DEMBELE KUTUA MANCHESTER UNITED
Manchester United wapo katika mazungumzo na miamba ya soka Barcelona juu ya uwezekano wa kufanikisha kumsajili, Ousmane Dembele.
[
https://res]
Kwa mujibu wa Daily Record, vigogo hivyo vya soka kutoka Premier League wanamuhitaji Mfaransa huyo kwa mkopo huku Barcelona wanachohitaji wao ni kutaka kumuuza moja kwa moja kwa dau lenye thamani ya euro milioni 100.
Inadaiwa mpaka sasa uongozi wa Old Trafford akiwemo Ed Woodward wameshafanya mazungumzo na upande wa pili wa Barcelona juu ya uwezekano wa kumnasa nyota huyo.
My Take: Huyu naye tutaishia hivyo hivyo tu kuzungumza naye zen tutashindwana kwenye malipo, cz tunamtaka kwa mkopo ila barca wanataka mpunga.