nae kabisa ni mbahatishaji mno hamna kocha humu, yn ana uwezo mdogo sana kwakweli, badala atoe pogba aingize Donny anatoa Bruno badala atoe Rashford aingize Cavani anatoa Greenwood, hzo ni sub nyepesi kabisa hata mm nmeziona kadri mchezo ulivyokuwa unaendelea.

So mm kuanzia leo sina imani kabisa cz nshamuona ana bahatisha tuu na hatutafika popote na kocha huyu, hayo ni mawazo yangu cwezi kumlazimisha mtu kuamini ninachoamini mm japo Ole atabaki kuwa legend ila kwenye ukocha HAPANA.
Inauma sana kuona mimi ambae sijawahi fundisha ata team ya familia naona tatizo kabla hata game haijaanza ila kocha hajaona
 
Ole bhana

Pogba amechoka naongea na jamaa pembeni, nasema Pogba atolewe... mara paap TUTA (msimu huu Pogba anasababisha TUTA mara ya pili kizembe tu)

Halafu anakuja kumtoa Bruno (ambaye muda wowote anasababisha kitu) na kumwacha Pogba ambaye ana ball dance nyingi kuliko kufanya kitu uwanjani
OLE ni big fala.....
 
Mimi binafsi Fred asingekuwa na kadi ya njano hakupaswa kutoka, ila nilisapoti kutoka sababu ya muda wowote angeweza kula umeme (Mike Dean sio mtu mzuri)

Kwenye sub ya Fred kutoka na Cavani kuingia pia ni wazo uzuri ukizingatia tulikuwa tunahitaji goli shida inakuja kwa Ole anapokutana na timu kubwa kipaumbele chake cha kwanza angalau apate hata point 1

Pogba alichoka, huwa yupo reckless sana kwenye ukabaji especially maeneo kama ndani ya 18. Bruno pia alichoka, lakini uzuri wa Bruno anaweza kuwa off dakika 85, lakini dakika 5 akafanya jambo

Watu wataendelea kumponda Ole sababu ya makosa kama haya

Ninahisi Pogba asingesababisha penati, Ole angemtoa yeye. Ila kumtoa baada ya tuta ungeweza kuonekana anamtoa sababu ya kutoa boko. Kiujumla Pogba ilibidi atolewe kabla hata ya tuta, maana alionesha kuchoka mapema tu
Sure lakini pia heri angeingia Daniel James upande wa kushoto mara nyingi ulikuwa wazi tu au Rashford angehamia kushoto.
 
Back
Top Bottom