Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kama tulivyoongea hapo juu mkuu, tatizo ni fitness level tu.

Chukulia mfano Pogba tumemaliza Msimu, Ameumwa Corona alivyopona Ligi imeanza, Hata mazoezi hana unategemea nini?

Hebu tuangalie kwa Mifano Finalist wa Ulaya Msimu uliopita.

1. UEFA NI Bayern na Psg.
-Psg kafungwa mechi mbili mfululizo, kikawaida kwenye ligi yao ya wakulima ni Nadra PSG kufungwa nini kimempata?
-ninavyoandika Hapa Bayern kashatandikwa 3 mechi inaendelea kwanini?

2. Europa Sevilla na Inter
-Sevilla kapoteza Mechi 2 zilizopita kapigwa mpaka na Bilbao
-inter kacheza mechi 1 tu Serie A ameshinda ila tayari Ameruhusu Goli 3

Semi finalist kuna
-lyon mechi 4 zilizopita kashinda moja tu
-Rb lepzig mechi 4 kashinda 2 tu
-shaktar mechi 3 zilizopita kashinda 1 tu.

Je mkuu ni coincidence hii? TIMU ZOOOTE zilizofika Nusu ama Fainali ya Mashindano ya Europa ama EUFA zinafanya vibaya?

Jibu ni Rahisi tu, Fitness level ni Ndogo, wengine wamepumzika muda mrefu na Kujiandaa, waliofika mbali Uefa wamepumzika muda mfupi na hawajajiandaa.
Napenda sana jinsi unavyoweka fact hadharani
Wengi wamezoea blah blah tu
 
Sio VAR kuna baadhi ya sheria zimefanyiwa marekebisho ikiwemo ya mchezaji kushika ,msimu huu penati zitakuwa nyingi sana kutokana na hayo mabadiliko so kila mtu itafika zamu yake

Timu nyingi sana zimeshapata penati licha ya kucheza game chache

Sent from my Redmi 8A using JamiiForums mobile app
Wengi hawajui hii
Now mpira ukigusa mkono ni tuta hakuna ball to hand wala hand to ball
Ukishika umeshika
 
Chief-Mkwawa,

Safi sana. Nimependa sana your smart 'observation' japo sio directly conclussive proven fact ila kuna kitu kikubwa sana umeongea, nimegundua kilichofanya tucheze hovyo hizi mechi tatu za mwanzo japo tumeshinda mbili (Luton, Brighton) ni match fitness kwangu mimi nilimuangalia Paul zaidi ila kiujumla timu nzima iko chini sana. Binafsi nimeona mapungufu mapya makubwa zaidi benchi la ufundi halina contingency plan hasa hasa ktk vipindi vigumu hata msimu uliopita huwa hawawezi kucheza bila kikosi cha kwanza na kupata matokeo pia hata game plan tunaingia na moja tu ukitushika umetufunga.
 
Kwa zile hela mlizoweka mzee baba mnagombania drooo daaaa maisha yanaenda kasi sana
Wachezaji wamesajiliwa juzi tu hapa. Tulia hivyo hivyo, kikosi chenu mko tangu msimu uliopita bado nategemea kushinda kwa penati, mnashinda baada ya Refa kupuliza kipenga cha mwisho😂😂
 
Nimeshangaa sana jana Chelsea kushangilia sare kwa Westbrom, hii maana yake hawa jamaa ni wabovu sana msimu huu pia. Huwezi kufurahia sare kwa timu ndogo wakati umetumia zaidi ya pound 150M sokoni msimu huu mpya. Msimu huu timu nyingi ndogo zitawasha sana moto kwa wakubwa wakiongozwa na Leeds sasa kama wameanza kushangilia mapema kwa Westbrom wawasubiri Leeds na Everton.
 
Back
Top Bottom